Mwelekeo wa Ndoa yangu umefikia pabaya sana

Mwelekeo wa Ndoa yangu umefikia pabaya sana

Unaonea huruma watoto wako, wakati hata wewe ni mtoto wa watu.
Kina wakati kuishi na watu wasio sahihi kwetu ni kitanzi cha kurudisha nyuma maendeleo ya uchumi wa familia.
Fika sehemu, fanya maamuzi magumu hakikisha watoto unaishi nao.
Pia angalia sana huyu wa pili mwenye kukujali sana, Siku atakayoingia ndani, utakuja kukuta yeye sasa ndio Lucifer mwana wa yezebeli
 
Sasa situation uliyojiweka ndio utakoma. Utajuta nakwambia.

Unaona huruma kumuacha mama mtoto wako wa kwanza sababu ana watoto wako 2 na unapenda wanao walelewe na wazazi wote wakiwa pamoja sasa na huyo mpya unaeenda kumzalisha huyo mtoto wako utafanyaje? Utaishi nae?

Oa wote wawili watajiheshimu.

Wanasemaga ukitaka kumuua mbwa unampa jina baya, na ndo unachofanya mkubwa. Wewe lengo lako ni kumuoa huyo mchepuko wako haya ya kusema sijui wife kafanya hiki mara hiki ni kumtafutia chochoro ya kumuacha tu. Hivi we kwa akili yako mkuu unaamini kabisa hayo mahaba anayokuonesha mchepuko wako sasa hivi ndo ataendelea hivyo hivyo hadi milele ukimuoa? Pole sana.

Hata hivyo, yawezekana my wife wako ana stress za kumzalisha watoto na kuishi nae miaka kadhaa bila ndoa

All in all, cheza karata zako vizuri. Umeshafanya kosa kubwa kumpa mchepuko mimba! Hili lijue tu
Aisee nimelia
 
HABARI wakuu, kwanza kabla ya yote niwatakieni mfungo mwema.

Umri wangu ni Miaka 33, Nipo katika ndoa pia nina Watoto Wawili na huyu mwanamke, naona nisiandike Mengi kuhusu maisha yangu na huyu Mwanamke ila kimsingi tu ni MTU ambae ninapitia changamoto nyingi sana katika mahusiano haya, yaani kiufupi tu hata sielewi mwelekeo wa ndoa hii, Tulikutana nae tukachukuana nae Tukaamua kuishi pamoja hadi sasa tuna watoto wawili, lakini sijamtolea mahali, lakini sio kwamba sina uwezo wa kutoa mahali ila kinachonichelewesha ni aina ya maisha ambayo tunaishi nae.

Yaani siku za furaha ni za kuhesebakika kuliko siku za kununiana, ana vijisababu visivyokuwa na mashiko anajinunisha, Mara utastuka usiku unamkuta MTU amekaa kitandani analia bila sababu, Mara atoke akae jikoni usiku, Mara ajidai amepandisha presha nianze kumpepea usiku yaani ni mateso bila ya kifo.

Kimaisha siko vibaya ninamtimizia kila hitaji pia ninakaa kwangu sijapanga na Mimi ni mtu wa kutoka asububi narudi jioni kutokana na aina ya harakati zangu zinazoniweka mjini, sasa kulitokea kasumba Kikitokea kimgogoro kidogo ananinyima unyumba, hadi inafkia mda unazuka ugomvi ndo napewa huwa nawaza namna ya kuachana nae, ila nawaonea huruma sana wanangu, pia hata yy namuonea huruma, maana nishamzalisha watoto Wawili wote alafu nimuache huwa kimsingi naishi nae kwa sababu ya huruma, pia kwa sababu ya kuwaonea huruma wanangu nilitamani wanangu walelewe na wazazi wao ila mwelekeo wa Maisha haya sijajua hatima.

