Elections 2015 Mwita Waitara aitingisha Ukonga wakati akirejesha fomu za kugombea Ubunge CHADEMA

Elections 2015 Mwita Waitara aitingisha Ukonga wakati akirejesha fomu za kugombea Ubunge CHADEMA

Mkuu si ungeenda tu kugombea Tarime au unamuogopa Heche? Ukonga utapata kura za wakurya tu wauza mayai.

Nimekujibu hivi kutokana na majibu yako kwangu.

Jamaa yako leo anazomewa wapi? Nasikia anaanza ziara ya Arusha na Kilimanjaro.
 
Jamaa yako leo anazomewa wapi? Nasikia anaanza ziara ya Arusha na Kilimanjaro.
Mkuu umenichokoza mwenyewe mimi nilikuwa napita tu kwenye huu uzi.

Wewe si ulikwa mpambe wa John Nchimbi leo tena unajifanya mpinzani.

Njaa hizi.
 
Mkuu umenichokoza mwenyewe mimi nilikuwa napita tu kwenye huu uzi.

Wewe si ulikwa mpambe wa John Nchimbi leo tena unajifanya mpinzani.

Njaa hizi.
Naona umeanza kuweweseka kabla hata ajapata ubunge
 
TARIME WANAMKUMBUKA Mwita Waitara ni kiongozi mzuri,TARIME mwaka 2010 kura zake zilichakachuliwa na CCM ambapo Nyambari Nyangwine Alitangazwa mshindi.anafaa kuwa mbunge wa wananchi,hebu mpeni nafasi wana ukonga mtaona uwezo wake.
 
huyu jamaa hastahili ubunge tu ; huyu anatakiwa awemo kwenye baraza lijalo la mawaziri wa UKAWA , unajua kuna watu wameumbwa wawe viongozi tu hata tufanyeje , huyu waitara yuko hivyo.
 
Ahahaha nimemkumbuka alikuwa anampikia Nchimbi chai ofisini.

masahihisho , kilichomtoa waitara ccm ni kuhamishiwa ofisi ya nchimbi ili awe katibu wake , waitara aligoma na hakuwahi kufanya kazi hiyo , usimsingizie .
 
masahihisho , kilichomtoa waitara ccm ni kuhamishiwa ofisi ya nchimbi ili awe katibu wake , waitara aligoma na hakuwahi kufanya kazi hiyo , usimsingizie .
Lakini alikuwa CCM?
 
Tumulikie Mwita.
 

Attachments

  • 1435402976816.jpg
    1435402976816.jpg
    32.1 KB · Views: 346
Ndugu zangu, kama nilivyosema Watanzania tuna tabia ya kusameheana.

Mr Suggestion, labda hukuwa unafuatilia utawala wa daruso wakati huo au ulikuwa ndio kwanza unaingia, waulize wenzio waliokuwa wakongwe kwako watakwambia, mie sizungumzie Magesa ambaye nae aliishia kuwa fisadi tu, nazungumzia Mwita Mwikwabe Waitara, aliyeingia madarakani kwa kusaidiwa na mpiganaji wa wakati huo Tweve.

Naamini waliokuwa UDSM wakati huo japo wanaweza kumsamehe ni mashahidi hapa, utawala wa mwita ulidissappoint sana watu maana watu walijua wameingiza wapiganaji kumbe wameingiza mafisadi na wezi, jamaa walikuwa busy kupiga deal na kula pesa tu, kila kitu kwao ilikuwa biashara.

Msifieni kwenye mengine ila mkitaka kumsifia kuhusu urais UDSM mtaharibu maana wengi wanaufahamu utawala wake pale.

MASONJO SAMAHANI NIKUULIZE, ulisoma kozi gani pale UDSM?
na ulikuwa mwaka wa ngapi wakati Waitara akiwa Rais wa DARUSO?

Je, Unaweza kutueleza wana janvi ni deal gani alizokuwa akipiga akiwa kama Rais enzi hizo?

Kwa ufupi tu nikufahamishe, Mwita Waitara ni kiongozi shupavu asiyepelekeshwa hata kidogo na husimamia vema masrahi ya anaowaongoza.

Mimi kama Rais wangi enzi hizo, aliwahi kutuongoza kuikataa test ya Dr, aliyekuwa analazimisha tuifanye Jumapili badala ya katikati ya wiki, ambapo ndio siku muafaka ya kufanya Test. Kumbuka miongozo ya chuo hairuhusu kufanya test jumamosi wala jumapili.

Test haikufanyika na Dr. yule akakasirika na siku alipoileta katikati ya wiki akawa ameikaza balaa, lakini tukaipiga na akashindwa kutukamata. Manake test ya masaa mawili liliypangwa kufanyika J2 iligeuka kuwa ya Dr 60 ( saa 1) kwenye kipindi.

Sasa kaka, mtu kama huyo asiyepnda kupindishwa kwa sheria huoni kama ndiye anayefaa. Acha kumpakazia Mtu wa watu huyo.

Mwita Nakutakia kila la kheri kaka, na ungekuwa jimboni kwangu familia yangu yote ungechukua kura zao.
 
Mkuu umenichokoza mwenyewe mimi nilikuwa napita tu kwenye huu uzi.

Wewe si ulikwa mpambe wa John Nchimbi leo tena unajifanya mpinzani.

Njaa hizi.

Mkuu mbona hujanijibu? Nimekuuliza vipi kijana wetu anayezomewa kila mahali leo yuko wapi?

Ile video ya Tunduma ni ya kweli?

Kwenye Urais uko kambi gani? Uko ya mtu wa 'dini yetu' ama unamuunga mkono Padre Agustine Ramadhani?
 
mkuu umenichokoza mwenyewe mimi nilikuwa napita tu kwenye huu uzi.

Wewe si ulikwa mpambe wa john nchimbi leo tena unajifanya mpinzani.

Njaa hizi.

kuwa mpambe wa nchimbi sio shida...mabadiliko yanatokea wakati wowote....we unataka wote walioko ccm wasitoke? Acha utoto wa fb
 
Mkuu mbona hujanijibu? Nimekuuliza vipi kijana wetu anayezomewa kila mahali leo yuko wapi?

Ile video ya Tunduma ni ya kweli?

Kwenye Urais uko kambi gani? Uko ya mtu wa 'dini yetu' ama unamuunga mkono Padre Agustine Ramadhani?
Zitto yupo Tanga anafyeka magugu na kusambaza uzalendo.

Mimi sina timu najua rais anatoka CCM aje yoyote hamna tatizo.

Mkuu vipi huko Chadema lini wagombea urais wanaochukua fomu au nyie kuna mgombea urais wa maisha Padre Slaa.

Nasikia Criminal yeye ubunge basi tena.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom