Mwigulu ajikanyaga Bungeni kuhusu kodi ya Tsh. Trilioni 360 za Makinikia ya Dhahabu

Mwigulu ajikanyaga Bungeni kuhusu kodi ya Tsh. Trilioni 360 za Makinikia ya Dhahabu

Acha utumwa wa kijinga mkuu! Ilikuwaje Accasia watoe hizo b 700?

Na unaposema ile ripot ilikuwa kinyume cha 7.0, unaushahidi upi wa hiki usemacho kwamba JPM aliichakachua?

Na ikiwa aliichakachua, basi ni vema pia, maana, Taifa lilinufaika na uchakachuzi ule hadi tukapata hizo 700b za kujenga vituo viwili vya afya, na hiyo sio Kwa faida Kwa mchakachuzi, Bali ni Kwa watoto wa kitanzania na watoto wako wakiwemo
Nawewe sijui ulikuwa mchepuko wa bwana yule,maana unavyoangaika kumtetea utadhani umehaidiwa pepo
 
Acha utumwa wa kijinga mkuu! Ilikuwaje Accasia watoe hizo b 700?

Na unaposema ile ripot ilikuwa kinyume cha 7.0, unaushahidi upi wa hiki usemacho kwamba JPM aliichakachua?

Na ikiwa aliichakachua, basi ni vema pia, maana, Taifa lilinufaika na uchakachuzi ule hadi tukapata hizo 700b za kujenga vituo viwili vya afya, na hiyo sio Kwa faida Kwa mchakachuzi, Bali ni Kwa watoto wa kitanzania na watoto wako wakiwemo
Hao wana mimba zao za chuki kwa Mwendazake zilizogoma kukomaa na huyo kima (Lisu) wanaye muona wa maana naye alishawahi kuwa mwanasheria wa kampuni ya ACACIA,njaa tupu na ndio maana Lowasa aliwanunua.
 
Basis ya assessment ya 360T shilling dwelt on idiotic premises, I don’t believe TRA could stand in court to defend that madness and absurdity
 
Kila kukicha huyu mwigulu anazidi kuonyesha hiyo wizara haiwezzi zaidi ya ujanjaujanja!
Kwanza hata kujieleza kwa kujipambanua ni mzito saaaana!
 
Acha utumwa wa kijinga mkuu! Ilikuwaje Accasia watoe hizo b 700?

Na unaposema ile ripot ilikuwa kinyume cha 7.0, unaushahidi upi wa hiki usemacho kwamba JPM aliichakachua?

Na ikiwa aliichakachua, basi ni vema pia, maana, Taifa lilinufaika na uchakachuzi ule hadi tukapata hizo 700b za kujenga vituo viwili vya afya, na hiyo sio Kwa faida Kwa mchakachuzi, Bali ni Kwa watoto wa kitanzania na watoto wako wakiwemo

Haya mambo ni size ya wachumi, wahasibu na wataalamu wa biashara. Siyo kila mwana JF anayejua kiingereza anaweza kuinterpret.

Ninachikiona kilichobadilika kwenye mkataba wa Barick ni mrahaba tu kutoka I think 9% (au 6%) alizoacha JK hadi 16%. Lakini naye JK kuna kazi alifanya kwa kuwa wakati wa BWM ilikuwa 3%.

Hii economic benefit ni vague term. Ukisoma kwenye nadharia wanasema yaweza kuwa mapato yaliyopatikana, au gharama zilizookolewa. In short siyo kitu tangible kwa kuwa ni rahisi tu kuambiwa 'hatukupata economic benefits). Hiyo ni changa la macho ambalo negotiations team yetu chini ya Prof Kabudi ilibambikiziwa ikadhani ni kitu cha maana.

Mengine ya USD 190 Bilion maarufu kama Noah kwa kila Mtanzania imekufa na ilikiwa ni ndoto ya mwendawazimu au kwa lugha ya Tundu Lissu Professorial rubbish.

Ile USD 300 Million (Tshs 700 Billion) ilikubaliwa lakini kulipwa ni kwa miaka 6 minus madeni wanayoidai Serikali through VAT refund.

Makinikia yataendelea kupelekwa kama kawaida na Sheria za Tanzania hazitatumika kutatua migogoro, itabaki ni ile ile ya ICSID iliyoko London.

Halafu kuna kigingi kipya kimeongezeka kinasema Mkataba wa Barrick na Tz hautaathirika na sheria za madini zitakazotungwa baadaye.

ACACIA unaweza usiione kewnye logo lakini ACACIA ni Barrick na Barrick ni ACACIA. Makao makuu ya Barrick yako Toronto Canada. Kutokana na namna hizi multi nationals zonavyo manage biashara eapecially baada ya kuwa listed kwenye LSE, ilibidi waunde structure ya management ya shughuli zao London through ACACIA. So don't be fooled kuwa eti kampuni ya ACACIA iliyokuwa inatunyonya imenunuliwa. Bado ipo na kama ni kunyonya itaendelea.
 
