Mwenyezi Mungu: Sifa, Uwezo na Alama za uwepo wake

Mwenyezi Mungu: Sifa, Uwezo na Alama za uwepo wake

HORSE POWER

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2015
Posts
2,238
Reaction score
1,577
Habari WanaJF.

Karibuni tupambane kwa hoja. Wote wenye hoja wake hapa tupeane elimu na maarifa. Mimi nitatumia Quran na mazingira yanayotuzunguka.

JE MUNGU YUPO?
Kwangu mimi jibu ni NDIO. Nina sababu mbili za kukubali uwepo wake. Lwanza mimi mwenyewe na mazingira yaliyonizunguka na pili ni miujiza ya kitabu cha Quran. Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya Quran na mazingira tunayoishi.

Mwenyezi Mungu anasema:

Quran 45:3; "Bila shaka katika mbingu na ardhi ziko alama kubwa za kuonyesha kuwa yuko Mwenyezi Mungu kwa ajili ya wanaoamini".

Quran 45:4; "Na katika umbo lenu na katika viumbe alivyovitawanya, zimo alama vile vile kwa watu wenye yakini."

Quran 45:5; "Na katika kupishana (kufuatana) usiku na mchana, na riziki anayoteremsha Mwenyezi Mungu kutoka mawinguni (mvua) na akaifufua kwayo ardhi baada ya kufa kwake, na katika mabadiliko ya upepo, zimo alama pia kwa watu wenye akili."

Kumbe hapa tunathibitishiwa na Mwenyezi Mungu kwamba alama za uwepo wake zimetuzunguka. Huyu mwanadamu kwanza aanze kujichunguza yeye mwenyewe kwa umakini; jinsi umbile lake lilivyopangwa kwa ufundi mkubwa, na achunguze utendaji kazi wa mwili wake aone maajabu ya mifumo mingi inavyofanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu bila ya kusigana.

Je, haya masuala yamekuja yenyewe tu? Hakuna aliyeyapanga masuala haya kwa utaalamu na kuyasimamia yakafuata mpango wake?

Itaendelea!
 
Quran 45:3 umeinukuu kuwa kuna alama kubwa za kuonyesha Mungu yupo kwa ajili ya wanaomuamini,
Ni alama gani kubwa inayoonyesha huo uwepo wake? Hebu itaje hapa
Na kwanini huo uwepo wake uwe kwa watu fulani tu? Au ana upendeleo huyu Mungu wako?
 
Quran 45:3 umeinukuu kuwa kuna alama kubwa za kuonyesha Mungu yupo kwa ajili ya wanaomuamini,
Ni alama gani kubwa inayoonyesha huo uwepo wake? Hebu itaje hapa
Na kwanini huo uwepo wake uwe kwa watu fulani tu? Au ana upendeleo huyu Mungu wako?

Kazitaja, eti tujichunguze maumbo yetu na jinsi tumeumbwa kwa ustadi wa hali ya juu, unyeshaji wa mvua, usiku na mchana nk;

Sasa mimi namwambia kuwa Nimezaliwa na wala sijaumbwa, na kuhusu haya mengine mimi naweza kusema hata yeye anaweza kuangalia mazingira na akashangaa akaanza kutunga vitabu na kuwarubuni wajinga.

Mwandishi aliyatazama mazingira na akastaajabu, akapata mihemko ya kuandika kitabu. Pia akajitazama yeye akastaajabu kwa jinsi mwili wake ulivyo na utendaji kazi wake.

Ndivyo hata huyu mleta mada alivyotazama mazingira na yeye kwa ujumla akastaajabu na kukubali kwamba mungu yupo pasipo kuchambua mwandishi wa quran na biblia.

Nimuulize kaswali kadogo tu;

Mleta mada na wengine walivyo kama wewe, kwanini mmejitazama utata wa miili yenu, akili zenu, na utendaji kazi wa hivyo vyote, ambavyo havijafikia hata nusu ya utata wa Mungu wenu mkakubali kwamba mmeumbwa, Kwanini sasa mseme Mungu Hajaumbwa ilihali yeye ni wa utata kuliko ninyi?

Je, kitu chenye akili kama huyo Mungu chaweza kutokea tu kwa bahati mbaya kama mnavyokataa mwanadamu hawezi kuwako bila muumba kisa tu ni wa utata? Kwanini basi mkatae Mungu hajaumbwa wakati yeye ana akili kuliko mwanadamu?

Mimi naijua quran kidogo... Kiranga njoo maana najua wewe unaijua quran vizuri
 
aretasludovick

Kwanza katika maelezo yake hayo maswala ya usiku na mchana, mvua, muonekano wa binadamu yalinifanya nimuone jinsi gani ana elimu ndogo mana hajui hata mvua inapatikanaje.

