Mwita Waitara: Apigilia msumari umeya Ubungo, asema Boniface Jacob siyo Meya tena

Kosa la Mkurugenzi ni lipi? Yeye anajuaje kwamba barua Ile ni feki au siyo feki? na ilitoka kwenye chama husika. Kwa mujibu wa sheria na utaratibu meya anapofukuzwa anatakiwa akate rufaa kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za mitaa siyo Mkurugenzi. Waziri atapitia na kujiridhisha ukweli wa mambo ulivyo kabla hajatoa maamuzi yake. Kwahiyo, Naibu Waziri yupo sahihi kabisa.

CHADEMA wanapaswa kujitafakari sana, wanaweza kudhani adui yao ni CCM kumbe yupo ndani mwao wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona unakua mjinga kiasi hiki?

Sasa hapo kosa ni la mkurugenzi au kosa la Chadema, Chadema wakate rufaa kwa kipi hasa?

Mpaka mda huu Mkurugenzi ilitakiwa awe amejiudhuru kwa Uzembe na mkurupuko aliofanya

Sent using Jamii Forums mobile app
Uzembe upi alioufanya Mkurugenzi? Yye angejuaje kama Ile barua ni feki? Au Katiba ya Chadema inasemaje? Mahakama pekee ndo inaweza kutafsiri Katiba ya chama chochote na ikijiridhisha utaratibu ulikiukwa ndo inaweza kutengua maamuzi ya Mkurugenzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hio wanaamini kila barua toka popote
Ndio maana yake hiyo... sasa sijui itakuwaje siku mtu akipita ofisini kwao Lumumba na kuchukua headed paper za ccm, mihuri ya ofisi na kuwaandikia wabunge wote wa ccm kwamba wamefutwa uanachama wa ccm, itakuwaje hapo...?

Waitara anasema mambo kama vile mtu asiye na elimu ya chuo kikuu...Mkurugenzi hawezi kukubali kila barua, inafaa ajiridhishe kwanza kama ni fake au sio fake.. je huyo mkurugenzi alifanya due diligence kama hiyo barua ni fake au sio fake...waitara kama msimamizi na mkurugenzi wako mumeonyesha weredi wenu ulipo fikia.. mjitafakari kama mnatosha kwenye vyeo mamlaka yenu hayo...
 
Baada ya kuona jamaa hanunuliki Waziri kaamua kuja kivingine, unategemea ukate rufaa kwa Waziri kama huyu kweli? shame
 
kwa anaejua kwani ex Meya kafanya madudu gani ufipa au kijani hadi asulubiwe? mi sipendi kusikia effects napenda nipate causes and sources!!
 
Hana tofauti na aliye mtuma kwao neno amani tabu sana wao ni uchonganishi kwenda mbele laiti mngejua mliwapa madaraka wakati walishavunja family zao wakati huu unamfuta Meya unataka nini
 
KATI KATI YA MAPAMBANO YA CONVID19 WENGINE TUNAPIGA KELELE TUONDOE TOFAUTI TAIFA LIUNGANE ...TUNAFANYA SIASA ZA KIJINGA ZA KUFUKUZA MAMEYA WALIOKATAA KUUNGA MKONO JUHUDI ....SIO WAKATI WAKE HUU.....INASIKITISHA ......

LAKINI KWAKUA MKURUGENZI KAKIRI ALIKOSEA HII KESI NI TAMU YA KUITIA SERIKALI HASARA KAMA AKIENDA MAHAKAMANI NA AKADAI FIDIA ...ATALIPWA HATA KAMA SIO MWAKA HUU ...
 
Siwezi amini kama waziri, ambaye wakati wowote anaweza kuwa kwenye baraza la nchi , anasimama bungeni kutoa kauli kama hizi.


Hata kama pengine alipiga sanitizer kidogo lakini bunge ni sehemu nyeti sana.

Vitu kama hivi tulikua hatuwezi visikia awamu zilizopita.

Kwanini tusi amini huyu waziri ndio kaandika hii barua ya kugushi sahihi ya mtu mwingine ambalo ni kosa la jinai.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…