Mwinyi Mkuu Katundu atekwa na wanaodaiwa kuwa wanausalama, hajulikani alipo. Huu ni mtihani wa kwanza kwa Diwani Athuman

Mwinyi Mkuu Katundu atekwa na wanaodaiwa kuwa wanausalama, hajulikani alipo. Huu ni mtihani wa kwanza kwa Diwani Athuman

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Kwa niaba ya familia ya Mwinyi Mkuu Mohammed Saidi Katundu, kwa masikitiko makubwa kabisa tunatangaza kupotelewa na Baba yetu Mzee Mwinyi Mkuu Mohammed Saidi Katundu katika tukio ambalo lilitokea mkoani Mtwara wilaya ya Tandahimba alfajiri ya tarehe 15 Novemba 2019.

Baba yetu alikuwa nyumbani na familia yake baada ya kurudi kutoka kwenye shughuli zake za kuuza bidhaa zake mtaani almaarufu kama machinga. Ghafla usiku wa saa nane alivamiwa na watu ambao walijitambulisha kama maafisa usalama. Lakini cha kushangaza, waligoma kutoa vitambulisho vyao na kwa kuwa walikuja na silaha za moto ilibidi mzee wetu akubali kuongozana nao. Walimchukua pamoja na kubeba vitambulisho vyake vyote ikiwemo hati yake ya Kusafiria (passport). Hadi usiku wa siku hii ya leo (18 Novemba 2019) ni siku ya nne na hatufahamu mzee wetu yuko wapi.

Tumejitahidi kufanya juhudi za kumtafuta lakini juhudi zetu zote zimegonga mwamba huku Jeshi la polisi likikanusha kumshikilia au kuhusika na kumkamata Mzee wetu. Tunatoa wito kwa Watanzania wote, mwenye kupata taarifa kuhusu mzee wetu, awasiliane na familia haraka iwezekanavyo.

Imetolewa na Mbarouk Khan (simu: ..0672289926, 0658112230, 0716840684

2215601_Img-1574110732079.jpg

Katundu.jpg

Chanzo: Ukurasa wa Facebook wa Zitto Kabwe

My Take:
Tulitegemea baada ya mabadiriko TISS mambo ya utekaji na upoteaji hovyohovyo wa raia yangekomeshwa.
Lakini cha kusikitisha kumbe mambo yanaendelea business as usual!

Kama ni vyombo vya serikali vinahusika basi ukamataji wa raia una taratibu zake za kisheria lakini hii ya kuvamia watu na kuwapoteza haijakaa sawa.

Serikali itoe maelezo, huyu mwananchi yuko wapi na amechukuliwa na nani?

Haya mambo ni lazima tuendelee kukemea, huyu mtu ana familia yake inayomtegemea kama ana kosa basi afikishwe mahakamani siyo kupotezwa!.
 
Amechukuliwa usiku wa manane na watu waliojitambulisha kwamba ni askari ambao walikataa kutoa vitambulisho, sasa kwa nini wanafamilia walisubiri siku nne? Kwanini hawakuanza kufuatilia usiku huo huo? Siku hizi kuna simu za mkononi Je, walianza hizo pilika pilika na kuuliza?

Post ya Zito inaonyesha kwamba TISS wanahusika, Je, anao ushahidi?
 
Siku hizi hawateki watu kihivyo. Wanaongea na wahudumu wa mgahawa {restaurant} unayoenda kula kila siku na wakuwekea sumu katika hicho chakula kila siku mara ghafla unaanza pata mabadiliko ya afya katika mwili wako baada ya hapo unakufa peacefully hii hufanyika kwa watumishi wa umma zaidi. Wakija wanakwambia eti ni oda ya dg

Ikishindikana hiyo, wanaongea na madaktari wako katika hospitali unayotibiwa utachanganyiwa madawa ya kumeza kwa ugonjwa usioumwa. Taratibu wanakuua na kukumaliza, mbinu kutoka kwa wayahudi hizo
 
Amechukuliwa usiku wa manane na watu waliojitambulisha kwamba ni askari ambao walikataa kutoa vitambulisho, sasa kwa nini wanafamilia walisubiri siku nne? Kwanini hawakuanza kufuatilia usiku huo huo? Siku hizi kuna simu za mkononi Je, walianza hizo pilika pilika na kuuliza?

Post ya Zito inaonyesha kwamba TISS wanahusika, Je, anao ushahidi?

..hili suala hata Mzee Mwanakijiji aliwahi kulitahadharisha jeshi la Polisi na vyombo vya ulinzi na usalama.

..kumezuka tabia ya Polisi kuvaa nguo za kiraia, kubeba silaha za kivita, na kutekeleza majukumu ya jeshi la Polisi.

..Utaratibu huo mpya ndiyo unaotoa mwanya wa kufanyika hayo yaliyomtokea mhusika anayedaiwa na Zitto kuwa ametekwa na wanausalama.

..Itafika mahali wananchi watashindwa kutofautisha kati ya Polisi na majambazi.
 
Amechukuliwa usiku wa manane na watu waliojitambulisha kwamba ni askari ambao walikataa kutoa vitambulisho, sasa kwa nini wanafamilia walisubiri siku nne? Kwanini hawakuanza kufuatilia usiku huo huo? Siku hizi kuna simu za mkononi Je, walianza hizo pilika pilika na kuuliza?

Post ya Zito inaonyesha kwamba TISS wanahusika, Je, anao ushahidi?
Tatizo ni kwamba wanateka wanajulikana na bado wanatamba mitaani

Solution ni kudeal na ndugu zao
 
Machinga ana hati ya kusafiria..! I wish ningeishika hiyo hati niangalie mihuri... Then ndio tutajua machinga kweli au lah na ana la kueleza au lah..
Inshu hapo sio kuwa na passport, au huwa ana kwenda wapi, mnacho fail, ni kitu kidogo tu, njia za ukamataji, kwani ukiwatuma polisi wakaenda mchana tu, na kumkamata, na taratibu nyingine zikafuata, kuna tatizo? Kwani serikali zote huko nyuma hakukuwa na watu kama hawa?lakini approach haikuwa hii!! Ilani njia moja ya serikali zile zinazotisha wananchi!! Halafu unasikia viongozi wa dini wanatoa mapambio ya kusifia tu ili mambo yao yanyooke tu!! Bora yeriko nyerere anayeabudu mizimu ya mababu.
 
Wait a minute, yaani machinga ana hati ya kusafiria ?? ( Passport)?? kuna harufu ya jambo hapa.
Still loading.....
Nini maana ya title ya "Mwinyi Mkuu"?
Tukio alfajiri ya tarehe 15 November......baada ya kutoka kwenye shughuli zake za umachinga?......alivamiwa SAA nane Usiku......na watu waliojitambulisha.....??????
Still loading the dots...
 
Back
Top Bottom