Pre GE2025 Mwigulu: Anayeongea ndiye Waziri Fedha, mkirudi Majimboni waambieni Wajumbe wenu hakuna awamu imetoa pesa nyingi kama ya Sita

Pre GE2025 Mwigulu: Anayeongea ndiye Waziri Fedha, mkirudi Majimboni waambieni Wajumbe wenu hakuna awamu imetoa pesa nyingi kama ya Sita

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri wa Fedha, Mwigulu amejigamba Mbungeni kuwa "Anayeonge ndiye Waziri Fedha, mikirudi Majimboni waambieni Wajumbe wenu hakuna awamu tumetoa pesa kama awamu hii ya Sita

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

==
Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema hakuna awamu ambayo imetoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama awamu ya sasa inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Akichangia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Halima Mdee, Waziri Nchemba amesema anachokisema anakijua kwa sababu amekuwa kwenye Wizara ya Fedha tangu akiwa naibu waziri.

Amesema miradi inayotekelezwa katika majimbo ya wabunge ni uthibitisho wa fedha nyingi zinazoelekezwa kwenye maendeleo badala ya kubaki benki, kitu ambacho hata wao wanajua hakijawahi kuwepo.

Akitoa mfano, ameeleza kuwa mradi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere umetumia zaidi ya shilingi trilioni 6.5, kiasi ambacho ni sawa na bajeti ya maendeleo ya baadhi ya nchi.

Hata hivyo, Dkt. Mwigulu amekiri kuwa kuna maeneo ambayo bajeti haijatekelezwa kwa asilimia 100, akieleza kuwa sababu ni uchepushaji wa fedha kushughulikia majanga ya kibinadamu, kama maporomoko ya udongo yaliyotokea Hanang.

 
Alitaka kuzipeleka wapi kama siyo kwa wenyepesa zao wananchi? Ingekuwa serikali makini mtu kama huyu ni kumlima shaba tu...unakuwa na waziri wa fedha asiyejua kuwa pesa zinakusanywa ili iweje.
Inamaanisha kuna awamu pesa zinakusanywa ila hazipelekwi kwa wananchi?
 
Haya matapeli yanajua kusifia lakini huwezi kuyasikia yanazungumzia mfumko wa bei na thamani ya shilingi, mwaka 2021 bei ya petrol ilikuwa shs ngapi na sasa ni shs ngapi?
 
Kidogo nitupie middle finger nikakumbuka huku jukwaa la siasa ban nje nje
 
Alitaka kuzipeleka wapi kama siyo kwa wenyepesa zao wananchi? Ingekuwa serikali makini mtu kama huyu ni kumlima shaba tu...unakuwa na waziri wa fedha asiyejua kuwa pesa zinakusanywa ili iweje.
Inamaanisha kuna awamu pesa zinakusanywa ila hazipelekwi kwa wananchi?
Wivu.Kwani waliotangulia Kwa nini wao hawakuzitoa Kwa Wingi na kuzipeleka Kwa wenye pesa?

Hater 😁
 
Waziri wa Fedha, Mwigulu amejigamba Mbungeni kuwa "Anayeonge ndiye Waziri Fedha, mikirudi Majimboni waambieni Wajumbe wenu hakuna awamu tumetoa pesa kama awamu hii ya Sita

View attachment 3235330
Tunahitaji full disclosure. Watoe mchanganuo wa hiyo pesa kuonesha kiasi cha pesa yetu wenyewe, kiasi cha pesa tuliyokopa na kiasi cha pesa tuliyopewa na wafadhili kama msaada. Hatuwezi kuchekelea kupokea pesa ambayo ni financial burden ya kizazi hiki na vizazi vijavyo, kwasababu tutatakiwa kuilipa kwa waliotukopesha (kulingana na masharti yao)!
 
Halima mdee ndiye mwenyekiti wa LAAC?

Anamsifia Mwigulu Nchemba?

