Mwinyi Mkuu Katundu atekwa na wanaodaiwa kuwa wanausalama, hajulikani alipo. Huu ni mtihani wa kwanza kwa Diwani Athuman

Mwinyi Mkuu Katundu atekwa na wanaodaiwa kuwa wanausalama, hajulikani alipo. Huu ni mtihani wa kwanza kwa Diwani Athuman

Wilaya ya Tandahimba ni kubwa kijijiji gani? Ili tuweze wasiliana na jamaa zetu huko kuwaulizia mambo yalikuwaje hasa
 
Hivi kwa nini polisi wasijitokeze hadharani na kuukana huu utaratibu wa kuvizia watu usiku wa manane kwenye nguo za kiraia.

Kwa nini isiwe kama zamani polisi wakija kukamata mtu lazima uongozi wa mtaa husika uambatane nao maana hapajitikezi hata majibizano ya risasi kwenye hizi kamatakamata.

Kama polisi hawahusiki basi wanailea hii tabia.

Hata ukioneshwa kitambulisho cha polisi utajuaje kama ni valid? Wangapi mmewahi hata kuviona hivyo vitambulisho before?
Nani alikudanganya kuwa zamani polisi uongozi wa wa mtaa unaambatana nao? Ulisoma wapi? Unaongolea Tanzania au nchi nyingine?
 
Mzee Katundu amepatikana, Amepatikana akiwa mzima wa Afya lakini akiwa na uchovu mwingi, Mazingira ya kuachiwa kwake hayana maelezo ya kuridhisha lakini amekiri kuachiwa na waliomteka.

Asante wana JF kwa kupaza sauti dhidi ya vitendo vya kikatili, kinyume cha sheria, vya uhuni vya kishenzi vya utekaji wa raia.

Sisi sote kwa umoja wetu tuendelee kupiga kelele ili matendo kama haya tuliyokuwa tukiyasikia yakitokea huko kwenye nchi nyingine kwenye tawala dhalimu yakianza kutokea katika nchi yetu.

Kila mmoja akatae Thuggish, unlawful, oppressive na inhumane treatment ya wananchi kinyume cha sheria. Wananchi sharti walindwe dhidi ya matendo ya kihuni ya aina hii

Img-1574283952038.jpg
 
Nashangaa sana wanaouliza mmachinga kuwa na hatinya kusafiria.
Nawapeni tu taarifa huyu ni machinga maarufu wa kuuza marash ya kisunni kkoo huwa ana kibaiskeli chake. Aliwah kuishi arabuni.miaka.ya nyuma sana. Kkoo ana nyumba lkn pia mtwara ndiko inakokaa familia yake.

Btw kapatikana jana usiku akiwa kachoka sana na familia.yale.imesema itaongea leo
 
Mleta uzi pole yake lakini ni mbumbumbu. Mtu akijitambulisha ni askar Tayari ni askari? Kwa nini hamkujitolea wanafamilia watano kuongozana naye mkaone kituo anachopelekwa kisha mrudi nyumbani?
Imetajwa kuwa watekaji walikuwa na silaha za moto. Ungelikuwa wewe ungefwata mkia? Hayo mambo sikia yakitokea kwa wengine usiombe yakukute.
 
Kwa niaba ya familia ya Mwinyi Mkuu Mohammed Saidi Katundu, kwa masikitiko makubwa kabisa tunatangaza kupotelewa na Baba yetu Mzee Mwinyi Mkuu Mohammed Saidi Katundu katika tukio ambalo lilitokea mkoani Mtwara wilaya ya Tandahimba alfajiri ya tarehe 15 Novemba 2019.

Baba yetu alikuwa nyumbani na familia yake baada ya kurudi kutoka kwenye shughuli zake za kuuza bidhaa zake mtaani almaarufu kama machinga. Ghafla usiku wa saa nane alivamiwa na watu ambao walijitambulisha kama maafisa usalama. Lakini cha kushangaza, waligoma kutoa vitambulisho vyao na kwa kuwa walikuja na silaha za moto ilibidi mzee wetu akubali kuongozana nao. Walimchukua pamoja na kubeba vitambulisho vyake vyote ikiwemo hati yake ya Kusafiria (passport). Hadi usiku wa siku hii ya leo (18 Novemba 2019) ni siku ya nne na hatufahamu mzee wetu yuko wapi.

