Mzani wa ubaya ndani ya CHADEMA umeelemea upande wa Lissu!

Mzani wa ubaya ndani ya CHADEMA umeelemea upande wa Lissu!

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kinachoitwa pesa za Abdul na Lissu ni pesa zake za matibabu anazoidai Serikali, Abdul alikuwa anatumika kujaribu kusaidia kufanikisha zitoke. Hata hivyo ni jambo la kusikitisha katika nchi yetu mambo yanabidi kupelekwa hivi wakati mwingine ili mtu apate haki yake tu, ila huo ndio uhalisia.

Lissu alishapoteza imani na Mbowe muda mrefu akawa anajaribu kutengeneza mtandao wake dhidi ya Mbowe lakini haukufanikiwa sana, alijaribu kusingizia amehongwa magari na serikali.

Lissu akiwa makamu mwenyekiti alianza kubagua viongozi wa chama chake na kukigawa chama, alimpigia kampeni Msigwa dhidi ya Sugu na akajaribu bila mafanikio kutaka kumpigia kampeni Wenje dhidi ya wagombea wengine.

Lissu hajawahi kutoa kauli yoyote hasi dhidi ya Msigwa au kumtetea Mbowe kwa lolote pamoja na kashfa zote ambazo Msigwa amekuwa akimtolea Mbowe, hii sio kawaida.

Lissu alikuwa amepewa kwenye majukumu yake ya makamu mwenyekiti lakini pia amekuwa akijifanyia mambo ya ki chama kama mtu binafsi, yeye anavyoona inafaa tu bila kuzingatia mawazo ya wengine, maazimio, umoja na misimamo ya chama.
 
Wenje unahangaika sana leo utaandika sana,kwa hiyo wewe na rafiki yako mlienda Tegeta kwa Lissu kumbembeleza akachukue fedha zake za matibabu? Yaani Abdul awe na huruma na Lissu kiasi cha kuacha shughuli zake na kwenda Tegeta kuchukua nyaraka halafu asimamie malipo ya Lisu bila kutegemea malipo yoyote kutoka kwa TAL?
 
Ivi angepewa hiyo hela mambo yangeleta kashifa kubwa yaani kapewa hela au zimetoka kwa sababu ya Abdu hii ingeleta kashifa kubwa sasa wenje hajui mambo, haya huleta kashifa ,nahuyo kijana alibeba huruma kweli ? Ni muongo mwenye agenda yake
 
Wenje unahangaika sanana leo utaandika sana,kwa hiyo wewe na rafiki yako mlienda Tegeta kwa Lussu kumbembeleza akachukue fedha zake za matibabu? Yaani Abdul awe na huruma na Lisu kiasi cha kuacha shughuli zake na kwenda Tegeta kuchukua nyaraka halafu asimamie malipo ya Lisu bila kutegemea malipo yoyote kutoka kwa TAL?
Mtu anadai malipo yake ya kisheria, wengine wanajitokeza badala ya kutaka hiyo sheria ifuatwe wao wanataka kupitia mlango wa nyuma kitu ambacho wengine hawataki. Uelewa wa mambo ni mgumu sana. Mtu hawezi kulazimishwa kusaidiwa, sijajua ni kwa nini hadi sasa hayo madai ya Lissu ni danadana hadi sasa ingawaje kila siku tunaambiwa tii sheria bila shuruti. Mpeni Lissu haki yake bila kupitia mlango wa nyuma kwa akina Abdul na Wenje .

Kelele zimekuwa nyingi na serikali mmekaa kimya sana. Si haki kwa kweli. Mpeni malipo yake kama kweli yapo au kama hayapo, toeni ufafanuzi, vinginevyo munamuonea tu. Mtu kachungulia kuzimu bado tu munamsumbua, muoneeni huruma ya kibinadamu basi... hata hilo nalo ni taabu? Anachotaka ni haki yake tu bila kupitia mlango wa nyuma.
 
Kinachoitwa pesa za Abdul na Lissu ni pesa zake za matibabu anazoidai Serikali, Abdul alikuwa anatumika kujaribu kusaidia kufanikisha zitoke.

Lissu alishapoteza imani na Mbowe muda mrefu akawa anajaribu kutengeneza mtandao wake dhidi ya Mbowe lakini haukufanikiwa sana, alijaribu kusingizia amehongwa magari na serikali.

Lissu akiwa makamu mwenyekiti alianza kubagua viongozi wa chama chake na kukigawa chama, alimpigia kampeni Msigwa dhidi ya Sugu na akajaribu bila mafanikio kutaka kumpigia kampeni Wenje dhidi ya wagombea wengine.

