Mwenye sample ya talaka tafadhali

Mwenye sample ya talaka tafadhali

nashukuru kaka kwa kuwa concerned na kuwa na kumbu kumbu nadhani sio kila mwanume anafaa kuitwa mume mi nafikiri nimechemsha tatizo langu ni upole if you remember that post nilisema kuna mengi ila nilikuja na lile nikamwelewesha kwa upole alichonijibu ni siri yangu,imagine tangu nimeoa nimekonda badala ya kunenepa kwa sababu hapiki anamuachia dada mimi hupenda kula chakula kizuri sasa dada sio mpishi mahiri,hajawahi hata kupika chai,sio mjuzi wa kupika na hataki kujifunza
2.tendo la ndoa miezi minne sasa sijapata
3.akitoka kwenda misele haagi
4.hajawahi kunifulia au kupiga pasi japo mara moja
5.hasafishi chumba cha kulala
6.simu zake zina password
7.siri za ndani anatoa nje kwa majirani na kwa ndugu zake
8.ana mawasiliano na jamaa ambaye tuliwahi kugombea mwanamke kabla hatujaoa
9.maji ya kuoga hajawahi kutenga hata siku moja
10.akipewa kitu na mwanamme ananionyesha na kuniambia waziwazi
11.haendi kwenye nyumba za ibada
12.usafi wa nyumba hauridhishi
13.ana majibu makali yanayoweza kukufanya ukazimia
14.marafiki zake wote ndoa zimewashinda
mengine nitaongezea baadae ngoja nikumbuke

Nasikitika kukuambia kuwa kuna mwanaume mwenzio ambaye anadai huduma zote ulizotaja hapo juu ila hawajibiki kwa lolote katika familia yake ili hayo yaweze kutimia.
1. Eneo analoishi wanatakiwa kununua maji hanunui maji kwa matumizi ya familia yake yakufua
nguo zake yatatoka wapi?
2. Simu zake ziko wazi ila hazionyeshi mawasiliano yake ya siku kwa siku, yaani hana missing
call wala received call wala sms mpya labda inayotoka kwa mkewe.
3. Yeye haendi kwenye nyumba za ibada muda wote ni kulala na kulalamika
4. Hatoi zawazi yoyote kwa mkewe wala mtoto
5. Matusi ya kutukana ukoo mzima pale manapogombana na kuhita mke malaya. Mwanamke wa aina hii
atakuwa na hamu ya kumpa unyumba/
6. Hajuhi ada ya mtoto wala vaa yake.
Na mengine mengi
 
kivipi mkuu?

i-miss-you.jpg
 

[TD="class: content, width: 614, bgcolor: #1E3D70"]
III. AINA ZA TALAKA
[/TD]
[TD="width: 106, bgcolor: #1E3D70"][/TD]

[TD="class: content, width: 614"]

[TD="class: content, width: 547"]