?

Na unaposema ile ripot ilikuwa kinyume cha 7.0, unaushahidi upi wa hiki usemacho kwamba JPM aliichakachua
Ushahidi upo. Ripoti aliyosa siku ile Pro Mruma siyo original. Pili makontena ya makinikia bado yanasafirishwa, nenda ukapime au waulize wahusika wa TRA wakuambie kuna dhahabu kiasi gani
 
Haya mambo ni size ya wachumi, wahasibu na wataalamu wa biashara. Siyo kila mwana JF anayejua kiingereza anaweza kuinterpret.

Ninachikiona kilichobadilika kwenye mkataba wa Barick ni mrahaba tu kutoka I think 9% (au 6%) alizoacha JK hadi 16%. Lakini naye JK kuna kazi alifanya kwa kuwa wakati wa BWM ilikuwa 3%.

Hii economic benefit ni vague term. Ukisoma kwenye nadharia wanasema yaweza kuwa mapato yaliyopatikana, au gharama zilizookolewa. In short siyo kitu tangible kwa kuwa ni rahisi tu kuambiwa 'hatukupata economic benefits). Hiyo ni changa la macho ambalo negotiations team yetu chini ya Prof Kabudi ilibambikiziwa ikadhani ni kitu cha maana.

Mengine ya USD 190 Bilion maarufu kama Noah kwa kila Mtanzania imekufa na ilikiwa ni ndoto ya mwendawazimu au kwa lugha ya Tundu Lissu Professorial rubbish.

Ile USD 300 Million (Tshs 700 Billion) ilikubaliwa lakini kulipwa ni kwa miaka 6 minus madeni wanayoidai Serikali through VAT refund.

Makinikia yataendelea kupelekwa kama kawaida na Sheria za Tanzania hazitatumika kutatua migogoro, itabaki ni ile ile ya ICSID iliyoko London.

Halafu kuna kigingi kipya kimeongezeka kinasema Mkataba wa Barrick na Tz hautaathirika na sheria za madini zitakazotungwa baadaye.

ACACIA unaweza usiione kewnye logo lakini ACACIA ni Barrick na Barrick ni ACACIA. Makao makuu ya Barrick yako Toronto Canada. Kutokana na namna hizi multi nationals zonavyo manage biashara eapecially baada ya kuwa listed kwenye LSE, ilibidi waunde structure ya management ya shughuli zao London through ACACIA. So don't be fooled kuwa eti kampuni ya ACACIA iliyokuwa inatunyonya imenunuliwa. Bado ipo na kama ni kunyonya itaendelea.
Bila shaka tunakubaliana kuwa, b700 accasia alikubali kuzilipa baada ya mchakato wa mazumgumzo uliotokana na kwere kwamba, wamekuwa wakiiba madini yetu siyo!!

Swali ni!...

Iwapo accasia hawakuwa wezi wa madini, Kwa nini wakubali kulipa au vyovyote utakavyita, dolla 300m?
 
Bila shaka tunakubaliana kuwa, b700 accasia alikubali kuzilipa baada ya mchakato wa mazumgumzo uliotokana na kwere kwamba, wamekuwa wakiiba madini yetu siyo!!

Swali ni!...

Iwapo accasia hawakuwa wezi wa madini, Kwa nini wakubali kulipa au vyovyote utakavyita, dolla 300m?
Hivi wewe umefika japo Form 4? Mbona kichwa chako kigumu kuelewa? Je waalimu wako waliwezaje kukupasisha na kichwa kigumu hivyo?
 
Hivi wewe umefika japo Form 4? Mbona kichwa chako kigumu kuelewa? Je waalimu wako waliwezaje kukupasisha na kichwa kigumu hivyo?
Ukishindwa kujibu, maana yake unaongozwa na chuki!

Huongozwi na chuki, jibu maswali, na usipojibu maswali, ndio nyie JPM aliwatimua Kwa sabb ya vyeti vya kufoji na ndio maana umejaa chuki mkuu
 
Ukishindwa kujibu, maana yake unaongozwa na chuki!

Huongozwi na chuki, jibu maswali, na usipojibu maswali, ndio nyie JPM aliwatimua Kwa sabb ya vyeti vya kufoji na ndio maana umejaa chuki mkuu
Hata Magufuli alikuwa na PhD ya kufoji, njoo na hoja nyingine
 
Hawa maprofesa wa Makinikia wanatakiwa kuchunguzwa kama waliipotosha serikali na ripoti yao, kwani ripoti ya makinikia ilileta madhara makubwa ikiwemo maelfu ya watu kupoteza kazo, uwekezaji kusuasua kwenye sekta ya madini, serikali kupoteza mapato n.k
@ Mruma na Usoro hatuwezi kuwa na watu wanapotosha serikali na kufanya maamuzi kupitia taarifa ambazo sio sahihi...
 
