Tangu lini NURU (Tundu Lissu) na GIZA (Magufuli) vikachangamana na kuwa kitu kimoja?
Je, shetani anaweza kulitaja jina la YESU KRISTO? Thubutu. Ataungua moto bila huruma...
Na hivi itawezejanaje? Kwamba, mtu uliyemtandika risasi 16 za bunduki aina ya AK47 na SMG halafu akafa na baadaye kufufuka, utapata wapi ujasiri wa kulitaja jina lake tu achilia mbali kukaa naye meza moja mnywe chai??
Kama unataka kujua kuwa hili haliwezekani, muulize shetani aliyewaingia watawala wa Kiyahudi na Kirumi kumshtaki Yesu Kristo kwa uongo, wakamhukumu kumsulubisha msalabani mpaka akafa, wakamzika na baadaye akafufuka na kuwatokea akiwa hai....
Waulize hao watawala wa Kiyahudi na Kirumi kama wana ujasiri wa achilia mbali kutaja jina lake tu bali wa hata kumtazama tu. Hawawezi kama ambavyo huyu mzee hataweza kamwe....!!
Hii ni asili ya kawaida, kwamba, shetani kamwe hawezi kulitamka jina la Yesu Kristo kwa sababu hiyo ni NURU na GIZA...
TUNDU LISSU ni NURU na MAGUFULI ni GIZA. Nuru na Giza havichanganani kamwe...!!