Mzazi ananilazimisha kwenda kidato cha Tano

Mzazi ananilazimisha kwenda kidato cha Tano

Designing ya nini?
Tuanzie hapo maana huwa mna ndoto za kizungu sana katika nchi ambayo kutwa rasilimalu zinauzwa.
Mtakufa vibaya nyie nawahurumiaaaa
Unataka aende 5 akasome nini cha ajabu au ndio ninyi bado mna mawazo ya kijinga ya kusomea ualimu, hamjui dunia inakwenda wapi, kwa taarifa yenu elimu ya sasa haijali umesomea mambo ya uzunguni au wapi, cha msingi iwe inakwenda na wakati, amkeni vilaza nyie
 
Ungekuwa unaenda chuo kusomea kozi za skills za kueleweka. Kama ufundi magari, umeme,. Unesi , ufundi electronics,, Ningekusapoti.

Ila mambo ya kwenda chuo kusomea designing naona haupo serious na maisha.

Ni bora uende advance
Huko Advance anapata nini? Cheti cha form6 ni wapi utakitumia kupata kazi? elimu ya form6 inakupa ujuzi gani zaidi ya takataka za kukalili ambazo hazina impact katika maisha ya uhalisia, ifike wakati tuelewa hii elimu yetu haswa 5&6 haina umuhimu wowote zaid ya kupoteda muda, ni bora upate ujuzi hata wa kubeba zege kuliko kujaza manots kichwani yasiyo na faida.
 
Tatizo wazazi wengi wampeitia huko ndio maana wanaamini ndio njia sahihi lakini ukweli ni kwamba kama nyumbani kuna uwezo wa kulipa ada ya chuo ni heri mtu aende chuoni, huko 5 na 6 ni kwa wale wasio na uwezo wa kwenda chuoni ama walae wanaotaka kuwa walimu wa advance

Kwenda chuo kuna faida ambazo mtu wa form 6 hawezi kuja kuzipata,

mimi nilisoma form 6 naingia chuoni kusome degree nakutana na wale waliosoma diploma tayari wapo wenye kazi tayari wanajisomesha, yaani wanaongeza elimu ya degree ili wapandishwe madaraja sio kuanza kutafuta ajira kama sisi

Waliowahi kuanza chuo mapema wana uwanja wa ajira mkubwa, wao wanaweza kuomba kazi za diploma na degree lakini wale wa form 6 wanaomba kazi za degree tu, kazi za diploma nafasi 10 zinatangazwa unakuta wanaoomba ni 500 lakini kazi za degree nafasi 10 wanaoomba ni elf 10,

Kitu kingine ni kwamba wanaoenda kusomea diploma wana cv inayovutia kiuzoefu kuzidi aliesoma form 6, ni kwamba wao wamesomea taaluma kwa muda mrefu zaidi tangu wamemaliza form 4, wana vyeti vya kitaaluma vingi (certificate + diploma + degree) na pia wana wamefanya kazi kwa vitendo maofisini zaidi kuliko yule wa form 6 anaeanza kusomea taaluma kwa mara ya kwanza baada ya form 6.

Urahisi wa Kubadili kozi, Mtu wa diploma anaweza kubadili kozi baada ya kupata muda wa kutafakari kwa kina akiwa chuoni kozi anayoona itamfaa, Mfano anaanza kusomea certificate ya mwaka moja designing lakini huko chuoni anakuja kuona kuna kozi nyingine nzuri zaidi, akiingia diploma anabaili kozi na huko anaweza kuona kuna kozi flani anaweza kupata connection ajira, akiingia degree anabadili, wale wa form 6 hawana urahisi katika hili

Kuzoea maisha ya chuo mapema, Nakumbuka nikiwa chuoni baada ya kumaliza form 6 watu wengi ule mwaka wa kwanza walikuwa hawafanyi vizuri kwenye masomo kwajili ya ugeni wa vitu vingi kuanzia uhuru wa maisha ya chuoni, style ya kusoma, kuandaa assignments, presentations, n.k. muda huo wenzetu waliosoma diploma washavizoea, Ni kweli kwamba waliokuwa wanakimbiza ni wale vipanga wa form 6 lakini pia waliokuwa wanafeli sana ni hao hao wa form 6, wale wa diploma walikuwa average na ni kwasababu kipindi hicho wengi walikuwa wana divison 4 form 4, lakini siku hizi hata wenye division 1 na 2 wanaenda naamini hali imebadilika.
 
Huko Advance anapata nini? Cheti cha form6 ni wapi utakitumia kupata kazi? elimu ya form6 inakupa ujuzi gani zaidi ya takataka za kukalili ambazo hazina impact katika maisha ya uhalisia, ifike wakati tuelewa hii elimu yetu haswa 5&6 haina umuhimu wowote zaid ya kupoteda muda, ni bora upate ujuzi hata wa kubeba zege kuliko kujaza manots kichwani yasiyo na faida.
Kwani ukisoma Advance unashindwa kwenda Chuo. Sijaona point yako ya kwenda vyuo vya kati kama una ufaulu mzuri Form 4
 
Unataka aende 5 akasome nini cha ajabu au ndio ninyi bado mna mawazo ya kijinga ya kusomea ualimu, hamjui dunia inakwenda wapi, kwa taarifa yenu elimu ya sasa haijali umesomea mambo ya uzunguni au wapi, cha msingi iwe inakwenda na wakati, amkeni vilaza nyie
Akienda advance ndio hapo ataanza kupata elimu halisi ya kuweza kupambanua ni kipi atakachoweza/kumuddu kufanya mbeleni. Hiyo elimu alopata ya F4 inaitwa O-level manake yuko sifuri kimwelekeo. Bada ya hapo akienda F5 - 6 ndo akili itafunguka.
Unanikumbusha enzi zile eti ukiwa F2 unawakejeli walimu na kuwatambia wenzako kwa msemo eti Hela yangu haihesabiwi kwa "x" na "y". Kumbe hatukujua maisha sio suala la x na y, bali ni zaidi ya hapo.
 
