Mwisho Mwampamba: Vyombo vya habari viliniandika kwa uongo, hakuna pesa yoyote niliyoshinda kwahio sio kweli eti nilifirisika

Mwisho Mwampamba: Vyombo vya habari viliniandika kwa uongo, hakuna pesa yoyote niliyoshinda kwahio sio kweli eti nilifirisika

Lile GHOROFA allilopanga makongo na kuishi na Ray C alipewa bure ? Ile Subaru aliyokuwa nayo alipewa bure ? Kila siku alikuwa anaamka mchana na kucheza pool table na wana pale makongo mwisho na kuwanunulia bia . Je hizo bia alikuwa anapewa bure ?
Jomba acha ubishi. Google upate ukweli kuhusu zawadi za washindi wa big brother mwaka alioshiriki Mwisho. Hakupata hela yoyote huko ila kupitia umaarufu wa BBA alipata dili za hapa na pale.
 
Jomba acha ubishi. Google upate ukweli kuhusu zawadi za washindi wa big brother mwaka alioshiriki Mwisho. Hakupata hela yoyote huko ila kupitia umaarufu wa BBA alipata dili za hapa na pale.
Sina ubishi mimi naongelea ushindi wa kwanza Mwisho alinunua Subaru mbichi akapanga bonge la ghorofa Makongo juu. Ukiingia kwa Mwisho unashangaa kumwona ray c anatembea na bikini wacha weee. Mwisho alikula bata aisee mimi nilishuhudia kwa macho yangu. Alikuwa anaamka mchana anaenda kijiwe cha pool table anawanunulia wana supu na bia za kutosha. Mwisho alifungua baa mikocheni nadhani ulikuwa haujazaliwa enzi hizo. Hata ningekuwa mwisho nisingelalamika maana alimaliza starehe za dunia. Kila akipiga safari ana pakti lake . Mimi siongelei ushindi wa juzi juzi hapa mimi naongelea ushindi uliotutambulisha kumbe kuna big brother.
 
Hahahahah

Ila kiba eti anasema hakuwa yeye
Wapo wengi Sanaa 😊 hata mkoa Kuna jamaa R.I.P akirud bongo alikua na cash Sanaa south Africa.

Akarud bongo akaanza production kwenye mambo ya entertainment tv na redio wilayani..akijulikana Kama MSOUTH..

ilikua ukitaka mgombane upigwe wimbo wa MAC MUGA_WA ALIKIBA MAANA ULIELEZEA MAISHA YAKE HALISI........

Some of lylics,
mchizi wa bongo Mac MUGA yupo simple Sana macmuga
 
Tuligawana Mali za urithi nikapata mgao mzuri wa fedha ,baada ya kuwa nimetoka jela ,baada ya mwaka niliposikiliza huu wimbo nilijihisi Kama nataka kuwehuka hivi .

Mimi Kama mtafiti wa Mambo madogo madogo katika jamii ,nikajiaminisha kuwa huu wimbo utakuwa una maadhi mabaya na yasiyofaa kusikilizwa na waliofirisika kwa kuwa unatonesha madonda yaliyokwisha anza kukauka .

Hivyo kwa heshima yako mkuu ,ningeomba uufute huu wimbo weka tu jina lake ila kuukopi lyrics zake zote tuko wengi utatuliza na kutuumiza
Kweli mkuu ngoja niufute...ni kweli kabisa,
Kuna watu huwa hawapendi kusikia huu wimbo
Huu wimbo una Maumivu Sanaa Sanaa Kuna watu ukipigwa huu wimbo huomba dj au mtu anae deals na music 🎵 🎶 eneo Hilo astopishe au apige text
 
Sina ubishi mimi naongelea ushindi wa kwanza Mwisho alinunua Subaru mbichi akapanga bonge la ghorofa Makongo juu. Ukiingia kwa Mwisho unashangaa kumwona ray c anatembea na bikini wacha weee. Mwisho alikula bata aisee mimi nilishuhudia kwa macho yangu. Alikuwa anaamka mchana anaenda kijiwe cha pool table anawanunulia wana supu na bia za kutosha. Mwisho alifungua baa mikocheni nadhani ulikuwa haujazaliwa enzi hizo. Hata ningekuwa mwisho nisingelalamika maana alimaliza starehe za dunia. Kila akipiga safari ana pakti lake . Mimi siongelei ushindi wa juzi juzi hapa mimi naongelea ushindi uliotutambulisha kumbe kuna big brother.
Alikuwa mtu wa pili na hakupata hela yoyote. Hizo hela unazoziongelea wewe ni vyanzo vingine. Kumbuka pia Mwisho hajatoka familia fukara.
 
Ni kweli, mtu unakuta alikuwa na fantasy zake kwahiyo akipata hela anaona ndiyo muda sahihi wa kuzitimiza

Mademu yeye na kilaji yeye 😅🙌
😁😁
Ni kawaida tu yani ni sawa na mtu atoke kwenye familia maskini halafu akapata zali kiasi milioni hazisumbui. Huwa ni kama wanarukwa na kichaa kwa hizo fantasies
 
Ni kweli mshindi alikuwa binti fulani kutoka Zambia nadhani alitwa Charisey kama nimepatia jina. Na Mwisho alishika nafasi ya pili, ila aliporudi kaburu alikula bata sana, mpaka bia aina ya safari ilipewa jina lake. Mtu anakuja kaunta anakuambia nipe Mwampamba baridi, miaka iyo nilikuwa kaunta sehemu. Zamani misemo ilikuwa mingi kutokana na matukio mfano castle lager walipobadiri chupa mpya ilitwa mwanamke nyonga pia kulikuwa na simu twanga pepeta na TID(mnyama mzee wa zeze) na juzi kati hapa zilitoka safari mwendoka(375mil)
 
Kweli mkuu ngoja niufute...ni kweli kabisa,
Kuna watu huwa hawapendi kusikia huu wimbo
Huu wimbo una Maumivu Sanaa Sanaa Kuna watu ukipigwa huu wimbo huomba dj au mtu anae deals na music 🎵 🎶 eneo Hilo astopishe au apige text
Unaumiza Sana hasa uwe broke na ukizingatia ulikuwa vizuri nyuma .
 
Back
Top Bottom