Mwenyezi Mungu: Sifa, Uwezo na Alama za uwepo wake

Mwenyezi Mungu: Sifa, Uwezo na Alama za uwepo wake

Kwamna hoja ni ngeni au si ngeni si jambo la msingu, na sijaona umuhimubwa kusema hoja si ngeni.

Cha muhimu ni hoja kupata jibu.

Unalo jibu la hoja?

Watu waliposhindwa kujibu "Poincare's Conjecture" hawakulitatua kwa kusema "swali hili lina zaidi ya miaka 200 halijajibiwa". Si geni. Walitafuta jibu mpaka wakalipata.

Swali hiki nimelisoma mara ya kwanza miaka takriban 20 iliyopita, katika kitabu cha "Philosophy of Religion: An Anthology". Na limejadikiwa kwa mamia kama si maelfu ya miaka, bila jibu la kuridhisha kutoka kwa wale wanaosema mungu huyu yupo.

Swali la msingi kabisa ni hili.

Kwa nini mu gu mwenye iwezo wote, ujuzi wote na yoendo wote hajaumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani wakati ambapo alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Hujalijibu.

Nukuu zako ni hafifu na hazijibu swali.

Kwani zinatoa uwezekano wa mungu kushindwa kuumba ulimwengu usio na mabaya.

Hazijibu swali, zinarudi kwenye msi gu wa mimi kuyliza swali.

Swali zuri sana ndugu yangu.Naomba nikujibu kama ifuatavyo,iwe ni faida pia kwa wale wenye swali kama lako.
Quran 76:1; "Hakika ulimpitia binadamu wakati mrefu katika dahari,hakuwa kitu kinachotajwa.(Binadamu ndiye kiumbe wa mwisho kuletwa ulimwenguni).
Quran 76:2; "Kwa hakika tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyochanganyika;(ya mwanaume na mwanamke),ili tumfanyie mtihani (kwa amri zetu na makatazo yetu);kwa hiyo tukamfanya ni mwenye kusikia na mwenye kuona."
Quran 76:3; "Hakika sisi tumemuongoa,(tumembainishia njia zote mbili;kuwa hii ndio ya kheri na hii ndio ya Shari).Basi (mwenyewe tena) atakuwa mwenye Shukrani au awe mwenye kukufuru. (kukanusha)."
Hapo jibu liko wazi kwamba huyu mwanadamu ana hiari ya kuchagua;aidha kushukuru au kukufuru kwani kawekewa wazi kila kitu.Na kapambanuliwa njia ya uongofu na upotevu;kwa hiyo ni juu yake kuchagua kwani huo ni mtihani.Na Mwenyezi Mungu kaumba maovu kama mtihani kwa wanadamu.
 
Eti mungu yupo
Afu mtu ana qoute Qur'an
Nani kasema Qur'an ndio kitabu cha kutoa facts.
Wewe uliye qoute unahitaji usome Darwin's book entitled The Origin of Species

Ndugu yangu,Charles Darwin ni binadamu.Ni mwanasayansi na anayeheshimika.Sasa ikiwa aliweza kufanya tafiti nyingi za kisayansi,unadhani huo uwezo alionao kaupata wapi?
 
Mimi nawaachia wa nukuu Quran, maana ndicho kutabu wanachokuamunu.

Katika Quran, imeandukwa kwamba kuna watu mungu atawafanya mioyo yao iwe migumu kumuelewa. Hata wafanyeje hawatapata rehema ya kumjua. Ndivyo alivyotaka mwenyewe.

Sasa nawauliza. Inakuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote akawa na roho mbaya hivyo?

Hao watu wamemkosea nini mpaka awapangue hivyo?

Na kama yeye mwenyewe ndiye aliyewapangia kutomjua hata wafanye nini, siku ya kiama atawahukumu? Kwa kosa gani?

Mpaka sasa sijapewa jibu.

