Mwitikio wa Serikali na Wengine juu ya Mengi kutaja mafisadi!


Naona 400 milions zinafanya kazi yake,ukiwa na pesa burdani kweli,ukiwa na pesa kama Somaiya,aah,hakuna shida....Watanzania wajue ccm imenunuliwa,na kama na wao wamo ndani ya kapu haya,tufanyeje sasa,maana JK mwenyewe kimyaa!
Yani ni shida kujuwa yuko upande gani,naona shida iko kwenye hao watano waliobaki ambao Mengi hajawataja,ila kutajwa kwa kina Subash Patel ni sawa na kutajwa kwa JK mwenyewe hilo liko wazi,na kwahiyo JK amewekwa kwenye mtego ambao hawezi kujinasua kwani maji moto ni unga tu unahitajika ugali uliwe.
R.E Mengi si mjinga kama wapambe wa mafisadi wanavyofikiri.
Shukran kwa R.E Mengi kwa kujitolea kwa ajili ya Taifa letu na kuazisha chachu kwa watanzania,chachu ya ukombozi,time is running out,na kutokana na pressure iliyopo, explosion lazima itokee ili taifa letu listawi.
 
Jana wazee wa Yanga walitoa kauli kuhusu mfadhili wao kutobughudhiwa hata kidogo. Juzi mapato ya mechi ya Yanga Vs Simba yalikuwa kidogo sana mpaka wadau wote ikiwemo Serikali imestushwa na udogo wa mapato ukilinganisha na idadi ya watuwaliongia uwanjani. Kwakuwa Yanga ni taasisi ya michezo na imekuwa ikitegemea viingilio vya mlangni kuendesha timu yao tokea ianzishwe hadi juzi juzi tu ndipo timu hiyo imekuwa ni taasisi ya mtu binafsi.

Ni kwanin wazee hawa hawajatoa tamko kuhusu uchache wa mapato ya mechi timu yao inazocheza? Je kwa kushindwa kutolea tamko masuala ya michezo ambyo ndio core function ya taasisi yao na badala take wakakamua kujiingiza katika mjadakla ya ufisadi ambapo mtuhumiwa sio siri anatumia fedha nyingi kwa timu hiyo. Je wazee hawa hawajageuzwa sehemu ya ufisadi hapa nchini?

Kwa kuwa kuna wakati wazee hawa hawa walikuwa wakingaa kwenye vyombo vya habari wakimsifia Mengi kwa ufadhili wake japo mdogo, na sasa wanafadhiliwa na mtuhumiwa wetu wa ufisadi, hawafanani na mke anayechangua mume kutokana na uwezo wke kifedha (natanguliza samahani kwa kutumia mfano ambao is a bit gender sensitive)
 

Mpoki,

Nakuelewa na asante sana kwa Pole. Ila hizi habari na picha huwa nikianza kuzisikia na kuona huwa namkumbuka marehemu baba. Mzee aliishia darasa la nne ila alikuwa na akili sana kuzidi hao vijana wa CCM na tena ukichanganya wotee!!
Siku moja alituchukua hadi sehemu ambapo ilikuwa imebaki sakafu na wanakijiji wanatumia kukaushia unga. Akatuuliza mlishawahi kufika, mnajua hapa palikuwa nini? Tukasema hatujui. Akasema hapa Wakatoliki walikuwa wameanza kujenga mission yao na haya ni mabaki ya majengo yao. Hili lilikuwa eneo zuri sana na walilipenda. Ila tatizo moja likazuka, mnaona lil jengo? (Umbali kama wa nusu km), tukasema ndiyo (ulikuwa msikiti), ilizuka vita moja kubwa sana. Moja ya watu wapinzani wa jamaa kujenga pale alikuwa Sheik mkuu wa kijiji (wa wakati ule). Wazungu mwisho wakachoka na wakaondoka. Mzee alisema kuwa kama pale pangejengwa basi kijiji chetu leo hii tungelikuwa na ndugu na jamaa wengi ndani na nje ya nchi na huku wengine wakiwa na vyeo vikubwa sana. Hadi leo nikikumbuka huwa siamini kuwa ni maneno yanayotoka kwa mzee aliyeishia darasa la 4.
Sipo hapa kukashifu dini ya Kiislam na sababu kubwa ni kuwa nusu ya familia yangu, marafiki na jamaa ni waislam. Ila ukweli ni kuwa Wanyamwezi tunapenda sana kuwa na wake wengi na dini ya Kikristo ilikuwa inazuia. Hivyo wengi walikuwa wanaingia kwenye Uislam kama fasion maana inabidi uwe na dini na kigezo kikubwa unaweza kuwa na wanawake hadi wanne ingawa ukiangalia ni kuwa wengi walikuwa hawawapendi wote sawasawa kama dini inavyotaka. Pia ukiwa na wake wengi unakuwa na watoto wengi na hivyo unakuwa na Manpower almost ya bure (utumwa wa aina fulani) huku wewe baba ukiwa unatanua tu au kujifanya umekuwa mmfanya biashara na wanao/wake zako ndiyo wana produce.

