Huwajui wachezaji wa kitanzania wewe huwa wanaviwango vya kupanda na kushuka hivyo hivyo.
After all kwa sisi wafuatiliaji wa mpira tulikuwa tunamfahamu Nchimbi toka akiwa Tanzania Prisons baadae Njombe Mji na Azam Fc hivyo kiwango chake kilikuwa kinafahamika.
Hata Yanga walimsajili baada ya kuwafunga goli tatu na Yanga wakiwa hawana striker upgrade yake tu hivi angekuwepo Makambo ungeweza kumhitaji huyo Nchimbi ,?
Sent using
Jamii Forums mobile app
Anyway ni kawaida ya watu wa soka kujiona yy anajua zaidi kuliko mtu mwingine yy ni mfuatiliaji zaidi kuliko shabiki mwingine.
Bro hatuishi pamoja, hatujuani nani mfuatiliaji zaidi nani hajui, hayo tuyaache .
Dunia nzima viwango vya wachezaji kupanda na kushuka ndiyo tabia ya soka. Ndo maana kuna wachezaji wengiii lkn wanaotumika kwenye vilabu kila wakati ni wachache wengine wanakuwa ingia toka halafu anapotea mechi kadhaa.
Nchimbi ni mshambuliaji chipukizi anayejengeka si kweli kwamba kapewa nafasi Yanga sababu ya kuwafunga.
Nakubali yanga ilikuwa inahaha kutafuta mshambuliaji na ndo maana kama utakumbuka ilijaribu kumsajili mpaka SALAMBA toka LIPULI siku za nyuma kidogo sababu ndiye aliyekuwa HOT kiasi mpaka Simba ikamsajili.
Nchimbi ndiye mshambuliaji aliyekuwa HOT wakati Yanga ikiwa inahaha kutafuta mshambuliaji huku Nchimbi akiwa ameng'aa timu ya Taifa kwa kupewa nafasi na kocha MATOLA.
NCHIMBI kaonekana na wengi kuwa anakitu kinachoweza kuisaidia timu, ndo maana kapita huko kote, Matola baada ya kuichukua PT akamuongeza DITRAM na kumpa majukumu.
Matola baada ya kuingia national team akashauri na kumuongeza DITRAM na kumpa majukumu na kuyatekeleza vyema.
Luc & Boniface wamempa majukumu katika mechi ngumu na kayatekeleza vyema lkn bado anazidi kukomaa.
Angekuwepo Makambo , ungeweza kumuhitaji huyo Nchimbi? Kwangu hili swali jibu lake ni jepesi sana NDIYO.