Ndugu yangu Kiranga,jibu lipo.Mwanadamu kupotea atake mwenyewe na halikadhalika kuongoka atake mwenyewe.
Quran 76:3; "Hakika sisi tumemuongoa mwanadamu,(tumembainishia njia zote mbili;kuwa hii ndio ya kheri na hii ndio ya shari).Basi (mwenyewe tena) atakuwa mwenye Shukrani au mwenye kukufuru (kukanusha)."
Aya hii inaweka wazi kwamba mwanadamu ana uhuru wa kuchagua;aidha kupotea au kuongoka.Halazimishwi.Kikubwa hoja imfikie.Lakini pamoja na mwanadamu kupewa akili ya kupambanua,mitume na manabii kuja na hoja kwa huyuhuyu mwanadamu na halikadhalika na vitabu vya muongozo kuletwa kwa huyuhuyu mwanadamu,bado wapo vichwa ngumu mpaka leo.Hao hata uwaonye namna gani,uwape hoja za kila namna na kuwanasihi kadri iwezekanavyo bado watakanusha.Hawa sasa ndio Mwenyezi Mungu anasema wenye nyoyo ngumu kuliko jiwe,maana hata jiwe linaweza kupasuka na kupitisha maji.
 
Ni jambo jema na linalopendeza kwamba hapa JF kuna wasomi wengi na wazuri,na hasa masuala ya sayansi.Mimi nimeishia darasa la saba.Bila shaka nitapata elimu.
Nina maswali matatu kwenu mnaokanusha uwepo wa Mungu kwa hoja za kisayansi:
1.Ni wapi/nini/nani asili au chanzo cha sayansi?
2.Hao wanasayansi wametumia uwezo mkubwa wa akili katika tafiti zao.Je,ni wapi asili ya huo uwezo wao wa kiakili?
3.Ni kwanini basi kwa uwezo wao huo wameshindwa kubuni mkakati wa kisayansi ili wasife au kuurudisha uhai?
 
Ndio maana nasema usome usome The Origin of Species
Utaelewa uwezo wote aliupata wapi.
Au wewe unafikiri alipewa na mungu?

Wewe ni mwanasayansi,nijibu kwa mujibu wa sayansi.
 
Swali zuri sana ndugu yangu.Naomba nikujibu kama ifuatavyo,iwe ni faida pia kwa wale wenye swali kama lako.
Quran 76:1; "Hakika ulimpitia binadamu wakati mrefu katika dahari,hakuwa kitu kinachotajwa.(Binadamu ndiye kiumbe wa mwisho kuletwa ulimwenguni).
Quran 76:2; "Kwa hakika tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyochanganyika;(ya mwanaume na mwanamke),ili tumfanyie mtihani (kwa amri zetu na makatazo yetu);kwa hiyo tukamfanya ni mwenye kusikia na mwenye kuona."
Quran 76:3; "Hakika sisi tumemuongoa,(tumembainishia njia zote mbili;kuwa hii ndio ya kheri na hii ndio ya Shari).Basi (mwenyewe tena) atakuwa mwenye Shukrani au awe mwenye kukufuru. (kukanusha)."
Hapo jibu liko wazi kwamba huyu mwanadamu ana hiari ya kuchagua;aidha kushukuru au kukufuru kwani kawekewa wazi kila kitu.Na kapambanuliwa njia ya uongofu na upotevu;kwa hiyo ni juu yake kuchagua kwani huo ni mtihani.Na Mwenyezi Mungu kaumba maovu kama mtihani kwa wanadamu.

We nae unachosha sana, mbona bado hujajibu swali mpaka sasa zaidi ya kuquote mistari isiyo na msingi wowote katika uzi huu?
Mi nikiamua kuaichambua hiyo mistari yako hutachelewa kulalamika.
Hizo aya zako ulizonukuu quran 76:1-3 zinaonyesha kuwa huyo Mungu wenu hakuwa peke yake katika hiyo kazi ya uumbaji sasa nataka kujua alikuwa na nani? Na hao aliokuwa nao wametoka wapi?
Hivi huyo Mungu yupo kweli au ni hadithi tu hizi unazotuletea?

Swali lilikuwa rahisi tu
Huyo Mungu wako mwenye uwezo wote kwanini hakuumba dunia isiyowezekana kufanyika mabaya?
 
Ni jambo jema na linalopendeza kwamba hapa JF kuna wasomi wengi na wazuri,na hasa masuala ya sayansi.Mimi nimeishia darasa la saba.Bila shaka nitapata elimu.
Nina maswali matatu kwenu mnaokanusha uwepo wa Mungu kwa hoja za kisayansi:
1.Ni wapi/nini/nani asili au chanzo cha sayansi?
2.Hao wanasayansi wametumia uwezo mkubwa wa akili katika tafiti zao.Je,ni wapi asili ya huo uwezo wao wa kiakili?
3.Ni kwanini basi kwa uwezo wao huo wameshindwa kubuni mkakati wa kisayansi ili wasife au kuurudisha uhai?