Nafahamu kuwa hata mikoa mingine kuna umasikini. Ulaya/USA pia wako. Ila tatizo la Tabora kubwa kabisa ni umasikini wa mawazo. Unakuta mtu ana akili zake timamu, ardhi ya kutupa Sikonge, ana afya tele lakini analalamika kuwa hana pesa na summer nzima amekaa tu anasubiri msimu wa mvua ndiyo aanze kazi. Hajishughulishi kwenye kilimo cha nyanya, miwa, vitunguu, kabegi, michicha nk au kwenda kwenye ufugaji wa samaki, nyuki nk. Amekaa tuu!!! Akikuona anasema umpe visenti kidogo maana kakwama. Jioni ikifika, wao ni kwenye ulevi wa tende.....🙂 Ehhh bwana wee, Tabora kuna Bangi, gongo na Wanzuki kwa wingi sana.

Natoa ombi kwa mtu yeyote atakesoma hapa na siku moja awe Rais au PM. Ili sisi Wanyamwezi tuendelee, basi ni viboko lazima vitembee. Ndiyo kitu pekee ndugu zangu huamka. Vinginevyo basi labda kama alivyoandika Masanilo kuwa "Unafyeka kizazi kizima na kuanza upya...." Uzuri mmoja wa hawa Wanyamwezi ni woga sana. Ukiwatetemesha kidogo, watafanya kila kitu unachotaka. Viboko kwanza na shule ndiyo ifuate baadaye. Hawa wataendelea kuwachagua Vibaka hata kama vibaka watakuja na kubeba watoto wao. So longer wakati wa uchaguzi wamepewa vi-Tshirt.

Mafisadi wa Tabora wanalisikiliza sana huu wimbo na huwa wanautumia. Mwanzo ulikuwa utumike kuwashambulia wakoloni, ila sasa wanautumia wao kutunyanyasa sisi, huku wakizuia watu wengine wasiusikilize (mfano ni maneno ya Mwanakijiji uliyosema). Hebu angalia chini kuanzia dakika ya ya Kwanza (1:00). Yes, we don't want no Rostam philoso

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=KyLLlgdY2aQ"]YouTube - bob marley-one drop[/ame]

They made their world so hard (so hard):
Every day we got to keep on fighting (fighting);
They made their world so hard (so hard):
Every day the people are dyin (dying), yeah!

And then you give us the teachings of his majesty,
For we no want no devil philosophy; (Rostam Aziz, Manji, Lowasa etc)
A you fe give us the teachings of his majesty,
A we no want no devil philosophy

NB: Mtoto mmoja wa Sheick mkuu wa kijiji nilimkuta akiwa ofisa wa elimu wa Mkoa. Nilishangaa sana na nafikiri aligundua. Akasema kisa cha yeye kusoma ni kuwa alisaidiwa na Mwalimu Kauga (Wale wazee Old School na walimu kwelikweli). Mwalimu Kauga alipoona jina la kijana akajua huyu hataletwa shuleni. Akaandika barua ya tishia nyau, na akawaomba Polisi waigonge muhuli. Jioni kijiji kizima kilipata habari kuwa Sheick kapata barua ya Polisi. Basi Sheick hakuwa hata na akili ya kufukiria zaidi ila kumpeleka kijana middle school (Mbirani, Sikonge) ambako alienda hadi akamaliza form 6 miaka hiyooooo huko Tanga. And his father was proud of him. Nilifika kwake na kukuta misahafu ya dini na mezani gazeti la New Africa na nikashinda siku nzima nasoma mpango wa Wanigeria kumteka nyara Diko na mpango ukakwama Hethrow Airport.
Kweli, kile kizazi kilikuwa kingine. Sasa hivi ni Watoto ambao baba zao walikuwa ugali wa Yanga na ma-bulga sijui??
 