[TD="class: content, width: 609"] Wanazuoni-Allah awarehemu-wameigawa talaka katika mafungu mawili makuu; Talaka Rejea na Talaka – Baini. Na hili fungu la pili (Talaka – Baini) linagawika pia katika sehemu mbili; Talaka Baini Sughraa na Talaka Baini Kubraa kama utakavyo ona katika ufafanuzi ufuatao:
  1. TALAKA REJEA: Hii ni ile talaka ambayo isiyo ondosha hukumu za ndoa na wala haiondoshi milki ya mume. Bali uhusiano wa ndoa huendelea kuwepo maadam mtalaka (mke) yungali edani, hapo kunamuelea mume mtaliki kumrejea ndani ya eda hiyo bila ya muafaka kutoka kwa mtalaka wala ndoa mpya. Iwapo hakumrejea hata eda ikamalizika, bila ya shaka atapambanuka nae na wala hamiliki tena kumrejea ila kwa radhi yake (mtalikiwa) na kwa ndoa mpya kwa mujibu wa taratibu zote za kisheria.
Na Talaka – Rejea hii hutuka kwa matamko ya talaka yenye kufumbuliza katika kufahamisha talaka, nayo ni yale matamko yote yanayo chimbuka kutokana na kitenzi “TWALAQA – AMETALIKI”. Mithili ya mume kumwambia mkewe: “Wewe ni mtalikiwa” au “nimekutaliki” au “Wewe ni mwenye talaka” au “i juu yangu talaka”. Na wala kutuka kwa talaka kwa matamshi haya na mfano wake miongoni mwa matamko fumbulizi, hakuhitajii nia. Bali talaka hutuka kwa matamshi hayo bila ya kuwepo haja ya nia kutoka kwa mume, bali lau atadai mtaliki (mume) kwamba yeye hakukusudia talaka, hatokubaliwa wala kusikilizwa. Naam, kama hivi na kwamba Talaka Fumbulizi inakuwa Rejea, iwapo ni talaka ya kwanza au ya pili. Ama ya tatu, hapana rejea baada yake mpaka mwanamke mtaliki aolewe na mume mwingine. Hii ni kwa sababu talaka hiyo ya tatu inampambanua mwanamke na mwanaume huyo “Bainuuna Kubraa” kama lijulikanavyo hilo kisheria.
  1. TALAKA BAINI SUGHRAA: Hii ni ile talaka ya kwanza na ya pili ambazo mume huzitoa kwa kutumia mojawapo ya matamko ya “Kinaaya” – Fumbo, pindi atakapo nuia talaka kwa tamko fumbo hili. Tamko Kinaaya la talaka ni pamoja na mume kumwambia mkewe wakati wa ugomvi: “Nenda kwenu” akikusudia talaka kwa tamko hilo na hutuka talaka hiyo kuwa ni “Talaka Baini”.
Na hukumu ya aina hii ya talaka ni kwamba talaka hii inaondosha hukumu za ndoa pale pale na unyumba haubakiwi na athari yo yote zaidi ya eda. Kwa hivyo basi, hawawezi kurejeana ila kwa kifungu kipya cha ndoa kwa mujibu wa sheria.
  1. TALAKA BAINI KUBRAA: Hii pia huitwa kwa Istilahi za Kifiq-hi “Talaka Batti” – “Talaka ya kukata” nayo ni ile talaka ya tatu. Na hukumu ya talaka hii ni kwamba inaondosha pale pale milki ya ndoa na uhalali vyote pamoja. Mke mtalikiwa hawi halali tena kwa mumewe mtaliki huyu mpaka aolewe na mume mwingine, halafu amuache na eda imalizike. Baada ya yote hayo, ndipo kunamjuzia mume wake huyu wa awali kumuoa upya kwa ndoa ya kisheria na kwa kufuata taratibu zote husika.
Na hapa tunapenda kuitumia fursa hii kuwatahadharisha waume ambao hukithirisha kuacha dhidi ya wayatendayo kinyume na hukumu za sheria. Wenye kuzitumbumkiza nafsi zao na familia zao katika majanga na taabu zinazo kuwa mzigo lemavu juu yao. Sote tunajua ada ya kuacha acha imeenea na kutapanyika katika miji mingi hivi leo kwa sababu ya kuenea kwa ujinga. Hakika mshahara wa ujahili wa majahili hawa na kulinda familia na kuchunga haki za wanandoa, hauwi kwa kutunga sheria/kanuni nyepesi katika masuala binafsi. Wala kwa kufuata/kutumia kauli za baadhi ya maulamaa ziwe ni dhaifu au zina nguvu zinazo tolewa kwa hoja ya kulinda familia. Bali kwanza utengenefu huwa kwa kuzitengeneza nafsi zilizo fisidika na kuwafundisha majahili hawa hukumu za dini. Na kuwakemea wanao chezea hukumu za sheria kwa kuzembea majukumu na amana waliyo pewa na uma. iv. Kuhalalikiwa na mtalaka talaka tatu: Tunacho kimaanisha kwa mas-ala haya, ni kuhalalika mwanamke aliye achwa talaka tatu (Talaka Baini Kubraa) kwa mume wake kwa kwanza. Na uhalali huu hupatikana kwa kuolewa na mume mwingine, kama alivyo sema Allah Taala: “NA KAMA AMEMPA TALAKA (ya tatu) BASI SI HALALI KWAKE BAADA YA HAYO MPAKA AOLEWE NA MUME MWENGINE. NA AKIACHWA (na huyo mume mwengine), BASI HAPANA UBAYA KWAO KUREJEANA WAKIONA KUWA WATASHIKAMANA NA MIPAKA YA ALLAH. NA HII NI MIPAKA YA ALLAH ANAYO IBAINISHA KWA WATU WANAO JUA”. [2:230]
Hukumu ya kisheria inayo patikana ndani ya aya hii ni kwamba mwanamke aliye achwa “Talaka Baini Kubraa” (talaka tatu), anahalalika kwa mume wa kwanza. Pale itakapo malizika eda kwa mume wake wa sasa aliye muoa baada ya kuachwa na yule wa kwanza, kisha nae akamtaliki. Na hii ndoa ya pili inayo muhalalisha muachwa wa talaka tatu kwa mume wa awali, ni wajibu makusudio yake yakawa ni dhati ya ndoa na isiwe kutafuta uhalali kama wafanyavyo watu majahili wanao ichezea sheria ya Allah. Ikiwa ndoa hii lengo lake ni kuhalalisha, atapata dhambi aliye kusudia hivyo.
[/TD]
[/TD]
[/TD]
 
Uko sahihi makamee ila Tanzania, mamlaka ambayo inatoa talaka ni mahakama pekee. Hakuna cha mume kuacha

Zipo talaka pia nje ya mahakama,Tamko ama andishi analolitoa mume na zinakubalika kua ni talaka ndoa huvunjika.(kwa ndoa za waislam).
 
Hahahah!!!

Nahisi ni wewe mkuu ulikuja hapa last time...

Last time nilikuambia kuwa wewe mwanaume hiyo ndoa yako umesingiziwa, huna stamina ya kuitwa mume...

Ona sasa unataka kumuacha mkeo, na bila shaka kisa ni ile habari ya hati ya kiwanja kuandikwa jina la mkeo...

Haya muache tu, wakati wewe wamuona wa kazi gani wengine wamuona malkia na wammendea kweli.

Nataka sitaki hiyo.
 
Aisee hata mimi nahitaji sample ya talaka,
 
nashukuru kaka kwa kuwa concerned na kuwa na kumbu kumbu nadhani sio kila mwanume anafaa kuitwa mume mi nafikiri nimechemsha tatizo langu ni upole if you remember that post nilisema kuna mengi ila nilikuja na lile nikamwelewesha kwa upole alichonijibu ni siri yangu,imagine tangu nimeoa nimekonda badala ya kunenepa kwa sababu hapiki anamuachia dada mimi hupenda kula chakula kizuri sasa dada sio mpishi mahiri,hajawahi hata kupika chai,sio mjuzi wa kupika na hataki kujifunza2.tendo la ndoa miezi minne sasa sijapata3.akitoka kwenda misele haagi4.hajawahi kunifulia au kupiga pasi japo mara moja5.hasafishi chumba cha kulala6.simu zake zina password7.siri za ndani anatoa nje kwa majirani na kwa ndugu zake8.ana mawasiliano na jamaa ambaye tuliwahi kugombea mwanamke kabla hatujaoa9.maji ya kuoga hajawahi kutenga hata siku moja10.akipewa kitu na mwanamme ananionyesha na kuniambia waziwazi11.haendi kwenye nyumba za ibada12.usafi wa nyumba hauridhishi13.ana majibu makali yanayoweza kukufanya ukazimia14.marafiki zake wote ndoa zimewashindamengine nitaongezea baadae ngoja nikumbuke
Sasa wewe ulioa au ulikuwa bachela,/???, yashangaza ati///??..
 
jamani naomba mwenye sample ya talaka humu ndani anipostie nataka kufanya maamuzi magumu kidogo


Hii hapa:

"Wewe fuska, kuanzia leo hii sikutaki kwani tabia zako za kugawa kisamvu hovyo hovyo kwa wauza maji na urembo imenishinda. Kuanzia leo hii, nataka uchukue kilicho chako na urudi kwa wazazi wako labda ukiwa huko ndipo utajitafakari na kujuwa ujinga wangu kwako ni upi. Nilikupenda kwa dhati kumbe mwenzangu ulikuwa mtalii/dalali wa mapenzi na kuunadi utu wangu. Sikutaki tena kwani sitaki ku share magonjwa na wenzangu wajanja, nenda zako pengine utapata mjinga mwingine atakayeweza kuvumilia ufuska wako."
 
Kuna moja niliiona miaka kadhaa iliyopita iliyoandikwa na mtu anayenihusu (sasa ni marehemu). Iliandikwa:

"Mimi ..... leo nimemuacha Mama ...... Si mke wangu tena. Hanidai, simdai. Ataendelea kubakia na mtoto wetu wa mwisho ... mpaka hapo atakapokuwa mkubwa".

Chini kaweka saini yake. Unaweza kutumia hii kama template.
 
dah
hiv hii sector imeingiliwa na mapepo au nn?
miezi 6? au ndo kuolewa kuondoa nuksi?

Mara nyingi wanawake wanazivunja ndoa zao kwa kiburi chao, wakati wa uchumba utamwona ni mpole ana heshima, ndoa ikifungwa mwezi 1 mwingi tayari kaishaanza kutoa makucha yake. Jiulize, utakuta kijana alikuwa ni mtu wa kuwahi kurudi nyumbani lakini baada ya kuoa tabia inabadirika, anachelewa kurudi nyumbani na akirudi kalewa. Ndoa badala ya kuwa paradiso ndogo inakuwa jehanamu ndogo.
 
Back
Top Bottom