Mwingira amlaani mchungaji Loliondo!

Kudadadeki hivi kumbe ndo upande wa pili wa anayejiita "mtume na nabii"....I cant believe my nose!!!!!!!!?????? :hatari:
 
These wahubiri fears to loose their obedient followers who are the major source of their income:embarassed2:
 
hata kama ni adui yako inabidi umpende kama nafsi yako, sasa huyo mwingira ana interest zake,,, kazi 2nazo cc waumini,
 
Wahubiri hawa wamekuwa kama chuma ulete....kila siku wanawatisha watu kuwa siku za mwisho zimekaribia watu waweke hazina kwa bwana, cha ajabu hazina hizo zinawekwa kwao. Mahubiri yao asilimia 80 ni michango, sadaka na fungu la kumi, asilimia 15 ni kutishana kwamba ukimkosea mungu hakika utakufa muda wowote na asilimia tano ndo neno lenyewe la uponyaji....UWIANO UKO WAPI?:embarassed2:
 
Aangalie asije akaomba akafa yeye badala ya babu.Yeye anahubiri utajiri, babu hana tamaa na fedha.
 
Wizi mtupu! Mwingira, Loliondo, Kakobe, Rwaka... Mungu ndo anajua mkweli na wa haki yupi!
 

Umesema vema Judy, lakini kwa kesi hii ilivyo sasa hivi, hatuhitaji sana, kuisema na kuipigania kwa jinsi ya MWILI.
Tukubali tu kwamba Efeso 6:10-18 ifanye kazi wakati huu.
Hasa mstari wa 18: Kwa Sala zote na maombi mkisali kila wakati katika roho mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote.
 
babu ataendelea kutoa huduma kama kawa mwingira and co.endeleeni kuomba lengo letu ni moja tu kuponya wagonjwa.
 
Mwingira Pia aache kutoza michango kanisani si kipaji na uwezo kapewa na Mungu!,

Puuuuuuuuuuuuuuuuuumbaffffffffffffffff!

Alaniwe Mwingira Na kizazi chake, Na roho yake ya Kishetani ya kumwombea babu wa loliondo na loliondo mabaya Ife, tena ife Mara Moja!
 
Mkisali salini hivi "baba yetu uliye mbnguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, MAPENZI YAKO YATIMIZWE HAPA DUNIANI KAMA HUKO MBINGUNI, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu kama sisi nasi tunavyowasamehe waliotukosea, usitutie katika vishawishi,lakini utuokoe na yule muovu, kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu na utukufu, hata milele, AMEN". Ineleke mwingira anayafumbia macho baadhi ya mafundisho ya YESU tena mafundisho yenyewe ni ya msingi sana, sala aliyotufundisha sisi waamini, hapo nilipoandika kwa herufi kubwa, tumuombe MUNGU alitakolo lifanyike duniani kama mbinguni, "alitakalo" Si tulitakalo, akitaka dawa itolewe loliondo sisi tunakwenda kinyume na maombi yetu wenyewe, tunataka labda dawa itolewe na wanaojiita wenye upako, kwa wanavyojipambanua inatushawishi kuwa upako ni mali yao wala si mali ya MUNGU ROHO TAKATIFU, manabii mtawajua kwa matunda ya kazi zao. Watawaombea watu kufa badala ya msamaha, YESU aliomba akisema "baba wasamehe kwa kuwa hawajui walitendalo".
 
mbona wao wanachukua zaka kanisani??????????????

tena imeandikwa usilani usije ukalaniwa!!!!!!!!! hapa inakuaje?
 
Ni mara ya kwanza kusikia mpakwa mafuta,mchunga kondoo wa BWANA anamuombea mchungaji mwenzake KIFO sasa UNABII UNATIMIA natamani niishi nione mwisho wake ni nini,NAAMINI HAYA MAKANISA YANAYOJIITA YA KIROHO SASA YAMEFIKIA MWISHO,KWANI WATENDA KAZI WAO WAMEANZA KUTAPATAPA,Mwanagu kua uyaone,yetu macho na masikio SIYO LAZIMA KUMFUNDISHA MTU MZIMA ZURI NA BAYA,MCH.MWINGIRA FUNGA HUO MDOMO WAKO ULICHOKISEMA J2 SIYO MAFUNDISHO YA IMANI HIZO NI CHUKI BINAFSI UNAOWAELEZA NI WATU WAZIMA WANAOJUA ZURI NA BAYA SIKU AKIGUNDUA KUWA UNACHEZA NA AKILI ZAKE(MTU MZIMA)UTAUMBUKA VIBAYA KAMA HIYO DECI YENU MLIYOANZISHA ambayo leo hii unajitoa kuwa haukuwa mmojawapo au utafunga kanisa kwa kupungukiwa na wachangiaji.
 
siku zote mwizi akiibiwa anaumia sana.....pole mwingira..........

naona umejificha kwenye ngozi ya kondoo weee sasa naona uzalendo unakushinda pole sana.

dawa ya babu itibu au isitibu wewe siyo kazi yako,,na kumbuka wewe ni binadamu tu.

hakuna binadamu yoyote uliyemuumba, sasa iweje leo uombee wenzio wafe?? .

acha hizo mwingira,,utajiri ulionao usikulevye......
 
wanaona babu anawachukulia WATEJA WAO! ikumbukwe cku hz dini ni bsns entity kama zilivyo zingine! yetu macho! ukiamini nenda hutaki kaa kimya!
 