Lissu hajawahi kutoa kauli yoyote hasi dhidi ya Msigwa au kumtetea Mbowe kwa lolote pamoja na kashfa zote ambazo Msigwa amekuwa akimtolea Mbowe, hii sio kawaida.

Lissu alikuwa amepewa kwenye majukumu yake ya makamu mwenyekiti lakini pia amekuwa akijifanyia mambo ya ki chama kama mtu binafsi, yeye anavyoona inafaa tu bila kuzingatia mawazo ya wengine, maazimio, umoja na misimamo ya chama.
huenda ni kwasabb ya mdomo, papara, makelele na kubebwa na mabwenyenye ya magharibi 🐒
 
Wanapambana Mbowe asikubali uamuI wa familia agombee afe nao kisiasa. Mbowe asipogombea ataendelea kuwa na heshima ndani ya chama lakini akina Wenje watapotea tu.
 
Abdul yeye serikalini ni Nani Mpaka atumiwe na kina Wenje kumpatia Lisu HAKI ya pesa zake za matibabu?

Je huo ndio utaratibu wa Sheria unavyotaka kuwa mtu Akiwa na madai Fulani amtafute mtoto au ndugu wa kiongozi Fulani ili apate haki yake?

Yoda nawe unaingia kundi la watu wasiofuata Sheria.
 
Abdul yeye serikalini ni Nani Mpaka atumiwe na kina Wenje kumpatia Lisu HAKI ya pesa zake za matibabu?

Je huo ndio utaratibu wa Sheria unavyotaka kuwa mtu Akiwa na madai Fulani amtafute mtoto au ndugu wa kiongozi Fulani ili apate haki yake?

Yoda nawe unaingia kundi la watu wasiofuata Sheria.
Kuna vile nchi inatakiwa kuwa halafu kuna vile nchi ilivyo, kwa sasa nchi yetu ilivyo ni kwamba kama unamjua mtu mkubwa au unamjua mtu anayemjua mtu mkubwa ni rahisi zaidi kuipata haki yako pale inapotokea unazungushwa na kupigwa dana dana.
Lissu alipokutana na Samia Ubelgiji na akamueleza madai yake binafsi haukuwa utaratibu wa kisheria lakini alifanya hivyo kwa kuangalia uhalisia wa nchi hii kwamba Rais anaweza kuamua chochote na ikawa.
 
Kinachoitwa pesa za Abdul na Lissu ni pesa zake za matibabu anazoidai Serikali, Abdul alikuwa anatumika kujaribu kusaidia kufanikisha zitoke.

Lissu alishapoteza imani na Mbowe muda mrefu akawa anajaribu kutengeneza mtandao wake dhidi ya Mbowe lakini haukufanikiwa sana, alijaribu kusingizia amehongwa magari na serikali.

Lissu akiwa makamu mwenyekiti alianza kubagua viongozi wa chama chake na kukigawa chama, alimpigia kampeni Msigwa dhidi ya Sugu na akajaribu bila mafanikio kutaka kumpigia kampeni Wenje dhidi ya wagombea wengine.

Lissu hajawahi kutoa kauli yoyote hasi dhidi ya Msigwa au kumtetea Mbowe kwa lolote pamoja na kashfa zote ambazo Msigwa amekuwa akimtolea Mbowe, hii sio kawaida.

Lissu alikuwa amepewa kwenye majukumu yake ya makamu mwenyekiti lakini pia amekuwa akijifanyia mambo ya ki chama kama mtu binafsi, yeye anavyoona inafaa tu bila kuzingatia mawazo ya wengine, maazimio, umoja na misimamo ya chama.
Miaka 20 imetosha ni mingi sana
 
Kinachoitwa pesa za Abdul na Lissu ni pesa zake za matibabu anazoidai Serikali, Abdul alikuwa anatumika kujaribu kusaidia kufanikisha zitoke.

Lissu alishapoteza imani na Mbowe muda mrefu akawa anajaribu kutengeneza mtandao wake dhidi ya Mbowe lakini haukufanikiwa sana, alijaribu kusingizia amehongwa magari na serikali.

Lissu akiwa makamu mwenyekiti alianza kubagua viongozi wa chama chake na kukigawa chama, alimpigia kampeni Msigwa dhidi ya Sugu na akajaribu bila mafanikio kutaka kumpigia kampeni Wenje dhidi ya wagombea wengine.

