Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wangu CCM Taifa, Rais Dkt. Magufuli tafadhali achana na Kauli kama hii katika 'Kampeni' zako kwani zinakuharibia na zinachanganya

Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wangu CCM Taifa, Rais Dkt. Magufuli tafadhali achana na Kauli kama hii katika 'Kampeni' zako kwani zinakuharibia na zinachanganya

Hii kauli imetolewa zaidi ya nara tano sasa, Chadema hawajacapitalize kwenye huu udhaifu. Amekuwa anatoa kauli zinazopingana. Chadema mnatakiwa kuongea kwa sauti kuhusu hili. Ndio njia pekee ya kumwaibisha!
 
Wapinzani hawataki maendeleo ya vitu sasa asingekuwepo Kapuya mbunge wa CCM mdai maendeleo ya barabara hiyo barabara isingejengwa.Kasome sera ya Chadema hawana mpango na maendeleo ya vitu ina maana ukichagua mbunge wa Chadema sabau maendeleo ya vitu sababu hatayatafuta sera yake hairuhusu
Wala Dr Magufuli hajakosea
Walipo wabunge wa Chadema apeleke maendeleo ya vitu ya nini? Kuchagua mbunge wa Chadema ni kuchagua sera kuwa watu wa eneo hilo hawataki maendeleo ya vitu sasa kama hawataki unawalazimisha kuwapelekea?
Kwa hiyo anaposema maendeleo hayana chama ni geresha tu?
 
"Leo tutakubaliana?, kwa sababu siku nyingine huwa nawaeleza halafu hamfuati,niliwaambia mnichague mimi mkasema sawa, nikawaambia mnichagulie na mbunge wa CCM hamkunichagulia, nataka niwaeleze ukweli wala siwafichi asingekuwa Kapuya hii barabara nisingeijenga...mambo ndivyo yanavyokwenda hivyo".Dkt.Magufuli

ITV Tanzania / Nipashe

Hivi nyie mlio karibu nae akina Dkt. Bashiru Ali na Mzee Philip Mangula kwanini msishauri aachane na Kauli za 'Kibabe' kama hizi? Tunachoka sasa!!
Kwenye kampeni kuna namna nyingi ya kumshawishi mpiga kura, hii nayo ni mbini moja wapo katika kuhakikisha kuwa unapata kura za kutosha.
 
Wana CCM Wenzangu leo niwaambieni tu ukweli kuwa Kauli za 'Kibabe' na zenye 'Ubinafsi' kama hizi 'zinamuharibia' mno Mgombea Wetu Dkt. JPM.
Mmmhhhh.... leo ndio nimejua Kweli wewe ni "mwana ccm"
 
"Leo tutakubaliana?, kwa sababu siku nyingine huwa nawaeleza halafu hamfuati,niliwaambia mnichague mimi mkasema sawa, nikawaambia mnichagulie na mbunge wa CCM hamkunichagulia, nataka niwaeleze ukweli wala siwafichi asingekuwa Kapuya hii barabara nisingeijenga...mambo ndivyo yanavyokwenda hivyo".Dkt.Magufuli

ITV Tanzania / Nipashe

Hivi nyie mlio karibu nae akina Dkt. Bashiru Ali na Mzee Philip Mangula kwanini msishauri aachane na Kauli za 'Kibabe' kama hizi? Tunachoka sasa!!


Tatizo ameletwa mjini na Lori LA Ng'ombe hivyo azani Watanzania wote ni Ng'ombe tu wa kuwatandika ili waende marishoni.

Huyo Dr Bashiru akili aliziacha pale UDSM baada ya kuificha kadi yake ya CUF.
 
Yote tisa, fikiria pawe na mdahalo wa wagombea wote kisha mwongoza mdahalo aulize swali. Kuna uhalali gani wapiga kura kukupigia kura ilhali unaonesha kubagua hata kabla ya siku ya kupiga kura?
 
Huyu mzee washauri wake hawampendi, vinginevyo asingeendelea na hizi kauli zake tangu akiwa anafanya ziara mbalimbali kabla ya kampeni. Halafu ana kauli double standard mfano MAENDELEO HAYANA CHAMA lakini 'mkichagua upinzani sitawaletea maendeleo'
 
Wana CCM Wenzangu leo niwaambieni tu ukweli kuwa Kauli za 'Kibabe' na zenye 'Ubinafsi' kama hizi 'zinamuharibia' mno Mgombea Wetu Dkt. JPM.
Msema kweli mpenzi wa Mungu, yeye anaongea ukweli uliopo moyoni mwake, huenda wewe ndio hujamuelewa au humuelewi.
 
Mleta mada Magufuli yuko sahihi ukichagua mbunge wa Chadema ujue hutaki maendeleo ya vitu iwe barabara shule hospital nk

Sababu sera yao hawataki vitu Na wako wazi .Uchaguzi ni kuchagua sera sio mtu tu

Ukichagua Chadema ni ujumbe kwa serikali kuwa eneo hilo hamtaki vitu na Raisi anawajibika kuheshimu maamuzi yenu kwa kutoleta vitu iwe barabara au mradi wowote

Hivi 'Muasisi' Wetu wa Chama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Burito Nyerere anajua kuwa amekuacha Duniani 'Popoma' Wewe?
 
Wewe naye umeshapuuzwa na hoja yako hiyo mfu ila bado unahangaika tu!

Safi sana Mkuu na laiti angekuwa na 'Akili' wala asingekuwa anaandika mara kwa mara. Usishangae kusikia nae ni 'Think Tank' hasa wa huko CCM.
 
Wewe jamaa una akili kweli?Halafu unaweza ukakuta una familia kabisa,wewe ni mzigo hadi kwa watoto wako!Sijui utawafundisha nini!
Nimeshangaa sana!

'Wapumbavu' wachache kama Yeye ndiyo wamekifanya Chama chetu kiwe 'Kinachukiwa' na hata Mwenyekiti wetu nao 'Kutokukubalika' na Werevu.
 
Kaka YEHODAYA kwa mantiki hii, bhasi kama anawapatia watu kulingana na sera waliochagua i.e waliochangua upinzani bhas awapatie yale ya ilani ya upinzani!
Kwanini msumeno ukate upande mmoja?
Mimi binafsi nlikuwa namuona JPM bonge la genius lakini kiukweli am very disappointed!
Ni mweupe mno....if you know what am saying!
Magufuli ni mbaguzi
 
Wewe kila siku unamuunga mkono Lissu, leo unasema Magufuli ni m/kiti wako, siyo unafiki wa siasa? Ukweli Magufuli hafai, lakini ni bora kuliko waliopita na Lissu hafai zaidi!

Siku zingine ni vyema kama huna uhakika na Jambo fulani basi uulize Kwanza kabla ya Kukurupuka. Hivi kuna mwana JF asiyejua Mimi ni wa CCM?
 
Back
Top Bottom