Tumejitahidi kufanya juhudi za kumtafuta lakini juhudi zetu zote zimegonga mwamba huku Jeshi la polisi likikanusha kumshikilia au kuhusika na kumkamata Mzee wetu. Tunatoa wito kwa Watanzania wote, mwenye kupata taarifa kuhusu mzee wetu, awasiliane na familia haraka iwezekanavyo.

Imetolewa na Mbarouk Khan (simu: ..0672289926, 0658112230, 0716840684

Chanzo: Ukurasa wa Facebook wa Zitto Kabwe

My Take:
Tulitegemea baada ya mabadiriko TISS mambo ya utekaji na upoteaji hovyohovyo wa raia yangekomeshwa.
Lakini cha kusikitisha kumbe mambo yanaendelea business as usual!

Kama ni vyombo vya serikali vinahusika basi ukamataji wa raia una taratibu zake za kisheria lakini hii ya kuvamia watu na kuwapoteza haijakaa sawa.

Serikali itoe maelezo, huyu mwananchi yuko wapi na amechukuliwa na nani?

Haya mambo ni lazima tuendelee kukemea, huyu mtu ana familia yake inayomtegemea kama ana kosa basi afikishwe mahakamani siyo kupotezwa!.

Hivi now days mtu akipotea tu anakuwa ametekwa
 
Inshu hapo sio kuwa na passport, au huwa ana kwenda wapi, mnacho fail, ni kitu kidogo tu, njia za ukamataji, kwani ukiwatuma polisi wakaenda mchana tu, na kumkamata, na taratibu nyingine zikafuata, kuna tatizo? Kwani serikali zote huko nyuma hakukuwa na watu kama hawa?lakini approach haikuwa hii!! Ilani njia moja ya serikali zile zinazotisha wananchi!! Halafu unasikia viongozi wa dini wanatoa mapambio ya kusifia tu ili mambo yao yanyooke tu!! Bora yeriko nyerere anayeabudu mizimu ya mababu.
Atakuwa anafadhili ugaidi huyu
 
Mzee huyu ameachwa huru

Kupitia kwenye mjadala huu ni wazi watu wenye kanzu na ndevu wanatazamwa kwa chuki sana

Watu wamekwenda mbali kujenga kila aina ya dhana dhidi yake kwa kuwa mioyo imebugizwa chuki tuuuuu
 
Muogope Mungu, Si vizuri kumdhania mtu dhana mbaya bila ushahidi.
Usihukumu, usije ukahukumiwa, Kama huna ushahidi wa Jambo muachie Mungu ahukumu.
Hujafa hujaumbika!
We unaonaje, watu wamechinjwa Msumbiji na mpakani mwa Mtwara hamkupiga kelele, leo kachukuliwa mmoja tu kelele dunia nzima!! au waliochinjwa ni kuku? mmachinga gani anarudi usiku wa manane, ana hold passport, anaishi good life naona hata kwenye picha anaandaa msosi kwa gas coocker! ha ha ha ha ha haaa inataka moyo kuamini!
 
Tunasubiri atoroke kutoka huko alipo ili aje kufungua malalamiko yake ndipo tuweze kufuatilia.
Roma alishasema yaliyomsibu au Mo????? Tusubiri ipo siku wajukuu wetu wataandika wakati tumeshaoza makaburini. Mungu wao anawaona kama yupo. Huyo Mungu anayekaa kimya wakati watu wanateseka kwanini. Kutoka Misri Manna ilimwagwa jangwani kama ni kweli je sasa iweji dunia inalia au Mungu wamekuwa wengi na wanagawana majukumu?
 
Huyu ni zaidi ya Machinga. Kuna mahali amekosea!!!! Hati ya kusafiria!!!. Ukiangalia na mwonekano wake katika picha basi inatosha. Poleni ndugu zake.
 
