Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Kilimanjaro akamatwa na Polisi akidaiwa kupiga picha gari la Mkurugenzi wa TISS

Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Kilimanjaro akamatwa na Polisi akidaiwa kupiga picha gari la Mkurugenzi wa TISS

Si mpaka kesi ifike kwa pilato Lema alishinda rumande miezi sita na Ni mbunge na kiongozi wa juu chadema sembuse huyo mpiga picha mjinga

Chadema ruzuku haipo Tena sababu bunge linavunjwa karibuni hao mawakili ana hela za kuwalipa?

Watamtetea chama kivipi kwani walimtuma kupiga hizo picha kuwa ohh alikuwa kwenye majukumu ya kichama ya kibavicha!!

Hilo atalinywa yeye na ndugu zake.Asitegemee chama
Tulia utaona tu mkuu.
 
Ok dereva amepiga na yeye akapost...kwa lengo lipi? Ignorance of the law is no defence......asome Penal Code na Act ya Intelligence and Security Service of 1996
Aliyepost ni Kigogo labda yeye awe amepost kwenye ma group kisha SNITCH akawatumia POLICCM.
 
Ok dereva amepiga na yeye akapost...kwa lengo lipi? Ignorance of the law is no defence......asome Penal Code na Act ya Intelligence and Security Service of 1996
Umepigilia msumari kuna mengine nilitaka niandike lakini si vizuri Ku pre empty atakiona cha mtema kuni o
 
Mpaka hiyo gari inapigwa picha at 'a very close range' walinzi wa DG wa TISS walikua wapi?? Au dereva wa DG wa TISS ambaye naye ni mtu wa kitengo alikuwa wapi??? Tuanzie hapa
Wewe unadhani alikuwa wapi.? Ushauri wangu kwako soma intelligence and security service Act of 1996....kuropoka mambo ya TISS hapa unaweza kujikuta pabaya
 
Hilo gari limeandika " Usipige Picha"?
Hu utawala unaishi kwa hofu sana, sana, bora hata kunguru kuliko huu utawala wa Jiwe na Gwajima
Ndivyo unavyodhani??!! Kapiga picha gari ya CIA, MI 5, FSB, MOSAD na intelligence ya Kim Jong Un...
 
Kapige picha kambi ya jeshi bila ridhaa yao uone mziki wake

Kifaa cha usalama wa taifa iwe gari au afisa mwenyewe Ni Siri .Yeye kaweka wazi Kama Nani? Atawaeleza hao polisi????? Waliomkamata Athuman Diwani alikuwa polisi na Hakuna alijua kuwa Ni usalama wa taifa Tena ngazi ya juuu

Bila Shaka huyo mpiga picha atapata nafadi nzuri tu ya kuelezea kilichomsukuma asipige miti picha ya upareni ila apige nyumban kwa mkurugenzi wa usalama wa taifa na gari yake na makazi yake no
Naamini hata adipopelekwa mahakamani majibu atakuwa kayatoa na wao watakuwa wamempa maswali ya kutosha ya kukiweka kichwa chake sawa kiasi kuwa akiondoka hata Kama hatapelekwa mahakamani akiona gari ya usalama wa taifa atakuwa anaikimbia Kama mwehu na kuweweseka usiku kucha

Namtakia mahojiano mema na polisi!!!!!

..mbona Diwani Athumani mwenyewe amewahi kupigwa picha?

..sembuse gari anayotumia Diwani Athumani?
 
Ndivyo unavyodhani??!! Kapiga picha gari ya CIA, MI 5, FSB, MOSAD na intelligence ya Kim Jong Un...
Kama kitu hakijakatazwa means kimeruhusiwa, hao CIA, MOSSAD etc unapiga nao picha, si gari tu, wapo ndugi zetu ni CIA na wanafahamika, hapa hata ukiwa mgaombo kata kama alivyokuwa yule DC WA HAI OLE SABAYA anajiita usalama wa taifa, hovyo kabisa
 
Kesi za Korea Kaskazini hizi Nchi inaendelea kuwa na wajinga waliopoteza muda kwenda shule...
 
View attachment 1446830

Lembrus Mchome anadaiwa kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kupiga picha gari la Diwani Athuman akiwa Kwao Mwanga , ambapo gari hiyo imeonekana mitandaoni ikiwa imeegeshwa maeneo ya Mwanga .

Bila shaka kesi hii ikifika mahakamani itavuta hisia za wengi , maana hata kama ni kweli , kupiga picha gari la serikali linalotumiwa na ofisa wa serikali kihalali hatujui adhabu yake itakuwa nini .

#Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka ili kujikinga na virusi vya Corona
Mtoa mada unaendeshwa na mihemko, tulia na tafakari. Hivi kuna kosa la kupiga picha gari? No, na usitegemee such charge in the court of law. Think twice.
Hivi ukiwa upo nyumbani kwako umepaki gari yako uwani then mtu usiyemfahamu na usiyejua sababu unamkuta anapga picha nyumba yako na gari lako utamsalmia na kuondoka au utamkamata na kumpeleka polisi kwa mahojiano? Hii in kufanya fujo.
Huyu ni kiongozi wa idara nyeti na ni kiongozi wa kitaifa, analindwa alafu mtu tu anapga picha makaazi yake then unaona jambo la kawaida.
Tanzania ina usalama wa kutosha kwa kuwa tunaishi kwa kutilia mashaka na kuchukua hatua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoa mada unaendeshwa na mihemko, tulia na tafakari. Hivi kuna kosa la kupiga picha gari? No, na usitegemee such charge in the court of law. Think twice.
Hivi ukiwa upo nyumbani kwako umepaki gari yako uwani then mtu usiyemfahamu na usiyejua sababu unamkuta anapga picha nyumba yako na gari lako utamsalmia na kuondoka au utamkamata na kumpeleka polisi kwa mahojiano? Hii in kufanya fujo.
Huyu ni kiongozi wa idara nyeti na ni kiongozi wa kitaifa, analindwa alafu mtu tu anapga picha makaazi yake then unaona jambo la kawaida.
Tanzania ina usalama wa kutosha kwa kuwa tunaishi kwa kutilia mashaka na kuchukua hatua.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi nimekupa taarifa tu mjomba , sasa mhemko wangu ni upi hapo ?
 
Tatizo siyo gari ila vijana wa Bavicha hawaaminiki wanaweza kutumiwa na mabeberu.

Unafanya siasa kwa DG wa TISS?.........huyo bavicha kaingia cha kike!
Kwa kifupi ukitaka kupata tabu saaana ingia mgogoro na TISS utakuwa umekwisha, maana hao jamaa hawana tabu na mtu mpaka uwaaanze wewe mwenyewe kama huyu alivyojiingiza kichwa kichwa.
 
Back
Top Bottom