Mwigulu ni almasi ya Tanzania

Nimeshuka chini moja kwa moja kuangalia kama kuna namba ya simu. Watakusoma wengine.
 
Mmeshalipwa kuja kuleta uchawa humu
 
Punguza njaa
 
Chawa kazini

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app

Kwenye mkutano wa kariakoo Mwigulu na huyo mama wa viwanda wamevurugwa sana. Kila msemaji aliyesimama hakuna aliyetoa maneno mazuri kwa hao wawili!! Ingekuwa nchi zenye heshima kiutawala hawa wawili wasingeendelea kuwa kwenye Cabinet. Lakini kwa vile Samia hathamini ushauri wa wananchi kama ule waliompa kwenye ule mkutano basi aendelee kuwadharau kwani atakapokuja kuomba kura tena Mungu akimjalia asije shangaa watavyompokea!!Wananchi wamechoka na maisha ya chini huku kodi zao zikichezewa kama vile kihenge hakina mwenyewe!
 
Nipe namba ya simu ya mmiliki wa Esther luxury coach.
 
Ni aibu kwa kijana kama wewe kuongea vitu vya kipuuzi kama hivi.
Kwanza wewe hujui sera za CCM,ulikuwa CHADEMA muda si mrefu.
Nikwambie kuwa SAMIA atatawala miaka 20.
 

Huyu ni Mwigulu mwenyewe kajiandikia, anajiita Dokta wa uchumi, hizi ndio tabia za Mwigulu, badala ya kutatua matatizo ya wafanyabiashara ambazo zimesababishwa na sheria mbovu, anaanza kujiandika mitandaoni ili kujionyesha yeye ni mzalendo, wakati ni hovyo sanaaa..

Mwigulu ataua biashara nyingi sana kwa kwa sheria mbovu na hazifai za fedha, na hajui biashara hata kidogo, na hajui akiua biashara, kesho serikali itakosa kodi kabisa.

Mwigulu anatumia mitandao sasa kujisafisha, eti watanzania wabantu ni wakwepaji kodi na watoa rushwa, eti watanzania wahindi au waarabu ndio walipaji wazuri wa kodi na kuhifadhi hesabu zao vizuri, haya ni matusi, na kama psychology ya Waziri wa Fedha ndio hii, basi hatuna mtu wizara ya fedha kabisa, haya maandiko ni ya Mwigulu kabisa ili tu kupingana na uhalisia wa wafanyabishara wanao pitia, na biashara zitakufa kwa mentality ya waziri wa aina hii.

Waziri Mkuu anahangaika sana kutatua matatizo ya wafanyabiashara sbb ya Waziri mbovu wa fedha
 
Kuikosoa makala hii unapasa kwanza uwe mzalendo wa Tanzania, pia uwe na facts za kutosha.
Unadai "facts", na huku makala yenyewe haina 'facts'?

Umeandika mambo kijumla jumla tu, lakini wewe unadai 'facts', hii si ni hayo hayo mambo ya "KiTanzania Pekee" uliyodai?

Kuhusu utetezi wako wa Mwigulu, hapa ninakupa 'benefit of doubt'.
Binafsi naanza kumtizama Mwigulu katika mwanga tofauti na ule niliokuwa nauona huko siku za nyuma.

Inawezekana kabisa mkasa huu ndio ukamjengea heshima zaidi kuliko aliyowahi kuwa nayo hadi sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…