Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Wengine tunaangalia hizi hotuba zao kama burudani tu, ni sehemu nzuri ya kuinjoi ufundi wa maneno.

Tumsubiri January atatisha zaidi, nategemea atakuja na movie ya miiko ya uongozi.
 
Mkuu, Nafikiri swali ni je unaweza kuthibitisha kwa ushahidi usio na shaka kuhusu hayo machache. Kisha tunaweza kujadili hayo mengi.

Hii ni fursa yetu wapiga kura kuwajua hawa watu vyema


Nikuthibitishie nini juu ya Mwigulu kutukana wapinzani kiasi cha JK kumsifia na kumpa vyeo?

Nikusimulie nini kingine kuhusu sinema ya Mwigulu juu ya ugaidi?

Ndugu unaishi nchi hii? mbona niliyoyasema yanajulikana Sana? usipende kutafuniwa tafuta utajua....

Au wewe ni miongoni mwa watu wanaosubiri kuwajua wagombea wakati Wa kampeni tu?

Kuweni serious ktk kufwatilia mambo ya nchi kwa ukaribu ili msikurupuke Kama hivi....
 
Imetulia hii Mpwa. Umekaa na kufanya yako kwa hekima na busara kubwa, hongera sana. Baadhi ya Watanzania ni wakurukupukaji kupita kiasi sijui kwanini huwa hawapendi kutafakari kwa kina kabla ya kukurupuka na kuandika yale ambayo hayastahili kuandikwa.

Tutaendelea kufanya makosa ya kuwapa mdaraka wasiostahili mpaka lini!? Kwanini hatutaki kujifunza kupitia makosa yetu ya miaka ya nyuma ili kuinusuru nchi yetu ambayo ilitakiwa iwe na maendeleo makubwa sana lakini inayumba miaka nenda miaka rudi kutokana na viongozi wasio na sifa hata moja ya kuliongoza Taifa letu, wezi, wanafiki, majangili, wauza unga, wapokea rushwa, waongo, wahuni n.k. Dah! inauma sana kuwasoma baadhi ya watu humu kwa jinsi wanavyokurupuka kila siku iendayo kwa Mungu.


Ahsante mpwa!!

Tutaendelea kufundishana ukweli....

UMASIKINI....UPUMBAVU.....UJINGA..... Wa wananchi Wa TZ ndio silaha kuu ya CCM kutawala mpaka Leo..
 
Bado sijajisikia hata msisimko kwa wote waliotangaza nia mpaka sasa .ile waooooooo waooooo waoooo na misisimko ya ngozi kwa kusikiliza hotuba bado sijapata .japo kiduchu mwigulu alitaka kunisisismua lakini kila nikimuangalia sura yake na maongezi yake ni tofauti.mpaka sasa tarehe 31 hatujapata msalary wa mwezi wa tano.sikui kama ataweza kuongoza nchi wakati a
Kawizara kadogo ka fedha kamemshinda.
Ata kwa Lipumba ujaona jipya,maana nae Katangaza
 
Lowassa watu hawampendi yeye, wanapenda fedha zake, kuwa mkweli Pasco.

Kibaya zaidi mkutano wa Jana Arusha umemvua nguo kabisa Lowassa kwa wale waliokuwa katikati.Mimi binafsi hata leo hii huyu bwana Lowassa asafishwe Richmond, simpi kura yangu kwa kuwa ni visionless, tired and outdated.

Eh! tupeni mipango na sisi tuzipate hizo fedha.

Lakini nakubaliana na wewe huyu mjamaa hana mvuto kwenye kuongea. Aende kwa rafiki yake JK au kwa Obama wakamfundishe kuongea.

Mimi kati ya watatu Mzee Wassira ndiyo ameniconvince kwani alikuwa na vision iliyoeleweka, na ameweka vipaumbele kwenye changamoto na jinsi ya kuvitatua.