Nimeamini CCM haipotezi pesa.
 
Waziri wa Fedha, Mwigulu amejigamba Mbungeni kuwa "Anayeonge ndiye Waziri Fedha, mikirudi Majimboni waambieni Wajumbe wenu hakuna awamu tumetoa pesa kama awamu hii ya Sita

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

==
Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema hakuna awamu ambayo imetoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama awamu ya sasa inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Akichangia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Halima Mdee, Waziri Nchemba amesema anachokisema anakijua kwa sababu amekuwa kwenye Wizara ya Fedha tangu akiwa naibu waziri.

Amesema miradi inayotekelezwa katika majimbo ya wabunge ni uthibitisho wa fedha nyingi zinazoelekezwa kwenye maendeleo badala ya kubaki benki, kitu ambacho hata wao wanajua hakijawahi kuwepo.

Akitoa mfano, ameeleza kuwa mradi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere umetumia zaidi ya shilingi trilioni 6.5, kiasi ambacho ni sawa na bajeti ya maendeleo ya baadhi ya nchi.

Hata hivyo, Dkt. Mwigulu amekiri kuwa kuna maeneo ambayo bajeti haijatekelezwa kwa asilimia 100, akieleza kuwa sababu ni uchepushaji wa fedha kushughulikia majanga ya kibinadamu, kama maporomoko ya udongo yaliyotokea Hanang.

View attachment 3235330
Ili kuthibitisha tuunde "DEPARTMENT OF GOVERNMENT EFFICIENCY ".
Kama ya Elon Musk.
 
Waziri wa Fedha, Mwigulu amejigamba Mbungeni kuwa "Anayeonge ndiye Waziri Fedha, mikirudi Majimboni waambieni Wajumbe wenu hakuna awamu tumetoa pesa kama awamu hii ya Sita

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

==
Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema hakuna awamu ambayo imetoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama awamu ya sasa inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Akichangia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Halima Mdee, Waziri Nchemba amesema anachokisema anakijua kwa sababu amekuwa kwenye Wizara ya Fedha tangu akiwa naibu waziri.

Amesema miradi inayotekelezwa katika majimbo ya wabunge ni uthibitisho wa fedha nyingi zinazoelekezwa kwenye maendeleo badala ya kubaki benki, kitu ambacho hata wao wanajua hakijawahi kuwepo.

Akitoa mfano, ameeleza kuwa mradi wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere umetumia zaidi ya shilingi trilioni 6.5, kiasi ambacho ni sawa na bajeti ya maendeleo ya baadhi ya nchi.

Hata hivyo, Dkt. Mwigulu amekiri kuwa kuna maeneo ambayo bajeti haijatekelezwa kwa asilimia 100, akieleza kuwa sababu ni uchepushaji wa fedha kushughulikia majanga ya kibinadamu, kama maporomoko ya udongo yaliyotokea Hanang.

View attachment 3235330
Hizo fedha mbona hatuzioni hata zikitusaidia madawa,shule hazina vitabu,madawati n.k. Au mmeongezea ma bus ya mikoani!?
 
Mshangao na Uhalisia wa Miradi ya Maendeleo

Katika kipindi hiki, kuna hali ya kuvunja moyo katika usimamizi wa fedha za miradi ya maendeleo nchini. Mikoa inaonekana kujiweka katika hali ya kujisifu bila kuzingatia ukweli wa mambo. Ni vigumu kuelewa jinsi miongoni mwa fedha za maendeleo, ambazo zinasemwa kuwa ni bilioni moja kwa kila mkoa, zinavyoweza kutosha kujenga barabara hata kilometa 10.

Katika muktadha huu, tunaona mikoa ikitangaza kwa fahari kwamba imepata fedha hizi, wakati ukweli ni kwamba fedha hizo hazitoshi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya msingi kama vile ujenzi wa barabara. Kwa mfano, bilioni moja inaweza kusaidia kujenga kilometa moja tu ya barabara ya lami, na hii ni katika hali nzuri kabisa. Hii inamaanisha kuwa fedha hizi hazitoshi kukidhi mahitaji ya barabara katika maeneo mengi ya nchi.

Watanganyika wengi hawana ufahamu wa hesabu na thamani halisi ya fedha hizi. Wengi wanashindwa kuelewa jinsi fedha hizi zinavyoweza kutumika kwa ufanisi na kusaidia kuboresha maisha yao. Kila mwaka, tunashuhudia ahadi nyingi za miradi kutoka kwa viongozi wetu, lakini katika ukweli, ni vigumu kuona mabadiliko yoyote makubwa. Hali hii inazua maswali mengi kuhusu uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za umma.

Ni wazi kwamba kuna pengo kubwa kati ya kile kinachotangazwa na viongozi na kile ambacho kinatokea kwenye ardhi. Wakati viongozi wanapojivunia kutolewa kwa fedha hizo, watu wa kawaida wanakabiliwa na changamoto za kila siku, ikiwemo barabara mbovu zinazowafanya wasafiri kwa shida na kupata huduma muhimu kuwa ngumu.

Katika muktadha huu, ni muhimu kujiuliza: ni nani anayewajibika? Je, ni viongozi ambao wanajitahidi kuonyesha mafanikio yasiyo halisi, au ni mfumo mzima wa usimamizi wa fedha za umma ambao unahitaji marekebisho makubwa? Hali hii inahitaji ufumbuzi wa haraka.

Kila mwaka, tunasikia ahadi za miradi ya maendeleo, lakini ukweli ni kwamba fedha nyingi zinatoweka bila ufuatiliaji wa kutosha. Hii inatufanya tujiulize iwapo kuna uwezekano wa kuona mabadiliko yoyote ya kweli katika maendeleo ya nchi yetu. Ni lazima kuwe na mfumo mzuri wa ufuatiliaji na tathmini ya miradi ili kuhakikisha kuwa fedha zinatumika ipasavyo.

Watanganyika wanahitaji kuwa na ufahamu wa jinsi fedha za maendeleo zinavyotumika. Ni muhimu kwa jamii kuwa na sauti katika mchakato wa kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo. Hii inaweza kufanikishwa kwa kuwepo na uwazi katika usimamizi wa fedha na kutoa fursa kwa wananchi kushiriki katika maamuzi yanayohusu maendeleo yao.

Viongozi wanapaswa kuzingatia umuhimu wa kutoa taarifa sahihi kuhusu matumizi ya fedha za umma. Wananchi wanahitaji kujua ni vipi fedha hizo zinavyotumika na ni miradi ipi inatekelezwa. Hii itawasaidia kuelewa thamani ya fedha ambazo wanachangia kupitia kodi na kuhakikisha kwamba wanahusika katika mchakato wa maendeleo.

Kwa upande mwingine, ni muhimu pia kwa serikali kuwekeza katika elimu ya kifedha kwa wananchi. Hii itawasaidia kuelewa vizuri masuala ya fedha na jinsi ya kuhimiza uwajibikaji kutoka kwa viongozi wao. Wananchi wenye elimu ya kifedha wanaweza kuwa na uwezo wa kuhoji na kufuatilia matumizi ya fedha za umma, na kwa hivyo kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Kwa kumalizia, ni dhahiri kwamba kuna kazi kubwa ya kufanya ili kuboresha hali ya miradi ya maendeleo nchini. Mikoa inahitaji kutathmini namna inavyosimamia fedha hizo na kuhakikisha kuna uwazi na uwajibikaji. Watanganyika wanapaswa kuwa na sauti katika mchakato wa maendeleo na kuwa na ufahamu wa thamani halisi ya fedha wanazotoa. Hili ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa maendeleo yanapatikana na yanakuwa na maana kwa kila mmoja wetu.
 
Back
Top Bottom