Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan aongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM, Ikulu Chamwino

Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan aongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM, Ikulu Chamwino

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM ambae ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika tarehe 21 Mei, 2023 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.


View attachment 2630035View attachment 2630037View attachment 2630039
Ngoja mie nitizame jambo jingine kabisaaa , Naona sasa wameachana na maji ya kilimanjaro kwenye mambo ya kiserikali na sasa wanatumia maji ya Dewdrop🤪🤪 ingawa wamepambana kuyabandua stickers🤪🤪😂😂😂😂😂
 
Ni jambo jema
Nilitaka tu kukuuliza swali kuhusu hizo picha, lakini nikajikuta vidole vikigoma kuliandika hilo swali!

Ngoja niseme tu kwamba hawa ndio vinara wanaotuamria maswala mazito sana ndani ya nchi hii nyakati hizi.
 
Ngoja mie nitizame jambo jingine kabisaaa , Naona sasa wameachana na maji ya kilimanjaro kwenye mambo ya kiserikali na sasa wanatumia maji ya Dewdrop🤪🤪 ingawa wamepambana kuyabandua stickers🤪🤪😂😂😂😂😂
Nimekuelewa mkuu, 'polokwane'
 
Tunataka kuona matokeo chanya ya hivyo vikao kwenye maisha ya wakulima na watu wa hali ya chini na sio matajiri na Wafanyabiashara wakubwa.

Hiyo ndio CCM ya Karume na Nyerere.
Ni Sauti toka nyikani hizi haziwanyimi usingizi wenye chama chao wakati huu.

Zisome vizuri sura hizo unazoziona kwenye hiyo picha, halafu uje hapa ueleze matumaini yako yanatoka wapi?
 
Hao watu wa chini wanapaswa kupaza sauti za ili changamoto zao zifanyiwe kazi. Hii tabia yao ya kukaa kimya na kusubiri kusemewa ndiyo hupelekea wanaowasemea kuitwa wachochezi. Changamoto zitakazofanyiwa kazi ni watakaoongea.
Lakini si wanapewa sabuni, nguo, ubwabwa, n.k., nyakati wanapotakiwa kutoa kura zao zinapohitajika kujazia zile zilizofutikwa ndani ya masanduku ya kura?
 
Back
Top Bottom