Nikagundua pia muandishi wa kitabu chake nae kuna uwezekano mkubwa kuwa hajamaliza hata elimu ya msingi ( kufuta ujinga) mana ana hoja dhaifu sana, ila niliamua tu kwenda nae polepole ili asije akakimbia kama kwenye ule uzi wake mwingine alivyoingia mitini.

Sasa kwa hii speed uliyoanza nayo napata mashaka.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza katika maelezo yake hayo maswala ya usiku na mchana, mvua, muonekano wa binadamu yalinifanya nimuone jinsi gani ana elimu ndogo mana hajui hata mvua inapatikanaje.
Nikagundua pia muandishi wa kitabu chake nae kuna uwezekano mkubwa kuwa hajamaliza hata elimu ya msingi ( kufuta ujinga) mana ana hoja dhaifu sana, ila niliamua tu kwenda nae polepole ili asije akakimbia kama kwenye ule uzi wake mwingine alivyoingia mitini.
Sasa kwa hii speed uliyoanza nayo napata mashaka.

Ha ha hah nimekumbuka kweli ule uzi aliukimbia 😀 ngoja tumsikilize maana anaonekana hajafuta ujinga bado
 
Huwa natilia sana shaka upeo na uelewa wa watu wanaoleta vifungu vya biblia na quaran kujustfy uwepo na ukuu wa Mungu....
Kila siku humu ndani wanawambia hivyo vitabu vinajicontradict na ni vya kutungwa tu na watu wakale lakn wao wanajifanya hata hawaelewi.i,e wanafikiri kila watu wanaviamini..?...huu ni zaidi ya ujuha
 
aretasludovick

Quran inakwambia kuna watu Mungu kafanya mioyo yao iwe migumu wasimfahamu, kwa makusudi.

Na hawa watu hata wafanyaje hawatapata rehema ya kumjua.

Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na ujuzi wote afanye kitu cha roho mbaya kama hicho wakati ana uwezo wa kuwapa watu wote rehema ya kumjua vizuri tu?

Ukichunguza utaona hakuna Mungu huyu, kitabu kimeandikwa na watu tu. Angekuwepo, kitabu kisingekuwa na basic contradictions kama hizi.
 
Last edited by a moderator:
Quran inakwambia kuna wagu mungu kafanya mioyo yao iwe migumu wasimfahamu, kwa makusudi.

Na hawa watu hata wafanyaje hawatapata rehema ya kumjua.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na ujuzi wote afanye kitu cha toho mbaya kama hicho wakati ana uqezo wa kuwapa watu wote rehema ya kumjua vizuri tu?

Ulichunguza itaoma hakuna mungu huyu, kitabu kimeandikwa na watu tu. Angekuwepo, kitabu kisingekuwa na basic contradictions kama hizi.

Chaajabu huyu mleta uzi kashakimbia
 
Quran inakwambia kuna wagu mungu kafanya mioyo yao iwe migumu wasimfahamu, kwa makusudi.

Na hawa watu hata wafanyaje hawatapata rehema ya kumjua.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na ujuzi wote afanye kitu cha toho mbaya kama hicho wakati ana uqezo wa kuwapa watu wote rehema ya kumjua vizuri tu?

Ulichunguza itaoma hakuna mungu huyu, kitabu kimeandikwa na watu tu. Angekuwepo, kitabu kisingekuwa na basic contradictions kama hizi.

Na Kama kweli yupo huyu Mungu basi sie huyo anayesifiwa kuwa ana upendo na kuweza yote, labda atakuwa mwingine tu
 
mungu yupo ........and no reference from any book (quraan or bible)..soma story ya mtu anayeitwa nostradumus alaf ujiulize ..those coincidences wher do they come from
 
mungu hawez jithibitisha kwake kwa kunyesha mvua hapana maana science ina majib teyar ya kutokea kwa mvua.....ila kamwe science haina majibu kwanini ramujan india alikua ana solve complex mathematics akiwa na miaka mitatu without learn anywher.......wakatoa majibu yasio ridhisha ety intuitive knowleg(knwlg from no wher)
 
mungu hawez jithibitisha kwake kwa kunyesha mvua hapana maana science ina majib teyar ya kutokea kwa mvua.....ila kamwe science haina majibu kwanini ramujan india alikua ana solve complex mathematics akiwa na miaka mitatu without learn anywher.......wakatoa majibu yasio ridhisha ety intuitive knowleg(knwlg from no wher)

Nafikiri unamaanisha Ramanujan. Umenikumbusha kitabu cha Robert Kanigel "The Man Who Knew Infinity: A Life of the Genius Ramanujan".

Ila kiwa genius mzigo, jamaa kuna wakati alitaka kujirusha aangukie kwenye reli agongwe na treni Uingereza.

