Mwarabu fighter kafungua kampuni yake ya ulinzi

Mwarabu fighter kafungua kampuni yake ya ulinzi

Jamaa ameona fursa kupitia umaarufu wa jina lake. Ni aibu kwa mtu mwenye jina kubwa katika jamii au mwenye umaarufu kuwa masikini. Umaarufu ni utajiri. Mimi nashangaa sana mtu unafahamika na watu zaidi ya laki moja halafu unalia njaa how come? Yaani umekosa kubuni kitu ambacho utakitumia kuchota pesa kwa watu hao laki moja?
Kuna msanii mmoja anaitwa Shilole,huwa kuna muda wengine wanamuonaga kama 'fyatu' lakini ana akili vibaya mno ya kutafuta pesa na kupiga hatua katika kila kitu.

Ametumia umaarufu wake sasa nasikia anapika na anauza vyakula safi tu.
 
Aliyewahi kuwa mlinzi wa msanii mkubwa diamond pltinumz amekuja na kitu kipya baada ya kuachana na kazi ya ulinzi katika kundi la WCB na kupata ajali mbaya iliyotaka kusababisha kuondoka na uhai wake.Mwarabu fighter ambae ameamua kuja na idea mpya ya kuanzisha kampuni yake ya ulinzi anasema kuwa inaweza kuwahudumia watu wote ikiwa ni kikundi au mtu mmoja mmoja.

Katika ukurasa wake wa instagram, Mwarabu fighert aliandika “Dear god please , bless the work of my hands.nilikiona kifo lakini ukanipa nafasi nyingine tena.mtanzania mwenzangu , hii ni kazi yangu na vijana wenzangu, nitasema na kufanya kweli daima fitina kwangu ni mwiko.upigie sima kwa mahitaji ya usalama wako binafsi,harusi, matamasha na nyumbani na popote ulipo , unapohitaji usalama.

Mwarabu Fighter hapo awali alikuwa akifanya kazi na Diamond Platinumz lakini kibarua kilikuja na kuota nyasi huku hgakuna aliwahi kutoa sababu ya yeye kuacha kufanya kazi na msani huyo.
Noted mkuu
 
Oooh!, Well done brother. Ndivyo inavyotakiwa vijana wote kuona fursa

I salute him!, badala ya kulia lia yeye kafanya kweli...safi sana
 
Huyu atapiga pesa,
Kuna jamaa huko state alianza kimchezo mchezo na kampuni ya Blackwater,
Leo hii,vijana wake wanakodiwa na serikali ya marekani,kuwalinda askari wa marekani katika maeneo hatari kama Iraq,afaghnistan,etc.
Na kisha kuwa bilionea mkubwa tu
Fursa hiyo kibongo bongo atapata wateja
 
La muhimu afanye kazi kwa kuzingatia Weledi atapata sana Pesa na Kazi nyingi.
 
Huyu atapiga pesa,
Kuna jamaa huko state alianza kimchezo mchezo na kampuni ya Blackwater,
Leo hii,vijana wake wanakodiwa na serikali ya marekani,kuwalinda askari wa marekani katika maeneo hatari kama Iraq,afaghnistan,etc.
Na kisha kuwa bilionea mkubwa tu
Unajua jamaa wa black water ni former special forces operator. Yeye mwenyewe ni former seal. Tatizo ni kupata vijana wenye background ya nzuri ya mafunzo ya kijeshi au uwanja vita hapa tz ni ngumu kidogo.

Ila wapo wachache... jamaa atafika mbali.
 
Inategemea. Da'Mange ana followers kibao Insta akaona aanzishe app yake lakini aliangukia pua.
App hata wewe unaweza fungua, kwani inagharimu Nini, tatizo serikali yako ilimletea figisu kupitia TCRA....kwani mange amekosa Nini...
 
Back
Top Bottom