Chanzo cha Sayansi nipale binadamu akipo aanza kuuliza maswali kuhusu vitu vinavyomzunguku bila kutoa majibu kama miungu, mungu au shetani,mapepo na nakadharika
Swali la pili nimeshajibu
Kwanza nani alikuambia wanasayansi wameshidwa kuendeleza uhai,sema ni bado hawaja gundua ila sio wameshidwa. Nahata kama wakigundua haina maana kwamba tuendelee kuishi ili iweje.
 
Kitu chochote cha kisayansi lazima kiweze kutafitiwa na kupata uhakika wa mambo yanavyokwenda. Sayansi ni juhudi tu ya mwanadamu kujiongezea maarifa ili aweze kuishi katika dunia hii. Hadi sasa ufahamu wa mwanadamu na uelewa wake kuhusu mazingira yake ameweza kuupata kwa muda mrefu na kadri anavyopata changamoto katika maisha yake. Vitu vyote anavyogundua mwanadamu kupitia utafiti wake kwakweli siyo kwamba havipo bali vipo tangu dunia ilipoumbwa. Ila juhudi za kuzivumbua hizo tunu ndio zinachukua muda mrefu kupitia wanadamu kujifunza na kuchunguza dunia na ulimwengu kwa ujumla. Hadi sasa mwanadamu kupitia ugunduzi wake ambao tunauita sayansi ameweza kufahamu dunia na ulimwengu kwa kiasi kidogo sana. Haitafika siku binadamu akayaelewa mambo yote yanayomzunguka. Hata kama atasoma vitabu vyote vitakatifu. Hata tunaowaita manabii na mitume wa mungu mwenyewe hawakuyafahamu mambo yote japo waliweza kufanya mambo mengi ambayo kwa watu wengine yalionekana kama maajabu au miujiza. Hata ufahamu wetu kuhusu mungu hatujaweza kuupata wote na hivyo hakuna hata mtu au mtume au nabii atakayesema anazifahamu siri zote za uungu. Kwahiyo, katika kuchangia mada hii ninachoweza kusema ni kuwa sayansi haitakoma kwani binadamu hajafaham mambo yote na wala sayansi ya ugunduzi kwa maana ya kujifunza mambo mapya haitakoma na wala binafamu hana uwezo wa utambuzi wa mambo yote ya dunia hii. Inatosha tu kuamini kuwa kuna mambo hatuyajui na wala hatutayajua yote hata kama tutalala macho. Kama hatuamini tujiulize kwann tunalala usingizi bila kujijua? Ni dakika ipi na nukta ipi mtu anaweza kusema alilala!!! Na ndio maana maandiko matakatifu yanatufunfisha kuwa mungu ni MWENYEZI (God is almighty) NI MUWEZA WA YOTE, ALIKUWEPO, YUPO ATAENDELEA KUWEPO NA HAFANANISHWI NA CHCHOTE. Ndiyo maana yote hayo tunayapokea kwa IMANI. Kama unaamini unaishia kusema AMINA. Hata kwa anayebisha hawezi kuwa na majibu, kwani mwenye majibu ya yote ni MUNGU MWENYEWE. Siku ikitokea binadamu awaye yote akawa na majibu ya yote hayo basi HUYO ATAKUWA NI MUNGU MWENYEWE. Ulimwengu hauna mwisho, na mambo yake yote hayana mwisho. Uwezo wetu wa kufikiri una mwisho na ndio tofauti yetu kati yetu na Mungu. Kwa akili zetu hatuwezi kuyajua yote kwasababu sisi sote ni WANA WA ADAM.
 
