Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Mwigulu anahubiri mambo ya misamaha mikubwa ya kodi na kodi za wajasiriamali wakati hata sasa hivi yupo wizara ya Fedha lkn hajafanya chochote,huyu mnafiki hana lolote tapeli huyu Mwigulu
 
tatizo ndani ya ccm hayo mambo ya ukawa hawawezi kuyakubali kamwe. mwigulu kazungumza mambo ya ukawa tupu.
Ni Mwigulu huyuhuyu huwa anapinga na kuponda Sera za UKAWA hasa CHADEMA kufa na kupona halafu leo tumuamini? Heri umuamini Malaya anayeuza mwili sio m....aya wa siasa.
 
Mwigulu hana lolote, anacheza na psychology ya watu, ndo maana alianza kuuelezea umasikini, akijua watu wengi wamepitia maisha yale, hivyo watasympathize nae, na amewapata. Wanasiasa wajanja sana! Lakin tukiangalia kwani viongozi wote waliopita na waliopo nani hajapitia maisha yale? Mtu kama mkapa aliekulia kusini kwenye umasikini wa kutisha mbona hakuja na style ya kuuelezea umasikini wake kama mwigulu? Utakuja kuona ni strategy. Lowassa mwenyewe nae kakulia familia ya kimasikini na kifugaji kama mwigulu, nae alie kama mwigulu? Umasikini wa umasaini na life style yao ni mbaya zaidi ya kina mwigulu. Hivyo strategy yake kwangu haina mashiko. Tatizo mtu yoyote wa ccm hawezi kubadili system iliyoko ndani ya CCM, nyerere mwenyewe alishindwa, sidhani kama huyu aje na maajabu yoyote. Watanzania kila ikifika uchaguzi wanaaminishwa na ccm kuwa kuna mtu amekuja kuleta mabadiliko! Lakini wanasahau ni uzao uleule wa nyoka. Kazi tulionayo ni kuibadili system, ccm inabidi iondoke, haijalishi anakuja nani na uongo upi...
 
Tuache ujinga na unafiki hapa, Mwigulu hafai na hana uwezo wowote wa kuwa mgombea Urais wa CCM, Kwa sababu alikuwa akilalamika, kukosoa tu mfumo wa sasa wa serikali na CCM na wakati huo huo akisahau kuwa yeye pia ni kiongozi wa juu wa serikali na CCM.

Yote kwa yote ameshindwa kujitetea kabisa kuhusu kashfa zinazomkabili mbele ya watanzania kama
1/Bomu la Arusha
2/Ushahidi wa kutengeneza kuhusu Ugaidi wa CHADEMA
3/Ushiriki wa kihuni katika bunge la katiba
4/Ahadi ya kuwakamata wasiolipa kodi katika wizi wa ESCROW
5/Kushindwa kutatua mgogoro wa wafanyabiashara kuhusu mashine za kukusanya kodi.
6/Kushindwa kuishauri serikali kuhusu kushuka vibaya kwa thamani ya shilingi.
7/Kushindwa kupambana na mafisadi bungeni, katika serikali na ndani ya CCM.
 
Wanabodi,

Tuweke ushabiki pembeni, kati ya watangaza nia watatu kati ya jana na leo, Mwigulu Lameck Nchemba is the most bonafide genuine mgombea so far, ukimuangalia huku unamsikiliza, utaiona his genuinity kutoka moyoni mwake ku practice what he preach na kiukweli nadhani kwa kati ya hawa watangaza nia so far, naamini Mwigulu can make the best president this nation has ever had tangu mwalimu Nyerere!.

Jee wewe mwenzangu ulibahatika kumsikia, unamuonaje?!.

NB Ku make the best president ni jambo moja, mgombea anayependwa zaidi so far ni Edward Lowassa, na mgombea the most experieced so fat ni Stephen Wasira, nikichukulia mchakato wa 2005 wakati JK alipochaguliwa, kama reference, assuming hawa watatu ndio wameingia tatu bora, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakipewa choice ya kuchagua between "the most loved", "the most experienced" and the "the best president", watachagua mtu anayependwa na watu, mtu atakayechagulika kwa urais na kuwatupa the rest, na hivi ndivyo JK alivyochaguliwa ile 2005 kwa sababu kwenye the finalist watatu, kulikuwa na "the most experienced" Dr. Salim, "The best Brain", Prof. Mwandosya, na "the good looking" Jakaya Kikwete, akapitishwa kwa hoja kuwa ndiye anayependwa na watu, as if mapenzi ya watu ndio uongozi wa nchi!.

JF has a role to play kuwaelimisha wananchi wetu waweze kufanya informed decisions kwenye choice of president, ili ifike mahali chaguo la mgombea wa CCM sio lazima ndio automatikally awe rais, wakituletea ule ujinga ujinga kama wa 2005, tunapiga tuu chini only if huko kungine kuna the better alternative!.

Ushauri wangu wa kwanza kwa wana JF, Mwingulu Nchemba is the man to keep watching seriously!.

NB. Kwa walionidhania mimi niko kambi fulani, uzi huu ni uthibitisho kuwa Pasco wa jf, hana chama, hana kambi, hana mtu, ila kuna watu anawakubali akiwemo yule 'jamaa yetu', hivyo sitarajii kuulizwa kama nimehama kambi kwa sababu sijawahi kuwepo kambi yoyote!.

Kiukweli mimi Pasco wa jf, nimeguswa na Mwigulu Nchemba!.

Vipi wewe?.

