Pre GE2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akamatwa uwanja wa Ndege Songwe

Pre GE2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akamatwa uwanja wa Ndege Songwe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Screenshot 2024-08-12 120607.png

Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Mhe. John Pambalu wamekamatwa na Polisi muda huu uwanja wa ndege Songwe wakijiandaa kuelekea Mbeya, Ukamataji huu umeongozwa na RPC wa Mbeya.

========================

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema anasema “Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu tangu akamatwe (jana Agosti 11, 2024) hatujui yuko wapi, Polisi hawasemi, hatujui kama yeye na wenzake wamekula au la, pia Lissu ana dawa anazotumia kila siku kutokana na majeraha ya risasi na sijui kama amekunywa dawa.”

Ameongeza “Kutokana na hali hiyo, Mbowe alilazimika kusafiri kwenda Mbeya kukutana na Polisi, alipowasili Saa 4 Asubuhi akiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana, John Pambalu, Polisi wakawakamata na hatujui wako wapi.”

Pia soma: Uzi Maalum wa Matukio ya Kiusalama kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Benjamin Kuzaga simu yake ilipokelewa na msaidizi wake aliyesema “RPC yupo kwenye kikao”


Pia soma=> Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa
 
Setting the very bad precedence...
Tunarud kule kule kwa Gaidi...
Time is not on their side unfortunately....

Siasa itachangamka sana kuelekea 2025....

CCM wenzangu tusijaribu maana we will not believe how things may turn out.
 

Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Mhe. John Pambalu wamekamatwa na Polisi muda huu uwanja wa ndege Songwe wakijiandaa kuelekea Mbeya, Ukamataji huu umeongozwa na RPC wa Mbeya.
Mambo mengine yanachekesha sana.
Mambo mengi ya msingi polisi T wameshindwa na hawaoneshi kuyaweza.Ukifika muda wa masuala ya CDM wanakua mahiri na intelijensia zinakua njema kwelikweli.Vibweka hivi!
 

Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe. Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Mhe. John Pambalu wamekamatwa na Polisi muda huu uwanja wa ndege Songwe wakijiandaa kuelekea Mbeya, Ukamataji huu umeongozwa na RPC wa Mbeya.

Pia soma=> Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa
Kama walipanga kuhatarisha usalama wetu wadhibitiwe hawa wanasiasa wakichekewa ndio yanatokea kama ya kenya au uingereza
 
Amuulize Magufuli na ajifunze kutoka kwake, ni swala la mda tu!
Magufuli alifanya nini? Na mlimfa ya nini? 😁😁

Mnajifanyaga mna Ushirika na Mungu 🤣🤣🤣

Ni hivi,Binafsi nilikuwa naunga mkono Mwendazake kuwaminya ila sikuunga mkono utaratibu wa kubinya biashara.

So long as Samia hana shida kwenye biashara,nyie wa kwenye siasa mbingwe tuu maana hakuna Cha maana mnatusaidia.
 
Laanatullah nzi wa jijani, viongozi wake na organs zake zote zinazoipa nguvu.
MAZAFANTAZ
 
Back
Top Bottom