Last edited:
Hawa wamesahau kwamba bila Mengi kuonyesha picha za mauaji ya Rwanda mwaka 1995 waingeshinda NCCR Mageuzi. Watumikia tumbo hawa. Ni uzalendo gani wanaouzungumzia ni ule wa kusimamia na kuendesha rushwa katuika chaguzi mbali mbali hapa nchini?

wakawadanganye wakulima wa Tumbaku waliozoea kuwaibia makato yao!!!!!!!!!!!!
 
Then mntakiwa kuwa gavana aitwaye Mnali, aliyewachapa viboko waalimu. This time vibokois demand driven.Whoops!!!!
 
Hatushangai sana maana ni juzi tu wamefadhiliwa na mmoja wa mafisadi, ukila nyama ya mtu utaendelea tu!
 
Pongezi bwana sikonge kwa kuonyesha ukweli kwamba jhata viboko ni demand driven ili Tabora iweze kuendelea. Kosa la Jk ilikuwa ni kumitimua kwa pupa pengine angemleta huko Tabora ilia wachalaze vibioko haswa hao vibaraka kutoka UvCCM
 
Nanyi msituletee za kuleta hapa Mengi amemtukana nani. Ameleza kile anachofahamu ambacho kinawakera wananchi wengi. Nyie mmekosa la kufanya basi nendeni kazibueni mifereji na vyoo mpate shughuli sio kukurupuka na kujidai sisi tunalaani kitendo bla bla pelekeni kule upuuzi wenu.
 
Ni njaa tu wao wanaona vijisenti wanavyopewa na fisadi Manji vina umuhimu mkubwa kuliko maslahi ya nchi yetu ambayo yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na ufisadi wa Manji.
 
Sikujua kwamba mtu aweza fisadi hadi bongo za watu!

Kumbe wale wazee wetu walio kuwa wanapewa shanga na wakoloni na kuuza nchi walikuwa sawa tu, Kwani sioni tofauti yao na hawa wa karne ya 21.
 
2009-04-30 14:37:56
Na Restuta James


Askofu wa Kanisa la Pentecostal Evangelistic lenye Makao Makuu mkoani Mbeya, Zebadiah Mwakatage, amemshambulia Waziri wa Nchi, Ofsi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, kuwa kauli yake ya kutetea mafisadi ni udhalilishaji serikali.

Alisema hali hiyo itafanya Watanzania kuamini kuwa waziri huyo na seikali yake wameajiriwa kuwa mawakili wa mafisadi.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Askofu Mwakatage, alisema anashangaza na kukatisha tamaa kwa tamko la serikali kupitia Waziri Simba, kutetea mafisadi na huku akijua umaskini unaokabiliwa Watanzania umetokana na kuchotwa kwa mabilioni ya fedha.

Alisema hata baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaosema Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, anajipendekeza kwa Rais Jakaya Kikwete ni heri kuliko kujipendekeza kwa mafisadi kama alivyofanya Simba.

``Hivi Waziri Simba ameajiriwa uwakili na mafisadi kuyatetea, maana wao wana fedha tena wana midomo yao ambayo wao ndio wangelalamika, kwanini aibuke na kuwatetea eti ni wafanyabishara safi, hapa kuna mashaka,`` inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Alisema kutokana na maandiko matakatifu, Mengi asione ajabu kuchukiwa na mafisadi na baadhi ya viongozi wa serikali bila shaka wana maslahi wanayopata kutoka kwa mafisadi.

Askofu Mwakatage alisema kwa kuzingatia kuwa msema kweli ni mpenzi wa Mungu, Watanzania wataendelea kuwaombea waadilifu, wanaouchukia ufisadi kama Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroud Slaa, Dk Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Same, Anne Kilango, Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka.

