Msaidie wewe mwenye elimu ya juu jinsi ya kupata pesa za maji vijijini,hospital za kutosha,barabara vijijini na kugharamia elimu maana kila siku mnazaa kama panya.

Vinginevyo ni porojo za kijinga tuu na maisha mtaani yanaenda.Harusi zinafanyika,fundi vyerehani wanazidi kupata kazi na Bar zinajaa.Wewe unaishi Tzn ipi amabyo haishiki? Unataka kodi ya maendeleo akulipie nani ili wewe utumie tuu?
 
Chadema mmeacha madai ya katiba mpya sasa mmehamia kwenye tozo za kodi ya kizalendo, kamwe hamto fanikiwa mnacho kitaka.
Hapa hapana chadema wala ccm hii kitu inaumiza kwa wanyonge wanaotumia hii miamala anotoka tu mbunge anasema kuwe na kodi ya uzalendo katika simu wakati yeye mshahara hauna kodi kwanini wasingeanza wao wabunge kodi ya uzalendo katika posho na mishahara yao kuliko kuwaumiza wanyonge, wengi wetu sisi wa tz ujinga wetu tunaanza kutizama vyama kuliko maendeleo yetu binafsi na ya nchi .
 
 
tulipee kodi hatuna namna
 
Hivi kila anayehoji vitendo vya serikali ni chadema tu? Haya mawazo ya ki chuma ulete ni sawa na ushirikina na kuendelea ni shida sana.
chadema ndio wana lengo la kuisumbua serikali yetu chini ya Rais wetu mpendwa.
nami nawashauri kamwe serikali yetu isikubali kuyumbishwa na kikundi cha wahuni wachache.
 
Chadema mmeacha madai ya katiba mpya sasa mmehamia kwenye tozo za kodi ya kizalendo, kamwe hamto fanikiwa mnacho kitaka.
Mwenzetu una ccm- pesa nini ambayo makato hayajaongezwa?
 

Mkisikiaga wengine wakiambiwa hakutakikani chokochoko basi muwe mnaelewa kuwa ndiyo kama huku kudai kilicho haki.
 
kwa hiyo unapenda vya buree eeehh!!!
unataka usadiwe na mataifa ya ulaya eeeh!!!
kumbuka pia misaada tunayo ipata kutoka nchi za ulaya ni KODI ZA WANANCHI WA MAREKANI, UGERUMANI, DENMARK, NEWZELAND, FRANCE, CHINA, UINGEREZA N.K, wananchi wazalendo wa nchi hizo wanatozwa kodi ambazo zingine ndio tunapewa ss misaada na wakati mwengine tunakopeshwa.
acheni kuwa walemavu wa akili lipeni kodi ili itusaidie maendeleo yetu.
Taifa imara itajengwa na sisi watanzania wenyewe kwa kulipa kodi sio kutegemea misaada au mikopo.
 
Watu wa mijini mnalia lia sana kama mnapimwa corona kwa kipimo cha mchina au kipimo cha tezi dume.Sisi wa vijijini tumemuelewa sana mama na Mwigulu kwa sababu hayo mapesa yatatuletea barabara za uhakika,yatatuletea maji ya uhakika,yatatujengea zahanati ,vituo vya afya na hospital na yatatujengea shule.

Nyie wa mjini hamjui tabu ya usafiri,hamjui kugombea maji na mifudo na vyura wala hamjawahi jifungulia njiani ukiacha mbali kulaliwa bei za mazao.So long as pesa itatusaidia ulalamishi wenu ni ujinga tuu.

Nitaamini kama uchumi ni mbaya siku ambayo nijija mjini nitakuta watu hawajengi,wanawake hawaendi saluni,Bar zimefungwa au daladala zimeacha kazi ila kama vyote vinafanyika ,nyie mnaopinga maendeleo yetu vijijini ni wapuuzi wa kupuuzwa na Serikali.
 
Wapumbavu sana hao,wanataka nani awalipie kodi? Mwisho wa mwaka muje muiulize Serikali kama pesa ilileta tija au hapana ila mimi huku niliko nimeanza kuona matangazo ya kazi za ujenzi ya kuzidi yaani.

Kwani hizo pesa zinaenda kuingia kwenye mfuko wa Mwigulu kwamba atatumia kwenye familia yake?
 
Chadema mmeacha madai ya katiba mpya sasa mmehamia kwenye tozo za kodi ya kizalendo, kamwe hamto fanikiwa mnacho kitaka.
MTU yoyote anayeikosoa na kuishauri serikali unamuona ni CHADEMA...AISEE CHADEMA IMEWAKAA KIASI HIKI?KWELI CHADEMA NI CHAMA PENDWA,KAMA MAJI TU USIPOYANYWA UTAYAOGA..POLENI
 
WANANCHI WA MAREKANI NA NCHI ZA ULAYA ZINAWASIKIA WATANZANIA kuwa hawataki kulipa KODI ETI WANATAKA WASAIDIWE!!!!
AISEE!
NGOJA WANACHI WENZETU WATUSIKIE! SIJUI WATATUONAJE, KWELI TUMEKOMAA AU TULIDEKEZWA MPAKA UKUBWANI?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…