Ila Mwigulu bado naona hana experience hata katika kueleza hoja kwani alikuwa akitoa maelezo tu hakuwa focused. Too many priorities hata akipewa miaka 20 hawezi kuzitatua
 
Hata akiwa most genuine tatizo mfumo wa ccm inawenyewe subirini mwicho wa mchakamchaka

Chama kipi hakina wenyewe Tanzania?Chadema yenyewe ina wenyewe kama ilivyo CUf ya wenyewe.

Tuangalie mtu, ukiangalia vyama utapotoka.Kwa nchi za kiafrika ni kiongozi mkuu ndiye anayeweza kubadilisha hali.Ukimtazama Mwigulu unaona kabisa kuwa yupo serious na anakerwa na yanayotukera.
 
Mimi sikuweza kusikiliza hotuba ya Mwigulu kwa muda mfupi lakini niseme kwa dakika hizo kama tano hivi alinivutia mno....anajieleza kwa ufasaha na anamiliki jukwaa. I was very very very disappointed na Comrade Lowassa jana. Jamani kuna nini kumuhusu Lowassa?! Yaani alishindwa kabisa kulimiliki jjukwaa. Speech yake ilikuwa imeandaliwa na anasoma utadhani mkuu wa mkoa au wilaya anasoma hotuba mbele ya Rais. Wasaidizi wake walishindwa hata kuandaa jukwaa na vipaza sauti. Kila muda walikuwa wanagonga gonga vipaza sauti...Lowassa aliomba wimbo gani ule wa Komba lakini haukutokea...Sijui nani yule alikuja na helikopta....aliyepaswa kuja na helikopta ni Lowassa na sio mwingine. Yaani wasaidizi wake hata protocol hawajui. Lowassa ameshafika jukwaani mwingine anaingia na helikopta what is that????? yaani wasaidizi wake wanapita pita jukwaani mara kibonde mara yule aliyevaa kofia kama ya kinana. hawakujiaandaa It is a disaster kwa Lowassa It is possible wanamhujumu. Kwanini Lowassa asiwe na tmu nzuri? Yaani akiingia kwenye mdahalo......

Haa ha ha Lowassa kichwani mtupu na mdomo pia ndio hivyo ata kutoa hotuba hawezi.

Yeye Lowassa kampeni anafanya kupitia pesa tu, zaidi ya hayo hakuna lolote.
 
Itakuwa Pasco alitegemea atapewa kazi ya kigawa vibahasha kwa Lowassa akapigwa chini.

Inabidi ajaribu bahati yake kwa Mwigulu.

Tukirudi kwenye mada, ni mapema sana ku judge, ngoja na wengine wote wanaojinadi watakapoisha.

ndiyo maana mtoa mada kasema so far. mkuu Pasco nafikiri tuanze kumwita Mwigulu ex machina. ccm sidhani kama wana mtu mwingine atayewaweza wapinzani kwa hoja zaidi ya mwigulu.
 
Last edited by a moderator:
Mwigulu tatizo ni huo upande aliopo..

"kutokana na umuhimu wa hii hutoba naomba niisome" EL, May 30, 2015 Arusha.

Yule mzee wa jana maskini hata ubongo haumruhusu kukariri tena, akaamua kutusomea maandishi tu teh teh teh
 
Wanabodi,

Tuweke ushabiki pembeni, kati ya watangaza nia watatu kati ya jana na leo, Mwigulu Lameck Nchemba is the most bonafide genuine mgombea so far, ukimuangalia huku unamsikiliza, utaiona his genuinity kutoka moyoni mwake ku practice what he preach na kiukweli nadhani kwa kati ya hawa watangaza nia so far, naamini Mwigulu can make the best president this nation has ever had tangu mwalimu Nyerere!.

Jee wewe mwenzangu ulibahatika kumsikia, unamuonaje?!.

