Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo amwagiwa Tindikali na watu wasiojulikana

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo amwagiwa Tindikali na watu wasiojulikana

MPANDA Jr

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2011
Posts
1,295
Reaction score
159
Mwenyekiti wa CCM Wilaya mpya ya Gairo Bwana Omary Awadhi, amemwagiwa tindikali usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Gairo. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo tukio hilo lilitokea usiku wa manane baada ya watu wasiojulikana kumgongea na kumwamsha.

Hata hivyo anasema aligoma kufungua mlango bali alifungua kioo cha dirisha la chumbani kwake. Watu hao walimuonya kutohudhuria kikao ambacho yeye ni mhusika alipokataa, ndipo ghafla akahisi kumwagiwa kitu usoni kilichomletea maumivu makali sana.

Aliwahi kunawa maji lakini hali bado ni tete.Muda huu yupo safarini anakimbizwa Dar kwa matibabu zaidi baada ya uso wake kuharibika.

GAIRO

---------------------------------------

Taarifa toka kwa mjumbe wa Jumuiya ya Wazazi (Jina kapuni) anasema kumekuwepo mvutano wa muda mrefu kati ya Mwenyekiti huyo na Mbunge wa jimbo hilo la Gairo Mhe: Ahmed Shabiby. Mgogoro huo ulichukua sura mpya baada ya ziara ya Kinana kwani mwenyekiti alimtuhumu Mbunge huyo kugawa chama huku na yeye akitangaza kugombea ubunge 2015. Kikao kilichosababisha mtafaruku huo ni cha tarehe06/07/2013 kuhusu wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya kutaka kupiga kura ya kutokuwa na imani na Mwenyekiti huyo ambaye magaidi waliomdhuru walimtaka asihudhurie.
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Na hao ni CDM?? mmeparanganyika na hata hamuwezi kurudi kuwa wamoja tena kwa laana ya kuua na kuibia watanzania.
 
CCM mnaanza kujidhiilisha kuwa nyie ndo wamwaga tindikali. Duh ashukuliwe Mungu. Ukweli utazidi kudhiilika.
 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya mpya ya Gairo Bwana Omary Awadhi, amemwagiwa tindikali usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Gairo. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo tukio hilo lilitokea usiku wa manane baada ya watu wasiojulikana kumgongea na kumwamsha. Hata hivyo anasema aligoma kufungua mlango bali alifungua kioo cha dirisha la chumbani kwake. Watu hao walimuonya kutohudhuria kikao ambacho yeye ni mhusika alipokataa, ndipo ghafla akahisi kumwagiwa kitu usoni kilichomletea maumivu makali sana. Aliwahi kunawa maji lakini hali bado ni tete. Muda huu yupo safarini anakimbizwa Dar kwa matibabu zaidi baada ya uso wake kuharibika.

GAIRO

kwenye red hao watakuwa wana ccm wenzake,kugombeana vyeo na pesa
 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya mpya ya Gairo Bwana Omary Awadhi, amemwagiwa tindikali usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Gairo. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo tukio hilo lilitokea usiku wa manane baada ya watu wasiojulikana kumgongea na kumwamsha. Hata hivyo anasema aligoma kufungua mlango bali alifungua kioo cha dirisha la chumbani kwake. Watu hao walimuonya kutohudhuria kikao ambacho yeye ni mhusika alipokataa, ndipo ghafla akahisi kumwagiwa kitu usoni kilichomletea maumivu makali sana. Aliwahi kunawa maji lakini hali bado ni tete. Muda huu yupo safarini anakimbizwa Dar kwa matibabu zaidi baada ya uso wake kuharibika.

GAIRO

Mleta mada inaonekana kuna kitu unajaribu kukificha sijui kwa makusudi ama hujui waambie wana JF nikikao gani emwagiwa tindikali alipaswa kuhuzuria, je hao watu waliomgongea mpaka akafungua dirisha hajawajua hata kwa sauti...
 
dhambi ya unafiki haiwaachi huru itawatafuna mpaka mtuombe radhi watanzania!
 
Since wanatafutwa viongozi wa cdm na baadhi bado wako dodoma,hatukawii kusikia kuwa mh fulani kakamatwa na kuhusishwa na tuhuma hizi..........
 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya mpya ya Gairo Bwana Omary Awadhi, amemwagiwa tindikali usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Gairo. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo tukio hilo lilitokea usiku wa manane baada ya watu wasiojulikana kumgongea na kumwamsha. Hata hivyo anasema aligoma kufungua mlango bali alifungua kioo cha dirisha la chumbani kwake. Watu hao walimuonya kutohudhuria kikao ambacho yeye ni mhusika alipokataa, ndipo ghafla akahisi kumwagiwa kitu usoni kilichomletea maumivu makali sana. Aliwahi kunawa maji lakini hali bado ni tete. Muda huu yupo safarini anakimbizwa Dar kwa matibabu zaidi baada ya uso wake kuharibika.

GAIRO

Mtajuta kumchagua MWINGULU KUA NAIBU KATIBU MKUU KAZI KWENU
 
Back
Top Bottom