Lissu hajawahi kutoa kauli yoyote hasi dhidi ya Msigwa au kumtetea Mbowe kwa lolote pamoja na kashfa zote ambazo Msigwa amekuwa akimtolea Mbowe, hii sio kawaida.

Lissu alikuwa amepewa kwenye majukumu yake ya makamu mwenyekiti lakini pia amekuwa akijifanyia mambo ya ki chama kama mtu binafsi, yeye anavyoona inafaa tu bila kuzingatia mawazo ya wengine, maazimio, umoja na misimamo ya chama.
Blame game means no business any more.
 
Kuna vile nchi inatakiwa kuwa halafu kuna vile nchi ilivyo, kwa sasa nchi yetu ilivyo ni kwamba kama unamjua mtu mkubwa au unamjua mtu anayemjua mtu mkubwa ni rahisi zaidi kuipata haki yako pale inapotokea unazungushwa na kupigwa dana dana.
Lissu alipokutana na Samia Ubelgiji na akamueleza madai yake binafsi haukuwa utaratibu wa kisheria lakini alifanya hivyo kwa kuangalia uhalisia wa nchi hii kwamba Rais anaweza kuamua chochote na ikawa.

Samia ni Rais wa nchi Mzee.
Kumueleza shida yako ni sehemu ya utaratibu wa kawaida na upo kisheria.

Rais lazima asikilize wananchi wake na kuwasaidia, Lisu anamuita Samia Rais. Ni kiongozi wake.

Ni Sawa na Mimi niende kwa Mkuu WA Mkoa kuomba msaada Fulani. Au nitafute mawasiliano ya Rais ili Kupata msaada Fulani.

Lakini kumtafuta mtoto wa Mkuu WA Mkoa au mtoto wa Rais huo sio utaratibu.

Yoda Leo umejionyesha jinsi ulivyo.
 
Yoda kwenye hili sakata la uchafu uliofanywa na Wenje & Abdul unapuyanga kinoma.
Mkuu mimi ni mtu mwenye fikra huru, nimemsikiliza Wenje amenishawishi kwamba hakuna pesa za Abdul zilizokuwa mahali ambazo Abdul alikuwa anachota kuwagiwa wakina Wenje, Lissu na wengine ndani ya CHADEMA kama hongo.
 
Wenje unahangaika sanana leo utaandika sana,kwa hiyo wewe na rafiki yako mlienda Tegeta kwa Lussu kumbembeleza akachukue fedha zake za matibabu? Yaani Abdul awe na huruma na Lisu kiasi cha kuacha shughuli zake na kwenda Tegeta kuchukua nyaraka halafu asimamie malipo ya Lisu bila kutegemea malipo yoyote kutoka kwa TAL?
Kwanza abduli ni nani kwenye hii serikali mpaka awe na maamlaka ya kumtafutia pesa za matibabu TL.?
 
Mkuu mimi ni mtu mwenye fikra huru, nimemsikiliza Wenje amenishawishi kwamba hakuna pesa za Abdul zilizokuwa mahali ambazo Abdul alikuwa anachota kuwagiwa wakina Wenje, Lissu na wengine ndani ya CHADEMA kama hongo.

Fikra Huru hazipo hivi Mkuu
 
Samia ni Rais wa nchi Mzee.
Kumueleza shida yako ni sehemu ya utaratibu wa kawaida na upo kisheria.

Rais lazima asikilize wananchi wake na kuwasaidia, Lisu anamuita Samia Rais. Ni kiongozi wake.

Ni Sawa na Mimi niende kwa Mkuu WA Mkoa kuomba msaada Fulani. Au nitafute mawasiliano ya Rais ili Kupata msaada Fulani.

Lakini kumtafuta mtoto wa Mkuu WA Mkoa au mtoto wa Rais huo sio utaratibu.

Yoda Leo umejionyesha jinsi ulivyo.
Wewe ndiye hujui, kisheria Rais sio mgawa haki nchi hii wala hatakiwi kushawishi maamuzi fulani ya utoaji haki yafanyike kwa sababu eti yeye ni Rais. Mahakama ndio chombo cha mwisho cha utoaji haki, kama Lissu alinyimwa pesa zake na bunge au na serikali angeenda Mahakamani na uamuzi wa mahakama ndio ulipaswa kuwa final.

Ni mfumo dhaifu tu wa haki ndio unaotoa mwanya wa wakuu wa mikoa, wilaya, mawaziri na Rais kufanya maamuzi ya kugawa haki mfano katika kesi za ardhi, kodi, mirathi n.k ila sio utaratibu sahihi wala sheria
 
Back
Top Bottom