Tangu mwezi wa Pili kuna shida ilitokea nikawa nanyimwa unyumba hadi ikafikia hatua nikakosa namna ikabidi nianzishe uhusiano na mtu mwingine ila kibaya nilianzisha kama njia ya kumaliza haja zangu nikirudi nyumbani najilalia zangu maana sikutaka ugomvi wa kutaka mbususu kwa wife ila kibaya naona nimezama mazima yani huyu mtoto anajua kucare, anajali kiufupi ninapata kila kitu ambacho nilikuwa nakosa awali, lakini kibaya zaidi na bahati mbaya kwa sasa huyu Mtoto ana ujauzito wangu, hapa nipo njia panda.

Kusema kweli ingekuwa uwezo wngu ningemuoa huyu mtoto maana kimsingi mke ninaekaa nae ameshindwa kutambua thaman yangu, lakini kila likija swala la wanangu huwa naishiwa nguvu maana siwezi kuruhusu wanangu kukaa mbali na Mimi pia sina imani kama mwanamke huyu ataishi na wanangu vizuri mda ambao Mimi sipo, kusema kweli najikuta naishi katika majuto niliingiaje 18 za huyu mwanamke! Na ni namna gani nitaepuka hili.

Pia kuhusu suala ya yeye Pengine ana mahusiano mengine siwezi jua na huwa sina asili ya kifuatilia maisha yake maana nipo bize sana na pia huwa sitaki kabisa kufanya kumfuatilia maana matokeo ya kumfuatilia MTU siku zote hayawi mazuri.

Kibaya zaidi ni kuwa jamii tunayoishi nayo inatuona tuko vzuri maana mchana tunaigiziana ila ikifika usiku hakuna MTU anamsogelea mwenzie.

USHAURI WENU MUHIMU
Inawezekana kuna mambo ameyajua/ ameambiwa ndio yanayomfanya awe na mawazo, kwa kipindi hiki cha sasa ambapo mwanamke anaambiwa ambiwa tu kuwa amefungwa na watu wa 'dini' kinawapa shida sana. Kinawafanya usiku wanaamka na presha, wananuna nuna, wanaona wengine wote ni wakosaji. Pengine ameambiwa na wanawake wenzake. Akiwa nje ataonesha tabasamu sana (kisaikolojia mtu anayeonesha maisha yake ni mazuri nje ujue ndani kuna kitu). Hapa ianbidi umuulize vizuri kinachomtatiza, kinachompa shida ya moyo.
.
Upande mwingine ni wewe mwenyewe, inawezekana kuna sehemu ulianza kutetereka kuwa mwanaume wa kumuongoza. Kuna sehemu apo umesema humfuatilii kabisa, kiukweli (haijalishi wanawake wa kisasa wanasemaje) wanawake wanahitaji mtu wa kumuongoza, mtu wa kumuambia hiki hapana, asipopata hayo huishia kuwa na kinyongo kwa mwanaume wake na kuanza kumletea vituko. Kama zamani mlikua mpo vizuri jaribu kukumbuka ni kuanzia wapi mambo yalienda mrama ili alafu angalia nini uliacha kufanya, inawezekana ni kwamba haupati muda naye wa kutosha kiasi akaona unamchukulia poa tu kisa ushamzalisha na hujamtolea mahari.
.
Kujumuisha yote hayo, anza kumuwekea mipaka, mfuatilie kidogo tu kumuonesha kuwa unamjali. Mpe muda ikiwezekana safiri ila muache vizuri, mshirikishe kuwa ungependa mtafute suluhisho ila kama mambo yanaendelea kuwa mabaya, maisha ni mara moja tu mzee, furaha yako ni ya muhimu.
.
Pia unaposema huyo wa nje unatamani ungekua naye, ingekuaje kama huyo wa nje mngefikia kwenye hii tabu uliyonayo na huyo wa ndani, je, ungeenda kutafuta wa nje mwingine au ungetafuta suluhisho?
.
Mi mtazamo wangu, watoto ni jambo jema lakini hawatakiwi kukufunga kufanya maamuzi kwa ajili ya furaha yako, sababu kama huna furaha kwasababu ya watoto watoto watakuaje na furaha kwako?
 
