Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Bila kujali itikadi za kichama, Mwigulu Nchemba ndo mtia nia pekee katika chama cha kijani (CCM) ambae anaongelewa kila kona ya nchi, magazeti na mitandao ya kijamii yameandika juu ya huyu mtia nia kwa kiwango cha juu kuliko mtia nia yoyote ndani ya chama hicho.
Katika jamii forum pekee zaidi ya michango takribani 2000 imelekezwa juu ya Nchemba toka jana siku ambayo mtia nia huyu alikuwa anatangaza nia yake ya kuusaka " unyerere" katika nchi hii. Michango hii inajumuisha michango yote inayomuunga mkono na ile yenye kumkosoa.
Swali: Je, hii ni ishara kuwa Nchemba ndo atapewa kuipeperusha bendera ya CCM kuelekea ikulu?


Mimi ni CUF lakini Mwigulu nimemkubali sana na katika watia NIA wote yeye peke yake ndio amenishawishi kama atakuwa Rais nchi anaweza kuipeleka mahali pazuri. Si mtu anayefuata au kulishizwa maneno ana misimamo madhubuti.

Nimemsikiliza Lowasa na Wassira Zaidi nahisi watanganyika wanampenda sana Lowassa lakin katika hutuba zao ni kama maneno ya kwenye redio tu hakukua na mikakati madhubuti ni kama vile JK alivyotaka kuingia madarakani tu.
 
Hayo mambo yote aliyosema Mwigulu yamekuwa yakipigiwa kelele na upinzani kwa muda mrefu, lakini chama chake kimeshindwa kuyagusa yeye akiwa miongoni mwao. Sidhani kama ataweza kuwa na jipya, kwao ni business as usual tu. Angekuwa nje ya System ningeweza kuwa na imani nae japo kidogo, lakini ndani ya CCM hamna kitu. Ili tutoke hapa tulipo tunahitaji mabadiliko ya uongozi kuanzia mtu na chama pia. Hata awe na sifa kama malaika, mtu aliye ndani ya CCM hawezi kuitoa Tanzania hapa ilipo. Hii ni kutokana na mifumo ya utawala ya CCM. JK Wakati anaingia alikuwa na ari, nguvu na kasi kama alivyokuwa anasema, lakini amechemsha..!
 
Ni upumbavu kuamini kwamba Mwigulu ndo anafaa kuwa rais Wa.awamu ya 5, eti kwa kigezo tu ni Mtoto Wa masikini! Punda mpaka alituonesha mpaka baba yake jinsi alivyo choka mbaya, sasa Mtoto Wa mkulima katufanyia nini cha maana? Pia ni upumbavu kuamini kwamba rais mzuri atatoka ccm peke yake awamu hii tunalipa hata jiwe almradi mkoloni mweusi akae mbali na ikulu yetu! Tutajipanga baadaye huko mbeleya safari!
 
weka mahaba niuwe pembeni, mwigulu yupo vizuri saaaana ni aina ya rais anaetakiwa kwa sasa. mabadiliko ni matendo na muda ni sasa. CCM kama wanajitambua wasifanye kosa la kumkataa mwigulu kwakua yeye pekee ndio nimemuona anajua shida zetu na njia ya kuzitatua. wengine wanaongea siasa tu
 
Hakuna mtu Genuine CCM ni wale wale, mabingwa wa kuzilelezea shida zetu mkiwapa madaraka watakuja kuwaeleza kitu kile kile wakati wa uchaguzi.

Umenena mkuu ccm imejaa siasa za danganya toto. Nchi ya Nigeria waziri wake wa kilimo amefanya mapinduzi makubwa. Hapa kwetu waziri wa kilimo - Wasira hajafanya lolote lakini anadai kuwa ataleta mapinduzi ya kilimo akipewa urais. Alichofanya wizarani kwa vipindi vyote alivyokuwepo ni nini? Chepi kitamfanya alete mapinduzi kama akiwa waziri wa kilimo hakuna la kujivunia? ccm ni yale yalee
 
....

Kati wa watangaza nia hawa watatu, kuna mgombea anayependwa sana na watu na huyu sii mwingine bali ni ni Edward Lowassa, jee ni kwa nini Edward Lowassa anapendwa sana, sababu zinajulikana!, ila kama urais ni kupendwa basi rais wetu ni Lowassa!.

.........


I beg to differ brother! Sema mwenye pesa na uwezo wa kukusanya watu wengi, kuna tofauti kati ya kupendwa na kukusanya watu wengi
 
Umenena ukweli tupu bila kubakisha kitu Pasco wa JF,me niko upande wa Mwigulu toka kitambo hajatangaza nia...,ila najua kwa mwaka huu hawezi pewa urais kwa CCM...
 
Vipi, Mwigulu mwenyewe si yupo hapa JF? Mbona hajakugongea like!
Hayo ni maneno hata kwenye kanga yapo. Huyu anakosoa sehemu kubwa ya sera za chama chake wakati tunamjua siku zote amekuwa akiwadhalilisha wanasiasa wa upinzani pale wanapozikosoa.
Ataongea maneno mazuri kama wenzake na matendo yatakuwa ni yaleyale, tunataka mabadiliko sio katika kuongea bali kutenda!
 
mimi nadhani Mwigulu hakujua kama atakuja kumbea urais hadi alipojiona ni maarufu ghafla,

1. angejua asingekuwa anaropoka au kutoa kauli chafu tena kana kwamba sio msomi.
mfano ccm ni ng'ombe wananchi ni ndama. mkikataa kutujagua udiwani mtakufa maana tutagoma kuwanyonyesha. Ni kazi ya srikali kumuudumia kila mwananchi bila kujali dini wala itikadi. ulitereza hapo mkuu.

2. Kama raia mwema kudai kuwa anaushahidi wa ugaidi huku akishindwa kuupeleka polisi, tena hata polisi kumuhoji ni udhaifu na kutafuta umaarufu mwepesi wa kisiasa.

3. kama Mwanasiasa mzarendo hakupaswa kuongea yale ambayo huwa anayapinga kisa kutetea ccm hashindwi kutetea mafisadi akiwa rais. Kigeugeu.

4. Herikopta ya msukuma ndio aliitumia kujitafutia umaarufu kule moro, wakati huohuo huyo jamaa ni mfuasi mkubwa wa EL. inanipa picha kuwa kuna uwezekano hawa lao ni moja.

5. Bingwa wa siasa chafu, Kutembea na Mtu aliyemwagiwa tindikali ili kuwatisha wananchi ubaya wa wapinzani wakati alipaswa kuwaeleza nini SERA zake na atatekeleza vipi.

6. Kama ukiwa na elimu ya Masters ulishindwa kubuni njia ya kisomi ya kujipatia Kipato (labda kama ulisoma elimu mbaya) ukaenda kubeba zege, nilitegemea labda ufanye kazi ya kuandika proporsals, projects, au hata kutafuta nafasi ya kufundisha ktk mamia ya shule hapo jijini,. utawezaje kubuni miradi au mawazo ya kuondoa umasikini kwa graduates hususani kipindi ambacho hata kupata internship ni kazi.(msoni ni yule anayetumia elimu yake kujikwamua kimaisha kwa mtazamo wangu mimi ambaye sijaenda shule)

7. Siku moja ukiwa umejaa jazba bungeni ulitamani kupata japo nafasi ya urais ili uwashughulikie wapinzani na watu waliokuwa na mawazo tofauti na yako. Hadi ukasiema usingekuwa waziri ungeongea maneno mabaya zaidi(jinsi nilivyokuelewa). Sasa ilinitisha kidogo kwa jaribu dogo tu lilikutoa kwenye mstari, je ukikabidhiwa nchi?? You need time to convince people that you are new Mwigulu.

Maoni yangu: Mwigulu wa leo sio kama wa miaka iliyopita. Unaonekana unakuja kama mkombozi lakni inabidi upate muda tujiridhishe vizuri kama kweli umebadilika au unatumia sifa mbaya ya USAHAULIFU wa wachache kutimiza malengo yako kisiasa.

yote kwa yoe, Nakupongeza kwa kutangaza lakini fanya marekebisho, kama unafaa siku ikifika utakuwa.

Hapo kwenye nyekundu,unawazungumziaje chadema inayongozwa na mbowe walipotutangazia kua wanamfahamu aliyerusha bomu pale Arusha!?
 