Huyu ni zaidi ya Machinga. Kuna mahali amekosea!!!! Hati ya kusafiria!!!. Ukiangalia na mwonekano wake katika picha basi inatosha. Poleni ndugu zake.

Hati ya kusafiria kwani sh ngapi?
Ni sh 150000 tu
Yaani unahukumu uhalifu wa mtu kwa muonekano?,
Ina maana Waislamu wote wenye muonekano wa Ibada wote ni magaidi?
Acheni unyanyapaa kwa binadamu wenzenu, Ni ukatili huo
 
Kwa niaba ya familia ya Mwinyi Mkuu Mohammed Saidi Katundu, kwa masikitiko makubwa kabisa tunatangaza kupotelewa na Baba yetu Mzee Mwinyi Mkuu Mohammed Saidi Katundu katika tukio ambalo lilitokea mkoani Mtwara wilaya ya Tandahimba alfajiri ya tarehe 15 Novemba 2019.

Baba yetu alikuwa nyumbani na familia yake baada ya kurudi kutoka kwenye shughuli zake za kuuza bidhaa zake mtaani almaarufu kama machinga. Ghafla usiku wa saa nane alivamiwa na watu ambao walijitambulisha kama maafisa usalama. Lakini cha kushangaza, waligoma kutoa vitambulisho vyao na kwa kuwa walikuja na silaha za moto ilibidi mzee wetu akubali kuongozana nao. Walimchukua pamoja na kubeba vitambulisho vyake vyote ikiwemo hati yake ya Kusafiria (passport). Hadi usiku wa siku hii ya leo (18 Novemba 2019) ni siku ya nne na hatufahamu mzee wetu yuko wapi.

Tumejitahidi kufanya juhudi za kumtafuta lakini juhudi zetu zote zimegonga mwamba huku Jeshi la polisi likikanusha kumshikilia au kuhusika na kumkamata Mzee wetu. Tunatoa wito kwa Watanzania wote, mwenye kupata taarifa kuhusu mzee wetu, awasiliane na familia haraka iwezekanavyo.

Imetolewa na Mbarouk Khan (simu: ..0672289926, 0658112230, 0716840684

Chanzo: Ukurasa wa Facebook wa Zitto Kabwe

My Take:
Tulitegemea baada ya mabadiriko TISS mambo ya utekaji na upoteaji hovyohovyo wa raia yangekomeshwa.
Lakini cha kusikitisha kumbe mambo yanaendelea business as usual!

Kama ni vyombo vya serikali vinahusika basi ukamataji wa raia una taratibu zake za kisheria lakini hii ya kuvamia watu na kuwapoteza haijakaa sawa.

Serikali itoe maelezo, huyu mwananchi yuko wapi na amechukuliwa na nani?

Haya mambo ni lazima tuendelee kukemea, huyu mtu ana familia yake inayomtegemea kama ana kosa basi afikishwe mahakamani siyo kupotezwa!.

Upande wa pili ukija ku balance story tunaweza kushangaa
 
Upande wa pili ukija ku balance story tunaweza kushangaa

Matokeo ya utekaji yameshamiri nchini, na huu ni muendelezo tu wa utekaji kama alivyotekwa Roma, Mo, Ben. Saanane, Kanguye na Azory Gwanda.
Hakuna cha kubalance story hapo.
 
Matokeo ya utekaji yameshamiri nchini, na huu ni muendelezo tu wa utekaji kama alivyotekwa Roma, Mo, Ben. Saanane, Kanguye na Azory Gwanda.
Hakuna cha kubalance story hapo.

Kuna mwanasheria Arusha rafiki yangu na hakimu wa serikali walitekwa tukahangaika weeeeeee! Baada ya mda wakaonekana kituoni na tuhuma halali kabisa za kusikitisha!

Wakati mwingine vyombo vya I salama (kama basi ni wao) wanafanya kazi kwa utaratibu wao ili wasivuruge uchunguzi!
 
Back
Top Bottom