Wengi wa Watanzania hasa wanaoitwa wapinzagiza, ni wajinga na mamburula,

Ni ujinga kusema 700b alizitoa Lisu Kutoka miga!

Jpm anapata kosa lipi hapo na wakati alipokohoa tu 700b zikaingia Kutoka huko Accasia!

Kwa hicho walichotoa, Accasia ni majizii au si majizi?

Mnataka na hiyo kesi ya 360t akaisimamie yeye?

Pumbavu zenu vilaza na wafoji vyeti!
Hazikuingia walilipa 100 tu zingine zitatolewa misaadavmika 7 kumbuka ni watavyojisikia , ile ripoti ya prof ishachanwa
 
Acha utumwa wa kijinga mkuu! Ilikuwaje Accasia watoe hizo b 700?

Na unaposema ile ripot ilikuwa kinyume cha 7.0, unaushahidi upi wa hiki usemacho kwamba JPM aliichakachua?

Na ikiwa aliichakachua, basi ni vema pia, maana, Taifa lilinufaika na uchakachuzi ule hadi tukapata hizo 700b za kujenga vituo viwili vya afya, na hiyo sio Kwa faida Kwa mchakachuzi, Bali ni Kwa watoto wa kitanzania na watoto wako wakiwemo
Trilioni 450 zililipwa?
 
Sakata la Makinikia limetinga bungeni baada ya Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuhoji kwa nini Serikali ilikubali kupokea Tsh. Bilioni 700 zilizotokana na kesi za malimbikizo ya madeni ya Makinikia badala ya Tsh. Trilioni 360 ambayo ni madai halali kwa Tanzania.

Mpina amehoji swali hilo la nyonge za katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni leo Alhamis, Septemba 22,2022.

“Kwa nini Serikali ilikubali kupokea Tsh. Bilioni 700 kutoka katika kesi za malimbikizo ya madeni maarufu kama makinikia badala ya Tsh. Trilioni 360 ambayo ni madai halali katika nchi yetu,”amehoji.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amesema Serikali haijakubali kupokea fedha hizo (Sh700 bilioni) na kuacha Sh360 trilioni, isipokuwa ilipeleka malalamiko kuhusu kampuni za madini.

Hata hivyo, kabla ya kumaliza kulijibu swali hilo, Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alimkatisha na kutaka ufafanuzi wa majibu ya Serikali yaliyotofautiana na swali la msingi lililoulizwa na Mpina.

Akijibu swali hilo, Waziri Mwigulu amesema Serikali haikupokea kimya kimya fedha hizo (Sh700 bilioni) na kuacha Sh360 trilioni bali kilichofanyika ni kwa Serikali kupeleka malalamiko kwenye kampuni za madini.

Lakini kabla ya kuendelea kujibu, alikatishwa tena na Dk Tulia akimtaka kwenda kwa mtiririko huku akimtaka Waziri huyo kueleza juu ya tofauti ya fedha zilizoandikwa katika jibu la Serikali na zilizotamkwa na mbunge ili aweze kutoa mwongozo.

Akitoa ufafanuzi, DK Mwigulu amesema Sh360 trilioni anazozungumzia Mpina ni za makinikia wakati katika jibu la swali la msingi, kiasi kinachozungumziwa cha Sh4.21 trilioni ni za mashauri mengine ya kodi.

Baada ya maelezo hayo, Dk Tulia aliitaka Serikali kumjibu Mpina tena kwa kadri alivyouliza swali lake la msingi.

Akijibu swali hilo, Dk Mwigulu amesema Sh360 trilioni haipo kwenye Bodi ya Rufani ya Kodi (TRAB) wala Baraza la Usuluhishi la Mapato ya Kodi (TRAT).

Amesema rufaa za kikodi ni mahususi na lilikuwepo kwenye mzozo wa Serikali na Kampuni ya Barick kwahiyo ni kitu tofauti.

Katika swali la msingi, Mpina amehoji nini kinachosababisha kesi 1,097 za kodi za muda mrefu zenye thamani ya Sh360 trilioni na Dola za Marekani milioni 181.4 kutoamuliwa hadi sasa.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Hamad Hassan Chande amesema

hadi Agosti 2022, kulikuwa na idadi ya mashauri 854 kwenye hatua mbalimbali za usikilizaji, yenye kodi inayobishaniwa ya jumla ya Sh4.21 trilioni na Dola za Marekani Milioni 3.48 katika taasisi za rufani za kodi ambazo ni TRAB na TRAT.

Amesema hivyo, kwa sasa TRAB na TRAT zinaendelea kusikiliza mashauri hayo pamoja na mashauri mapya yanayoendelea kusajiliwa.

Aidha, amesema kwa nyakati tofauti, idadi ya mashauri ya kodi hupungua au kuongezeka kulingana na kasi ya usikilizaji na usajili.
Ukweli anaujua ndio maana akababaika
 
Back
Top Bottom