Sayansi kushindwa kueleza ujuzi wa Ramanujan haimaanishi kwamba kuna mungu, inamaanisha tu kwamba hatujajua vizuri ubongo unavyofanya kazi.
 
Katika sehemu iliyopita nilinukuu baadhi ya aya katika kujenga hoja yangu. Katika moja ya aya hizo,moja ilisema hivi Quran 45:3; "Bila shaka katika mbingu na ardhi ziko alama kubwa za kuonyesha kuwa yuko Mwenyezi Mungu kwa ajili ya wanaomini." Lakini sijaifafanua zaidi aya hii, pengine wapo wanaohoji Mungu ninayemzungumzia hapa ni yupi. Sasa hebu nieleze hili kwanza.

Mungu ninayemzungumzia mimi ni yule ni Mwenyezi Mungu muumba mbingu na ardhi na vilivyomo.

Quran 2:255; "Mwenyezi Mungu,hakuna mola ila yeye,na ndiye mwenye uhai wa maisha,msimamia kila jambo."

Quran 57:2; "Ufalme wa mbingu na ardhi ni wake.Anahuisha na kufisha.Na yeye ni mwenye uweza juu ya kila kitu."

Quran 57:3; "Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa mwisho.Naye ndiye wa Dhahiri na wa Siri. Naye ndiye Mjuzi wa kila kitu."

57:4; "Yeye ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi katika nyakati sita,kisha akakaa katika Enzi (yake). Anayajua yanayoingia katika ardhi na yanayotoka humo, na yanayoteremka kutoka mbinguni na yanayopanda humo. Naye yu pamoja nanyi popote mlipo.Na Mwenyezi Mungu anaona mnayotenda (yote)."

Hizi ni baadhi tu ya sifa za Mwenyezi Mungu ninayemkusudia. Nitazifafanua:

MUUMBAJI NA MSIMAMIAJI WA KILA JAMBO.

Yeye ndiye aliyeumba kila kitu;ndiye asili ya kila kitu unachokijua na usichokijua. Na ndiye msimamiaji/mwendeshaji wa kila jambo;hivyo basi kila kitu kinafuata mpango wake (kinakwenda kama kilivyopangiwa).

Mfano 1:
Jua linachomoza Mashariki na kuzama Magharibi. Hili halina ubishi kwamba huo ndio utaratibu wake tangu kuumbwa kwake. Haijawahi kutokea popote pale duniani kwamba jua limebadilisha utaratibu; pengine limechomoza Kaskazini na kuzama Kusini. Jua liko kwenye utiifu kwa yule aliyeliumba na kuliwekea utaratibu wa kufuata mpaka muda uliowekwa. Lisingekuwa na msimamizi lingefanya linavyotaka.

Mfano 2: Katika suala la kubeba mimba,jukumu hili Mwenyezi Mungu amempa mwanamke kwa namna alivyomuumba. Hili halihitaji maelezo mengi, hakuna siku mwanaume atabeba mimba kwa sababu hakuumbwa na sifa hiyo. Na hata kwa wanyama na wadudu nao ni hivyohivyo; jike ndiye mwenye kubeba mimba.

Mifano ni mingi ila itoshe tu kusema kwamba mifano hiyo miwili hapo juu,masuala hayo yako nje ya uwezo wa kiumbe chochote,si mwanadamu tu. Hakuna mwanadamu yeyote hata awe na elimu kiasi anayeweza kubadili utaratibu aliouweka Mwenyezi mungu.
Itaendelea!
 
Mungu ni nadharia inayofutika. vichwani mwa wanadamu kadri siku zinavyosonga watu wanaanza kuelewa njama za wana waisaraeli
 
Wewe ni mtupu upstair_sema utakuwa ni mmoja wa wale wavaa visuruali vifupi ndio maana unaamini watu wote wanaamini hicho kitabu cha kutungwa na mizimu ya kiarabu.
Mtu mwenye uelewa wa kweli na yuko exposed na mambo ya dunia ya sasa hawezi ku_quote vitabu hivi vya hadithi vya quaran na biblia kujustfy uwepo ama nguvu za Mungu.
 
Wewe ni mtupu upstair_sema utakuwa ni mmoja wa wale wavaa visuruali vifupi ndio maana unaamini watu wote wanaamini hicho kitabu cha kutungwa na mizimu ya kiarabu.
Mtu mwenye uelewa wa kweli na yuko exposed na mambo ya dunia ya sasa hawezi ku_quote vitabu hivi vya hadithi vya quaran na biblia kujustfy uwepo ama nguvu za Mungu.

Hata mi nahisi huyu ni wale wavaa pedo na kichwa chake kina shida kidogo
 
Back
Top Bottom