Nakubaliana na wewe Pasco kuwa kwa kusikiliza sera zao wote watatu wakati wanajinadi ni kweli kwa juujuu Mwigulu alijieleza vizuri na alivutia, lakini ukiangalia kwa undani sana,critically hamna kitu ni uongo uleule wa ma CCM kwa sababu hakuna alipoelezea strategies bali kila kitu ilikuwa ni ahadi tu, nikichaguliwa nitaweka utaratibu maalum kuzuia rushwa-UPI?, Nikichaguliwa elimu na afya-How? By the way kumbuka kiongozi utakayemuona ana maneno mazuri siyo kiongozi huyo kwa sasa Tanzania hatuhitaji maneno mazuri tunataka utendaji, kazi kwa kwenda mbele. Kwa maoni yangu Lowassa ndo hakuzungusha maneno wala hakuweka ujanja ujanja isipokuwa sidhani kama chama chake watampa nafasi kwani wanamuogopa ana hasira anaweza kuja kufunga watu ikithibitika walifuja fedha za umma
 
Huwezi kuwa rais alaf una singizia wapinzani magaidi mwigulu bado sana hawez kuwa rais labda rais wa bongo movies
 
Very true,Mwigulu Nchemba is the only man who can take Tanzania to higher levels.He told us how he will bring our Tanzania there,there where China,India ,Brasil are.Viva MWIGULU you are a visionary Leader.

Hakuna mtu anaeweza kututoa hapa tulipo ambaye yupo kwenye system ile ile watu wale wale mawazo yale yale washauri wale wale we need to change system must change Kwa kuwapa nafasi chama kingine wake na mawazo mapya mfumo mpya na mbinu mpya za kutupeleka hukoo juu
 
Hapo kwenye nyekundu,unawazungumziaje chadema inayongozwa na mbowe walipotutangazia kua wanamfahamu aliyerusha bomu pale Arusha!?

mkuu kosa ni kosa afnye Mbowe au Jk au Mwigulu ni kosa. Kwa sasa tunapoongelea nafasi kubwa ya nchi na muhusika anajitanabaisha kama mpiganaji na mleta neema mpya. Maneno mazuri hayatoshi na mwenendo wake past, future na present lazima tujiridhishe. Vinginevyo afafanue vizuri wao wakifika wakati wao nao lazima watueleze pia mkuu
 
Very true,Mwigulu Nchemba is the only man who can take Tanzania to higher levels.He told us how he will bring our Tanzania there,there where China,India ,Brasil are.Viva MWIGULU you are a visionary Leader.
Like he wasnt in the government,that there was no way he could have done all of that ,like he couldnt aid his president on those issues? be real !once CCM always CCM ! you will sing and dance same old tune unless uniambie wanakuja na ilani na sera tofauti kabisa ,period!
 
Katika siasa ikija kwa uchaguzi huwa ni hayo wanayoongea na kuingia wananchi.

Hata mie naona ile ya kuongelea familia itagusa wengi na yeye.

Inaonekana ameshajisafisha na kubadilika na sio yule niliyemjuliaga kwa maneno machafu na ugangwe.

Tunasubiria kuyasikia
 
Pasco,

Niliweka kitu kuhusu rais Anayetufaa vs Mbio za kupokezana vijiti, naona imefapigwa ban pengine kuna maneno yanayokiuka sheria. Wahusika tafadhali naomba hata copy yake maana mimi huandika pasipo kuacha nakala mahala popote zaidi ya hapa hivyo naomba nitumie ktk PM yangu.
 
Pasco,

Niliweka kitu kuhusu rais Anayetufaa vs Mbio za kupokezana vijiti, naona imefapigwa ban pengine kuna maneno yanayokiuka sheria. Wahusika tafadhali naomba hata copy yake maana mimi huandika pasipo kuacha nakala mahala popote zaidi ya hapa hivyo naomba nitumie ktk PM yangu.
Mkuu Mkandara, kwanza pole!, inawezekana wameiunganisha mahali, niliwahi kushauri thread ikiunganishwa, thread starter awe notified!.

Pasco
 
Mkuu Mkandara, kwanza pole!, inawezekana wameiunganisha mahali, niliwahi kushauri thread ikiunganishwa, thread starter awe notified!.

Pasco
Pasco
Unasemaje kuhusu mtu wetu kwa pigo hili la leo? Naona mpigaji anashusha zile za "Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini".
Je kuna ufufuo na uzima tena kwa "the chosen"?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom