Uchaguzi 2020 Mwenye ushahidi wa Dkt. Magufuli akimtaja Tundu Lissu kwenye kampeni zake tangu zilipoanza atuwekee hapa

CHADEMA ni wapinzani wa CCM lazima mtukufu Magufuli azungumziwe bila kuchoka wala kuchuja mapungufu yake
 
Magufuli si alikuwa anapenda kutajwa tajwa kwenye na kila kitu, hata watu wakipata ajali wakipona badala ya kushukuru Manesi na Madakari anatajwa yeye
Sasa ni lazima atajwe tena huyohuyo kwenye uovu na ufisadi na ulaji wa rambirambi.
Na ulaji wa 10% ununuzi wa Ndege
 
Sasa kama Magufuli ameharibu hii nchi kila kona kwa nini asitajwe kila saa?Wewe unaweza kuzungumzia ufisadi bila kumtaja anaefanya ufisadi?Yeye Lissu amefanya nini hadi atajwe na Magufuli?
Mtukufu magufuli anawabambikia kesi kesi uonevu unyanyasaji mwingi kwa wapinzani wanaacheje kumtaja?
 

Utakuwa zezeta bro.

Anayemwita mwenziwe kuwa ni bwana yule ni nani?

Anayesemwa na mgombea yule kuwa ni kibaraka ni nani?

Anayesemwa na mgombea yule kuwa katumwa na mabeberu ni nani?

Anayesemwa na mgombea yule kuwa alikuwa akimpigia simu yule mgombea wetu pendwa tokea ACACIA ni nani?

Anayesemwa na mgombea yule kuwa atawapa madini yetu mabeberu ni nani?

Labda kama ulimaanisha kuwa hajawahi mgombea yule kukiri tu kuwa yeye ndiye aliyekuwa mtu nyuma ya lile shambulizi la marisau?
 
 

Magufuli hana jeuri ya kumtaja Lisu kwasababu hana hoja ya msingi atayoongea itakayomfanya amtaje Lisu. Huo ndio ukweli. Lakini Lisu ana mambo kibao ya kuongelea dhidi ya Magufuli na ndio maana ana guts za kumtaja kila wakati kutokana na mambo hayo kumuhusu Magufuli direct.
 
Si alimwomba/alimtaja lisu akiwa jimboni(kwao lisu),"Mwambieni lissu aachane na uraisi aje nimpe kazi"
 

Tundu Lisu yupi?
Aliyekua amepangiwa mpaka namna ya kufanyiwa mazishi ,kwa maana kuwa alikua ameshapangiwa kifo na watu wasiojulikana au huyu anayeivuruga CCM na watu wake wasiojulikana ?

Huyu Lisu aliyepo ni wa Mungu mwenyewe. Asingeletwa na Mungu basi shetani alipanga kuwaliza watetezi wa Uhuru ,haki na maendeleo ya watu.
Nchi hii ingekuwa na Mabwana (CCM wenye madaraka) na Watwana (Watanzania wote Wasio na madaraka )

Kumtaja Lisu kwenye kampeni za CCM ni hatari mana mkutano mzima unaweza ukalipuka kwa shangwe ikabaki ni aibu kubwa .
Hivi kwa nini CCM meumia sana Lisu Kupona ? Kwani mliwatuma waliompiga risasi?
Muulizeni Mungu mwenyewe mana ndio aliyekataa Lisu auawe bila sababu.
 
ni kwa vile MATAGA & Magufuli kwa miaka yote 5 hicho kinachoitwa "mafanikio" wameki personalise kama "mafanikio ya Magufuli".

Tundu Lissu aliling'amua hili..... so, very intelligently and smartly, akaamua kuilenga nyota hii ambayo CCM wameichagua kusafiria na hadi sasa tunapoelekea kwenye kilele cha kampeni amefanikiwa kwa 100%.

sasa hivi wagombea ubunge wa CCM wanapata taabu sana kujiuza kwa wapiga kura wao kama wao kwani kwa miaka hii 5 waliaminishwa kuwa kura yao ya turufu ni Magufuli na "mafanikio" yake. Tundu Lissu ameichakaza turufu hii imekuwa nyang'anyang'a, imelegea na sasa inatembelea magoti kuomba kura.

Tundu Lissu is very smart!
 
Ndio nini hiki? Au unajaribu kugundua nini?
Mara ya mwisho kumtaja nina ni aliphatic dikiwa twitter ya kumpa pole bass Jamaa mwoga sana hata chakubanga na Bashiri hawajawhi sema au kulitaja hilo jina
 
Simba kumtaja Yanga, and vice versa ni jambo la kawaida.. tuliza kijambio kipigwe hewa
 


Magufuli anapenda kumuita Tundu Lissu kwa jina la "Mtu yule"--- anaogopa hata kutaja jina "Tundu Lissu", wataalamu wenye akili watuambie ni kwanini Magu kawa muoga kwa jina???🤣
 
Nilipokuwa mdogo Marehemu bibi yangu alituasa kutomtaja Marehemu. Kuna watu wanaamini Lissu alikufa. Si kwa risasi zile. Bado butwaa linawaambia wanaona msukule na maruweruwe. Asante Mungu kwa Muujiza wa Lissu.
 
Magufuli muoga kama kungulu anamtaja lissu kwa. Kila siku kwa mafumbo nini kinamzuia asimtaje jina

Anaogopa hana cha kumsemea maana hana kashifa
Amegundua aliamuru auuwawe kwa makosa
Anajuta kumtuma makonda kuongoza squad ya wauaji
Hana la kufanya maana tume haikumbeba hatua za mwanzo
Au ameufyata
 
Huwa hataji majina bali huamrisha wapigwe risasi na wasio julikana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…