Jamani sipendi kungilia dini lakini hapa nitasema huyu mwingira anakosea kusema kwa sababu ukisoma maandiko kila kitu lazima kiende na sadaka kumtumikia Mungu ni gharama ndo maana alisema kuwa ni rahisi ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko binadamu kuingia ufalme wa Mungu sasa huyu babu kwa kuwa yeye ameweka kiwango cha pesa ndo maana wameamua kumgandamiza hapo ila siku hizi ukienda makanisa yetu haya waumini wanashinikizwa kutoa kiasi kikubwa sana cha fedha ila watu awalalamiki ila kwa babu mia 5 watu wanalalamika. Ina maana ukiamua kufanya kazi ya Mungu lazima pia na wewe uishi kama watu wengine na maana ya kuwa babu angesema dawa ni bure yeye angekula wapi wakati anafanya kazi ya kugawa dawa asubuhi mchana jioni kwamba familia yake ile mawe? wachungaji wenyewe wanasoma na wanaajiriwa na bado wanalipwa mishahara hizo hela zinatoka wapi kama sio sadaka zetu. sasa kwanini huyu mwingira aongee maneno ya ajabu hivi wakati yeye mwenyewe anataka mtu akienda kanisani kwake lazima aende na sadaka na pia huyu babu aliletewa fedha taslim ml 10 lakini akamwambia huyo mtu apeleke kwenye kanisa lake kutoa yeye apokei zaidi ya 500 je mwingira anapokea mangapi kwanini amseme mwenzie.
 
Mimi si mshangai kabisa mwingira na mwingine yeyote yule.. Napenda kumuunga mkono ejogo maana watu wenye shida hata ukiwaambia nn wanafanya bila yakujuwa outcomes zake ni nn,. Mwingira hajafanya research yake vizuri kabla ya kuropoka kanisani kwake. Kwa taarifa kama kuna mtu amefika kule kila jumapili babu huenda kwenye kanisa lake kutoa mahubiri mazuri kama afanyavyo yeye kila jumapili na huongelea habari za yesu kama kawaida.. Fanyeni uchunguzi kwanza .

Kwani hayo mafuriko ya watu yangekuwa pale kibaha kwake kila mtu anataka huduma hiyo bure angepata wapi muda wa kumuhubiri huyu yesu mbona tunaona kwenye trinet tv yake wakati wamikesha ambulence huwa zinakuja kufanya nini????

Mimi natoa ushauri wawe kama proft. Tb-joshua.. Nae ana maji unajuwa kaweka nn??? Mbona hamumsemi mch lwakatare alikuja kuwauzi watu haykufanya kazi..nakumbuka sana msituone tupo kimya tunafuatilia sana haya mambo ya wachungaji

komeni...wachungaji hasa mwingira uliye anzisha mpaka mambo ya zone yote hii nikukusanya sadaka wivu wa nini..
 
Mi naona tu tunahitaji Mungu atusaidie tena sana, maana hawa wachungaji wengi wanatupotosha sana, wako kimaslahi sana kushinda wanachohubiri. Mwungira kuna siku nimemsikia akihubiri kwenye tv anafundisha eti ukimfumania mmeo na mwanamke mwingine usikubali, pigana naye hadi kieleweke, nikawa najiuliza huyu ni mchungaji wa aina gan? waumini wakianza kupigana na waume zao what will follow? Mwingine ni mzee wa upako, baba mkwe wangu alienda kusali huko siku moja na familia yake, wakakosea hawakufunga macho wakati anasali kilichotokea walikuja mabaunsa wakamburuza chini kama mbwa bila kujali uzee wake na bila hata kujua ni nani, hataki hata kusikia habari ya mzee wa upako. Nionacho mimi wanajikweza sana kushinda hata Yesu wanayemhubiri. Mungu na atusaidie, ila hana haki ya kumlaani ambilikile, wanasemaga ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo usiwe wa kwanza kurusha mawe
 
Huyu mwingira ni mwizi...na wafuasi wake ni vipofu wanaotumika kwa bahati mbaya sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…