Pasco

Kuchanganyana tuu
 
Pasco Sio wewe tu hadi sasa kati ya watangaza nia mwigulu yuko juu ngoja tuendelee kuona tatizo mfumo Wa ccm unaharibu viongozi wazuri ambao huwa tunawaamini ndio hapo sasa ninapoichukia ccm na yeyote aliye ndani ya ccm. Nimeweka ushabiki pembeni

Unamfahamu vizuri huyo jamaa kama jimbo lake limemshinda nchi ataiweza?
 
Jana kaongea kama mjumbe wa UKAWA,tatizo lake wakiyasema kina Mnyika wanaonekana wasaliti,hata kuunga mkono hoja ya upinzani inakuwa dhambi kwao,sasa jana ameyarudia yote!!
 
MWALIMU Nyerere daima nitakukumbuka.Ule msemo wa Watanzania tunahitaji mabadiliko umeshatimia,tumeyakosa CCM tutayapata sehemu nyingine nayo ni UKAWA tu.Tuliona nafasi adimu wanazozipata hawataki kuzitumia.Hivyi suala la RICHMOND mpango wa VUA GAMBA ugetekelezwa nani angewasema vibaya CCM? likaja suala la EPA nayo ilikuwa nafasi adimu ya kuonyesha mnavyochukia rushwa mlivyolimaliza walioiba mabilioni hasa jamaa wa kiasia kesi zao zikaishia kwa JK sisi vibaka tulioiba kuku mwaka huo baado tumo gerezani.Likaja suala la TEGETA ESCROW hadi Ikulu ikahusishwa Mpigaji wetu CHENGE na kundi lake wakaibuka tena,Mwigulu akasema waliotupiga hata kodi hawajalipa hadi leo.MABADILIKO YA KWELI HAYATATOKA CCM yatatoka UKAWA,kubaki IKULU CCM labda mbinu chafu za Katiba Pandikizi zitumike na za JIRANI YENU NKURUZINZA
 
Kaiza safari kwa kuwajibu maasimu wake, hajaonesha njia za kupita, binafsi nampongeza Wasira
 
Some of these folks are just prisoners of the moment.

Subiri na dogo wa Makamba naye atangaze nia yake uone atakavyomwagiwa misifa.

Utasikia haya haya na hata zaidi kuwa yeye ndo anafaa kuwa rais. Utaambiwa jamaa ni kichwa sana, jamaa ana maono ya kimaendeleo, na upuuzi puuzi mwingine kama huo.

Watanzania ni watu wa kuvutiwa na vitu vidogo vidogo mno, wepesi wa kusahau, na warahisi wa kuamini mazingaombwe
.
That's it. You nailed it
 
Wanabodi,

Tuweke ushabiki pembeni, kati ya watangaza nia watatu kati ya jana na leo, Mwigulu Lameck Nchemba is the most bonafide genuine mgombea so far, ukimuangalia huku unamsikiliza, utaiona his genuinity kutoka moyoni mwake ku practice what he preach na kiukweli nadhani kwa kati ya hawa watangaza nia so far, naamini Mwigulu can make the best president this nation has ever had tangu mwalimu Nyerere!.

Jee wewe mwenzangu ulibahatika kumsikia, unamuonaje?!.

NB Ku make the best president ni jambo moja, mgombea anayependwa zaidi so far ni Edward Lowassa, na mgombea the most experieced so fat ni Stephen Wasira, nikichukulia mchakato wa 2005 wakati JK alipochaguliwa, kama reference, assuming hawa watatu ndio wameingia tatu bora, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakipewa choice ya kuchagua between "the most loved", "the most experienced" and the "the best president", watachagua mtu anayependwa na watu, mtu atakayechagulika kwa urais na kuwatupa the rest, na hivi ndivyo JK alivyochaguliwa ile 2005 kwa sababu kwenye the finalist watatu, kulikuwa na "the most experienced" Dr. Salim, "The best Brain", Prof. Mwandosya, na "the good looking" Jakaya Kikwete, akapitishwa kwa hoja kuwa ndiye anayependwa na watu, as if mapenzi ya watu ndio uongozi wa nchi!.

JF has a role to play kuwaelimisha wananchi wetu waweze kufanya informed decisions kwenye choice of president, ili ifike mahali chaguo la mgombea wa CCM sio lazima ndio automatikally awe rais, wakituletea ule ujinga ujinga kama wa 2005, tunapiga tuu chini only if huko kungine kuna the better alternative!.

Ushauri wangu wa kwanza kwa wana JF, Mwingulu Nchemba is the man to keep watching seriously!.

NB. Kwa walionidhania mimi niko kambi fulani, uzi huu ni uthibitisho kuwa Pasco wa jf, hana chama, hana kambi, hana mtu, ila kuna watu anawakubali akiwemo yule 'jamaa yetu', hivyo sitarajii kuulizwa kama nimehama kambi kwa sababu sijawahi kuwepo kambi yoyote!.

Kiukweli mimi Pasco wa jf, nimeguswa na Mwigulu Nchemba!.

Vipi wewe?.

Pasco

Kuna msemo wa kielimu unasema "UMAHIRI WAKO ONYESHA KWENYE MAANDISHI"
Mkuu....umeandikaa....umechambua....
 
Jamaa kaipiga madongo serikali kisawasawa! Yaani utafikiri yeye siyo waziri wa serikali na pia ndo katoka kujiuzuru unaibu katibu mkuu wa ccm!
 
Kama wakitokea watafiti wengine tena kuja kupima IQ za watanzania, atapata shock result maana atashangaa kutokuona hata hizo IQ zenyewe
 
Back
Top Bottom