NB Ku make the best president ni jambo moja, mgombea anayependwa zaidi so far ni Edward Lowassa, na mgombea the most experieced so fat ni Stephen Wasira, nikichukulia mchakato wa 2005 wakati JK alipochaguliwa, kama reference, assuming hawa watatu ndio wameingia tatu bora, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakipewa choice ya kuchagua between "the most loved", "the most experienced" and the "the best president", watachagua mtu anayependwa na watu, mtu atakayechagulika kwa urais na kuwatupa the rest, na hivi ndivyo JK alivyochaguliwa ile 2005 kwa sababu kwenye the finalist watatu, kulikuwa na "the most experienced" Dr. Salim, "The best Brain", Prof. Mwandosya, na "the good looking" Jakaya Kikwete, akapitishwa kwa hoja kuwa ndiye anayependwa na watu, as if mapenzi ya watu ndio uongozi wa nchi!.

JF has a role to play kuwaelimisha wananchi wetu waweze kufanya informed decisions kwenye choice of president, ili ifike mahali chaguo la mgombea wa CCM sio lazima ndio automatikally awe rais, wakituletea ule ujinga ujinga kama wa 2005, tunapiga tuu chini only if huko kungine kuna the better alternative!.

Ushauri wangu wa kwanza kwa wana JF, Mwingulu Nchemba is the man to keep watching seriously!.

NB. Kwa walionidhania mimi niko kambi fulani, uzi huu ni uthibitisho kuwa Pasco wa jf, hana chama, hana kambi, hana mtu, ila kuna watu anawakubali akiwemo yule 'jamaa yetu', hivyo sitarajii kuulizwa kama nimehama kambi kwa sababu sijawahi kuwepo kambi yoyote!.

Kiukweli mimi Pasco wa jf, nimeguswa na Mwigulu Nchemba!.

Vipi wewe?.

Pasco

Kuguswa ni haki yako, lakini busara kidogo tu ilipaswa kukukumbusha kuwa tangu tupate uhuru Tanzania haijawahi kuwa na uhaba wa wanasiasa wanaojua kuongea nini wananchi wanataka kuskia. Huyu Mwigulu ni mhuni wa kisiasa tu, anacheza na maneno. Where has he been miaka yote hii? Huo uchungu kwa Tanzania ni wakati huu anaoutuzuga kuwa anaweza kutuongoza? Don't be fooled kirahisi hivyo. How many times umewahi kuhudhuria interview kwa employer you hate to death lakini ukauelezea wasifu wake kana kwamba wazungumzia malaika?

Hebu tuhabarishe, ukiweka kando kuguswa na maneno yake, kuna kipi katika CV yake cha kuwapa matumaini Watanzania kuwa 'tumepata sokoine mwingine'?

And by the way, Mwigulu ni Plan B ya Lowassa Raia Mwema - Lowassa kuhamia Ukawa?
 
Chombo Kikubwa cha habari kama JF kinashindwa kutuwekea video clips za hotuba za watiania!!!

Pamoja na kwamba sijapata nafasi ya kusikiliza hotuba za watiania kupitia CCM, sidhani kama kuna anayeweza kudhubutu kua-address ama kuazimia kurejesha mezani RASIMU YA KATIBA MPYA ya Mzee Warioba - ambayo ndio mwarobaini wa matatizo yanayolikabili tiafa hili.
 
Mwigulu tatizo ni huo upande aliopo..

"kutokana na umuhimu wa hii hutoba naomba niisome" EL, May 30, 2015 Arusha.

Yule mzee wa jana maskini hata ubongo haumruhusu kukariri tena, akaamua kutusomea maandishi tu teh teh teh

Haa ha ha...mkutano wa jana badala ya kumjenga ndio kwanza umemvua nguo
 
Pasco ndugu yangu! Hapa suala siyo mtu mzuri! Huyu kijana amegusa wengi lkn msiba wetu upo kwenye mfumo!!! Ataongoza chini ya chama twawala sasa yooote mazuri aliyotugusa nayo ikiwa ni pamoja na kuonyesha u-serious waks wakati wa kutangaza nia ni kazj bure! Tatizo hapa ni mfumo na siyo mtu! Mara ngapi mwigulu amelia na ufujaji wa fedha kwenye sherehe na matukio yasiyo na tija lkn ccm wameendelea kuchezea hela za walalahoi bila hata chembe ya huruma!
 
Back
Top Bottom