Myanmar: Kiongozi wa Kiraia aongezewa miaka mingine 4 jela

Myanmar: Kiongozi wa Kiraia aongezewa miaka mingine 4 jela

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
1641891345589.png

Mahakama nchini Myanmar imemhukumu jela aliyekuwa kiongozi wa kiraia Aung San Suu Kyi miaka mingine minne, kwa kosa la kumiliki na kuingiza vifaa vya mawasiliano- walkie-talkies kinyume cha sheria lakini pia kuvunja masharti ya kupambana na Covid-19.

Hukumu hii ya pili inakuja, baada ya Suu Kyi kupewa hukumu nyingine mwezi Desemba mwaka uliopita, iliyopunguzwa hadi miaka miwili na sasa hukumu zote mbili, ni miaka sita jela, huku kukiwa na wasiwasi kuwa huenda hatimaye akafungwa akapewa kifungo cha maisha jela.

Hukumu dhidi ya kiongozi huyo wa zamani wa Myanmar, kumeendelea kushutumiwa na mataifa ya Magharibi kwa kile wanachosema yamechochewa kisiasa.

Mwezi Februari mwaka uliopita, Aung San Suu Kyi baada ya chama chake cha National League for Democracy kushinda uchaguzi wa wabunge, alikamatwa na wanajeshi na kuzuiwa nyumbani, kabla ya kufunguliwa mashtaka mbalimbali.
 
Hawa wanajeshi wa Myanmar walishamfunga huyu Bibi jela miaka mingi sana hatimaye walimuachia huru wakamruhusu kushiriki siasa na akaja kuwa kiongozi.

Sasa wamempindua na wamemrudisha tena jela...huenda huyu Bibi anachopitia ni 'karma' kwa kufumbia macho unyama waliotendewa 'warohingya' huku akiwa kiongozi.
 
Mkuu jaribu kufuatilia historia ya huyu mama, hayuko hivyo unavyofikiri amejitahidi sana kupambania haki na maisha ya raia hasa wa myanimar ndio chanzo cha yote anayopitia.
Ni kweli mwanzo pale alijenga picha ya kuwa ni mpigania haki hadi akapewa nishani ya Nobel ya Amani...lakini alipopata uongozi na kuunda serikali ndio kipindi kilishuhudia mauaji makubwa ya watu wa Rohingya na wala serikali yake haikusikika kuzuia hadi kukazuka hoja kuwa anyang'anywe ile Nobel prize aliyopita...sina huruma nae kabisa kwa sasa we always leap what we sow
 
Unaongea nn mkuu, huyu ni gaidi kama magaidi wemgine, mbona kauwa raia sana hausemi
Fuatilia , usitegeme bbc na cnn kukuonesha viongiz bora ,hata Mandela walimwita Gaidi ila baadae alivyowasamehe wazungu wakamfanya shujaa , hizo media zinajali maslai ya wazungu tu , wapo tyr kumwita baba yako Shoga ili tu kumfanya asiendelee kupambana na maslai yao
 
Ni kweli mwanzo pale alijenga picha ya kuwa ni mpigania haki hadi akapewa nishani ya Nobel ya Amani...lakini alipopata uongozi na kuunda serikali ndio kipindi kilishuhudia mauaji makubwa ya watu wa Rohingya na wala serikali yake haikusikika kuzuia hadi kukazuka hoja kuwa anyang'anywe ile Nobel prize aliyopita...sina huruma nae kabisa kwa sasa we always leap what we sow
Bro hiyo ni michezo ya wazungu , huwa hawataki nchi dunia ya tatu zipate viongoz bora refer Libya ya Ghafaf , Syria ya Assad , Iraq ya Sadam , Ethiopia ya Abey ( ilipokaribia kuondoa tofauti zao wakatega mtego wa uchaguz ) , zote hizo zilikuwa zinaanza kupiga hatua wazungu wakayaingiza mataifa hayo kwenye mtego wa vita vya ndani ambapo Ni Either ushindwe au Ushinde ukafunguliwe mashtaka ya haki za binadamu coz unapigana na watu hawana gwanda so ukosi kuua raia wema
 
Mkuu jaribu kufuatilia historia ya huyu mama, hayuko hivyo unavyofikiri amejitahidi sana kupambania haki na maisha ya raia hasa wa myanimar ndio chanzo cha yote anayopitia.
Sio kweli mkuu hayu mama kaua sana huko sema labsa kwa vile wakiouliwa wengi ni waislamu na nyie hamuwapendi ndio mukampamba
Tumeshuhudia hata hapa wa kwanza aliharibu wa pili akatengeneza
Lakini akaambiwa eti ndio mbaya
 
Muuaji mkubwa huyu hadi leo pale rohingya wanapata tabu kisa ni huyu mama huyu ni wa kuchinja kabisa
Kill kabisa faster tu
 
Bro hiyo ni michezo ya wazungu , huwa hawataki nchi dunia ya tatu zipate viongoz bora refer Libya ya Ghafaf , Syria ya Assad , Iraq ya Sadam , Ethiopia ya Abey ( ilipokaribia kuondoa tofauti zao wakatega mtego wa uchaguz ) , zote hizo zilikuwa zinaanza kupiga hatua wazungu wakayaingiza mataifa hayo kwenye mtego wa vita vya ndani ambapo Ni Either ushindwe au Ushinde ukafunguliwe mashtaka ya haki za binadamu coz unapigana na watu hawana uhgwanda so ukosi kuua raia wema
Acha kusingizia kila kitu wazungu. Hao hao wazungu ndiyo walimpa hadi tunzo ya nobel, kila kitu kiko wazi wakati Warohingya wanauawa dunia nzima ilishuhudia. Watu wamekimbia makazi, watoto wameuawa, watu wamegeuka wakimbizi kisa tu tofauti za kidini.
She is not who she pretended to be.
 
Back
Top Bottom