Mwezi wa Ramadhani umeingia Masheikh wako Jela

Mwezi wa Ramadhani umeingia Masheikh wako Jela

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Tunakwenda mwaka wa saba au nane, Masheikh wasio na hatia wako Jela.

Waliwekwa ndani na Kikwete, Wakakandamizwa ndani na Magufuli, na Sasa Samia anakaribia Mwezi mmoja madarakani bado serikali yake imewaweka Jela.

Siyo masheikh wa Uamsho tu, kuna mamia kwa mamia ya Masheikh nchi nzima wasio na hatia wamewekwa ndani na utawala uliopita wa Magufuli.

Sasa Silaha ya hawa watu ni moja, Wataendelea Kumlilia Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma kwa dhulma wanazotendewa
Watasimama visimamo vya usiku, Watafanya visomo, Watafanya Kunuti, Watafanya dhikri sana, na Watafunga wakiwa jela.

Ole wao Madhalimu wenye kudhulumu watu hawa wa Mungu, Mungu atalipa kwa kila hadaa, kwa kila uongo, kwa kila dhulma waliyofanyiwa.

Namkumbusha Rais Samia, Rais Hussein Mwinyi kwa Ujumbe wa Mwenyezi Mungu aliompa Nabii Musa amfikishie Firauni kumtaka awaachie huru wana wa Israel.

Mwenyezi Mungu anasema:

"Arsil ma'anaa banii israil walaa tuaddhib humaa".

maana yake : " Waachie huru wana wa Israel na wala usiwaadhibu".

Na mimi nakueleza Rais Samia na Hussein Mwinyi, Waachieni huru watu hawa wa Mungu na wala msiwaadhibu.

Ujumbe huu nimekufikishieni, basi ni juu yenu kuupuuza au kuufanyia kazi, maana hatuombi tena, kama kuomba muwaachie hawa watu kwa miaka minane hamkufanya sasa TUNALIACHA JAMBO HILI MIKONONI MWA YULE MWENYE NGUVU ZOTE.
 
Hoja yako ingenoga kama ungewasemea wote walio magerezani kwa kubambikiziwa kesi...

Hii kuwatetea mashehe peke yake imekaa kibaguzi sana...

Hebu karekebishe hapo ili nikugongee LIKE

Kazi iendelee, tusizinguane
[emoji106]
 
Mnao waoneaga huruma hawa magaidi hivi hamfuatilii kinachoendelea Msumbiji jinsi majitu type hii yanavyo chinja wenzao. Kuweni serious bhana

Unajua kuna baadhi ya watu ujinga ni sehemu ya maisha yao.Mashekh ni magaidi walitaka kuifanya Tanzania kama Somalia halafu kuna mijitu inakuja hapa kubwabwaja eti waachiwe!.

Kwa taarifa yenu mpaka Mwaka huu bado watu wana endelea kukamatwa kuhusiana na ugaidi wa Zanzibar,Arusha na huko kusini.Ukiona unakula ugali wako kwa amani basi elewa kuna watu hawalali usiku na mchana kuhakikisha taifa libakuwa salama.

Hao Mashekh na wengine wote wakioshiriki matendo ya kigaidi hawastahili uhuru kama mwanzisha mada ,yafaa waishi huko magereza maisha yao yote.
 
Unajua kuna baadhi ya watu ujinga ni sehemu ya maisha yao.Mashekh ni magaidi walitaka kuifanya Tanzania kama Somalia halafu kuna mijitu inakuja hapa kubwabwaja eti waachiwe...
Naunga mkono hoja. Mashehe wa Uamsho chini ya Sheikh Farid ni hatari kama Osama.

Siku watakayoachiwa tu tutaanza kusikia, Kanisa limelipuliwa, padri kauliwa au kituo cha Polisi kimevamiwa.

Watanzania tuwe wakweli, matukio ya 2014 Mbagala, Bukoba na Zanzibar yalitia doa amani ya nchi yetu. Tanzania iko salama kwa mashehe kuwa rumande. Potelea pote
 
Back
Top Bottom