HABARI wakuu, kwanza kabla ya yote niwatakieni mfungo mwema.

Umri wangu ni Miaka 33, Nipo katika ndoa pia nina Watoto Wawili na huyu mwanamke, naona nisiandike Mengi kuhusu maisha yangu na huyu Mwanamke ila kimsingi tu ni MTU ambae ninapitia changamoto nyingi sana katika mahusiano haya, yaani kiufupi tu hata sielewi mwelekeo wa ndoa hii, Tulikutana nae tukachukuana nae Tukaamua kuishi pamoja hadi sasa tuna watoto wawili, lakini sijamtolea mahali, lakini sio kwamba sina uwezo wa kutoa mahali ila kinachonichelewesha ni aina ya maisha ambayo tunaishi nae.

Yaani siku za furaha ni za kuhesebakika kuliko siku za kununiana, ana vijisababu visivyokuwa na mashiko anajinunisha, Mara utastuka usiku unamkuta MTU amekaa kitandani analia bila sababu, Mara atoke akae jikoni usiku, Mara ajidai amepandisha presha nianze kumpepea usiku yaani ni mateso bila ya kifo.

Kimaisha siko vibaya ninamtimizia kila hitaji pia ninakaa kwangu sijapanga na Mimi ni mtu wa kutoka asububi narudi jioni kutokana na aina ya harakati zangu zinazoniweka mjini, sasa kulitokea kasumba Kikitokea kimgogoro kidogo ananinyima unyumba, hadi inafkia mda unazuka ugomvi ndo napewa huwa nawaza namna ya kuachana nae, ila nawaonea huruma sana wanangu, pia hata yy namuonea huruma, maana nishamzalisha watoto Wawili wote alafu nimuache huwa kimsingi naishi nae kwa sababu ya huruma, pia kwa sababu ya kuwaonea huruma wanangu nilitamani wanangu walelewe na wazazi wao ila mwelekeo wa Maisha haya sijajua hatima.

Tangu mwezi wa Pili kuna shida ilitokea nikawa nanyimwa unyumba hadi ikafikia hatua nikakosa namna ikabidi nianzishe uhusiano na mtu mwingine ila kibaya nilianzisha kama njia ya kumaliza haja zangu nikirudi nyumbani najilalia zangu maana sikutaka ugomvi wa kutaka mbususu kwa wife ila kibaya naona nimezama mazima yani huyu mtoto anajua kucare, anajali kiufupi ninapata kila kitu ambacho nilikuwa nakosa awali, lakini kibaya zaidi na bahati mbaya kwa sasa huyu Mtoto ana ujauzito wangu, hapa nipo njia panda.

Kusema kweli ingekuwa uwezo wngu ningemuoa huyu mtoto maana kimsingi mke ninaekaa nae ameshindwa kutambua thaman yangu, lakini kila likija swala la wanangu huwa naishiwa nguvu maana siwezi kuruhusu wanangu kukaa mbali na Mimi pia sina imani kama mwanamke huyu ataishi na wanangu vizuri mda ambao Mimi sipo, kusema kweli najikuta naishi katika majuto niliingiaje 18 za huyu mwanamke! Na ni namna gani nitaepuka hili.

Pia kuhusu suala ya yeye Pengine ana mahusiano mengine siwezi jua na huwa sina asili ya kifuatilia maisha yake maana nipo bize sana na pia huwa sitaki kabisa kufanya kumfuatilia maana matokeo ya kumfuatilia MTU siku zote hayawi mazuri.

Kibaya zaidi ni kuwa jamii tunayoishi nayo inatuona tuko vzuri maana mchana tunaigiziana ila ikifika usiku hakuna MTU anamsogelea mwenzie.

USHAURI WENU MUHIMU
Tafuta sukuhu ya tatizo lako la kupoteza hisia nae na kushindwa kushiriki vema tendo la ndoa naye. Mwanamke kama humfilishi kileleni hawezi kukuheshim. Tafuta tiba
 
Back
Top Bottom