Kitu chochote cha kisayansi lazima kiweze kutafitiwa na kupata uhakika wa mambo yanavyokwenda. Sayansi ni juhudi tu ya mwanadamu kujiongezea maarifa ili aweze kuishi katika dunia hii. Hadi sasa ufahamu wa mwanadamu na uelewa wake kuhusu mazingira yake ameweza kuupata kwa muda mrefu na kadri anavyopata changamoto katika maisha yake. Vitu vyote anavyogundua mwanadamu kupitia utafiti wake kwakweli siyo kwamba havipo bali vipo tangu dunia ilipoumbwa. Ila juhudi za kuzivumbua hizo tunu ndio zinachukua muda mrefu kupitia wanadamu kujifunza na kuchunguza dunia na ulimwengu kwa ujumla. Hadi sasa mwanadamu kupitia ugunduzi wake ambao tunauita sayansi ameweza kufahamu dunia na ulimwengu kwa kiasi kidogo sana. Haitafika siku binadamu akayaelewa mambo yote yanayomzunguka. Hata kama atasoma vitabu vyote vitakatifu. Hata tunaowaita manabii na mitume wa mungu mwenyewe hawakuyafahamu mambo yote japo waliweza kufanya mambo mengi ambayo kwa watu wengine yalionekana kama maajabu au miujiza. Hata ufahamu wetu kuhusu mungu hatujaweza kuupata wote na hivyo hakuna hata mtu au mtume au nabii atakayesema anazifahamu siri zote za uungu. Kwahiyo, katika kuchangia mada hii ninachoweza kusema ni kuwa sayansi haitakoma kwani binadamu hajafaham mambo yote na wala sayansi ya ugunduzi kwa maana ya kujifunza mambo mapya haitakoma na wala binafamu hana uwezo wa utambuzi wa mambo yote ya dunia hii. Inatosha tu kuamini kuwa kuna mambo hatuyajui na wala hatutayajua yote hata kama tutalala macho. Kama hatuamini tujiulize kwann tunalala usingizi bila kujijua? Ni dakika ipi na nukta ipi mtu anaweza kusema alilala!!! Na ndio maana maandiko matakatifu yanatufunfisha kuwa mungu ni MWENYEZI (God is almighty) NI MUWEZA WA YOTE, ALIKUWEPO, YUPO ATAENDELEA KUWEPO NA HAFANANISHWI NA CHCHOTE. Ndiyo maana yote hayo tunayapokea kwa IMANI. Kama unaamini unaishia kusema AMINA. Hata kwa anayebisha hawezi kuwa na majibu, kwani mwenye majibu ya yote ni MUNGU MWENYEWE. Siku ikitokea binadamu awaye yote akawa na majibu ya yote hayo basi HUYO ATAKUWA NI MUNGU MWENYEWE. Ulimwengu hauna mwisho, na mambo yake yote hayana mwisho. Uwezo wetu wa kufikiri una mwisho na ndio tofauti yetu kati yetu na Mungu. Kwa akili zetu hatuwezi kuyajua yote kwasababu sisi sote ni WANA WA ADAM.

Hili ni jukwaa la intelligence!

Mahubiri peleka majukwaa ya dini
 
Kumbe huyo Allah ni wa kike?
Hebu nielezee vyema mkuu huu umalkia wake ulianza lini au aliupataje pataje, je kuna mfalme pia hapo pembeni yake?

Aisee! Hata mimi naanza kushangaa.
 
nashindwa kuelewa how you guys mnaweza amini kuwa there is no the almighty GOD (the creator)
 
Hivi kwanini kuna watu wanaamini kuna mungu na kuna watu wanaamini kuwa hakuna mungu? tangu enzi hizo kumekuwa na mvutano huu si jambo la jana wala juzi kuwepo kwa mvutano huu. Haiwezekani pande zote mbili zikawa sawa lazima kuwe na upande ambao ndiyo uko sahihi na mwengine hauko sahihi,lakini mbona hadi leo mvutano huu hauishi kwa kujulikana ni upi upande sahihi?
 
Ni jambo jema na linalopendeza kwamba hapa JF kuna wasomi wengi na wazuri,na hasa masuala ya sayansi.Mimi nimeishia darasa la saba.Bila shaka nitapata elimu.
Nina maswali matatu kwenu mnaokanusha uwepo wa Mungu kwa hoja za kisayansi:
1.Ni wapi/nini/nani asili au chanzo cha sayansi?
2.Hao wanasayansi wametumia uwezo mkubwa wa akili katika tafiti zao.Je,ni wapi asili ya huo uwezo wao wa kiakili?
3.Ni kwanini basi kwa uwezo wao huo wameshindwa kubuni mkakati wa kisayansi ili wasife au kuurudisha uhai?

ukiisha fahamu kwamba mungu alimpa mwanaadam free will ya kusema na kuamini anacho kiamini hakuna tena swali hapo la kutaka kujua mungu yupo au hayupo maana jibu ni yupo ila kampa mwanadamu maamuzi ya kuamua kumtambua ama kutomtambua,
hivyo wasio mtambua mungu kwa mungu wapo sahihi maana wanaingia kwenye neno mungu kawapa uwezo wa kuchagua jema au baya, iwapo akitumia uwezo wake kuzuia maovu atakua amekiuka Uhuru alio mpa mwanaadam
 
Back
Top Bottom