``Nchi yetu tajiri kwa kila kitu, imebatizwa jila la dharau na aibu la umaskini, Mungu tuokoe. Wachonganishe ndimi zao mafisadi na waongo wote wasielewane,`` alisema Askofu Mwakaatage.

Juzi, Simba alijitokeza hadharani na kutetea wanaotuhumiwa kuwa mafisadi mapapa watano waliotajwa na Mengi na kwamba, kitendo cha kuwataja ni sawa na lugha ya kijiweni.

Simba alisema mapapa hao waliotajwa na Mengi ni watu safi na waadilifu kwa sababu, hawajahukumiwa na mahakama.

Alisema Mengi ameingilia kazi za serikali na kumtaka aiache ifanye kazi.
  • SOURCE: Nipashe
Hapo patamu. Sasa vita dhidi ya ufisadi inapamba moto walio upande wa ufisadi tutawajuwa na wa upande wa wananchi tutawajuwa
 
Alicho fanya mtumishi si kumshambulia bali kamweleza ukweli tupu. Alipo nifurahisha ni ombi lake kwa maulana awachanganye mafisadi waparulane!

Mungu hujibu maombi ya watu, na iwe hivo mtumishi.
 
- Nimewauliza wakulu huko ndani ya CCM, kwamba hii kauli ya UV-CCM maana yake ni nini kisiasa, the dataz ni kwamba:-

Kuna kijana anayeitwa Bashe, ndiye aliyeko nyuma ya hili tamko kwa 100%, nia na madhumuni yake ni kupata support ya Rostam ili amuondoe ubunge Seleli nothing more au less!

- Kila kiongozi anatafuta opportunity, hakuna anayejali wananchi wala taifa, huzuni sana kwa taifa hili!

Mungu Aibariki Tanzania!

FMES
 
Kuna kijana anayeitwa Bashe, ndiye aliyeko nyuma ya hili tamko kwa 100%, nia na madhumuni yake ni kupata support ya Rostam ili amuondoe ubunge Seleli nothing more au less!

Kamanda ndo vijana wenu hao mnawaandaa kuchukua uongozi wa juu wa chama na serikali...wamekaa kama mafisi kuvizia mizoga bila hata kufikiri.....wanatumika kwa njaa zao wala maslahi ya taifa hayapo! Rostam ni balaaa
 
- Finally Chadema! Kumbe wapo? Saaafi sana maana Mengi anahitaji msaada na bado sio too late, ingawa wamechele lakini wakati ni muafaka bado sasa tuweasikie kila wakati!

FMES!
 
Duh, kwenye msafara wa mamba hata makenge yamo. Haya ndi makenge yenyewe toka Tabora. Makenge ya namna hii yanastahili kuchapwa bakora.
 

Mungu hawezi kusaidia watu wa.ji.nga kiasi hiki. HAWEZI. Actions now, no more and the END should justify the MEANS we will use.
 

Much respect man. Ingawa mimi ni shabiki wa Yanga siwezi kumfagilia mtu aliyefisadi pesa zetu za Mashirika ya Hifadhi. Kila mwezi tunaktwa kwenye salary halafu yeye na wezi wenzake wanaziiba Kiulaini. Hao wazee wetu wa Klabu ni njaa tu inawasumbua, na uelewa wao pia ni mdogo masikini. waliwahi kumnyenyekea Mengi wakati wa mgogoro wao hapo nyuma.
 
miaka ya nyuma mengi alikwenda yanga na mawazo ya kujitegemea akawaambia yanga iwe kampuni kama vile MANUTD, arsenal, liverpool na nyinginezo. yanga wakamfukuza wakamwambia hawataki iwe kampuni, leo hii yanga ni omba omba kwa manji.

mengi alikuwa na mawazo ya timu kuwa kampuni miaka 20 iliyopita kabla ya watu binafsi kuanza kumiliki timu...
je yanga ingekuwa kampuni miaka ile leo ingekuwa wapi???
je hii tabia ya wana yanga kuwa omba omba na kukataa kujitegemea ina tufundisha nini sisi wa TZ wote?
je hii ni tabia ya wana siasa wetu kuomba omba?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…