Unataka aende 5 akasome nini cha ajabu au ndio ninyi bado mna mawazo ya kijinga ya kusomea ualimu, hamjui dunia inakwenda wapi, kwa taarifa yenu elimu ya sasa haijali umesomea mambo ya uzunguni au wapi, cha msingi iwe inakwenda na wakati, amkeni vilaza nyie
Sawa mzungu, endelea kumpumbaza kondoo mwenzio. Na ujuaji unawaharibu sana .
 
Nenda chuo achana na hayo matakataka ya form 5&6 hayana maana katika ulimwengu wa sasa zaidi ya kupoteza muda, wazazi wasio jielewa ndio hao wasiojua dunia iko wapi wanalazimisha watoto waishi zama za ujima za miaka 20 iliyopita wakidhani elimu bado ni ile ile.

Huyo mzazi wako asipokuelewa mtafute mtu mzima mwenye busara amueleweshe ajue mambo yako vipi, ni vilaza pekee hupeleka watoto A-level kwenda kupoteza muda, na ukiwauliza elimu ya 5&6 ina manufaa yapi, hawajui zaidi ya kukalili ujinga.

Ni wakati sasa wa kufuta huu mfumo mbovu wa kupoteza muda masomoni ktk mambo yasiyo na maana.

Nenda chuo ukapate maarifa& vyeti, ikishindikana nenda hata VETA na sio hiyo takataka ya 5&6
Asante sana kwa maana nyakati hizi advanced imekuwa ngumu Sanaa nimeenda pre form five nimechoka mapemaaa mambo ni mengi yanaumiza kichwa
 
Tatizo wazazi wengi wampeitia huko ndio maana wanaamini ndio njia sahihi lakini ukweli ni kwamba kama nyumbani kuna uwezo wa kulipa ada ya chuo ni heri mtu aende chuoni, huko 5 na 6 ni kwa wale wasio na uwezo wa kwenda chuoni ama walae wanaotaka kuwa walimu wa advance

Kwenda chuo kuna faida ambazo mtu wa form 6 hawezi kuja kuzipata,

mimi nilisoma form 6 naingia chuoni kusome degree nakutana na wale waliosoma diploma tayari wapo wenye kazi tayari wanajisomesha, yaani wanaongeza elimu ya degree ili wapandishwe madaraja sio kuanza kutafuta ajira kama sisi

Waliowahi kuanza chuo mapema wana uwanja wa ajira mkubwa, wao wanaweza kuomba kazi za diploma na degree lakini wale wa form 6 wanaomba kazi za degree tu, kazi za diploma nafasi 10 zinatangazwa unakuta wanaoomba ni 500 lakini kazi za degree nafasi 10 wanaoomba ni elf 10,

Kitu kingine ni kwamba wanaoenda kusomea diploma wana cv inayovutia kiuzoefu kuzidi aliesoma form 6, ni kwamba wao wamesomea taaluma kwa muda mrefu zaidi tangu wamemaliza form 4, wana vyeti vya kitaaluma vingi (certificate + diploma + degree) na pia wana wamefanya kazi kwa vitendo maofisini zaidi kuliko yule wa form 6 anaeanza kusomea taaluma kwa mara ya kwanza baada ya form 6.

Urahisi wa Kubadili kozi, Mtu wa diploma anaweza kubadili kozi baada ya kupata muda wa kutafakari kwa kina akiwa chuoni kozi anayoona itamfaa, Mfano anaanza kusomea certificate ya mwaka moja designing lakini huko chuoni anakuja kuona kuna kozi nyingine nzuri zaidi, akiingia diploma anabaili kozi na huko anaweza kuona kuna kozi flani anaweza kupata connection ajira, akiingia degree anabadili, wale wa form 6 hawana urahisi katika hili, wengi inabidi warudie upya kusomea degree.

Kuzoea maisha ya chuo mapema, Nakumbuka nikiwa chuoni baada ya kumaliza form 6 watu wengi ule mwaka wa kwanza walikuwa hawafanyi vizuri kwenye masomo kwajili ya ugeni wa vitu vingi kuanzia uhuru wa maisha ya chuoni, style ya kusoma, kuandaa assignments, presentations, n.k. muda huo wenzetu waliosoma diploma washavizoea, Ni kweli kwamba waliokuwa wanakimbiza ni wale vipanga wa form 6 lakini pia waliokuwa wanafeli sana ni hao hao wa form 6, wale wa diploma walikuwa average na ni kwasababu kipindi hicho wengi walikuwa wana divison 4 form 4, lakini siku hizi hata wenye division 1 na 2 wanaenda naamini hali imebadilika.


Unataka kusomea designing ya nini
Mkuu, umesahau mfumo wa ajira ulivyo siku hizi. Ukiajiriwa kwa cheti cha Diploma utaogelea na Diploma yako na utapanda vyeo(Promotions) hadi ufikie Bar. Ukienda kusoma Degree ukirudi utaajiriwa upya kwa cheti cha degree. Hapo ndipo penye changamoto na mtu anaweza kupata stress kwa sababu utakapoajiriwa kwa cheti cha Degree utaanza upya "Kuajiriwa mwenye cheti cha degree" na hapo ni daraja D ilahli ulipokuwa na diploma pengine ulishafika daraja F. Kwa hiyo utajikuta una mshahara mdogo kuliko yule aliyebaki na diploma yake.
 
Nenda chuo achana na hayo matakataka ya form 5&6 hayana maana katika ulimwengu wa sasa zaidi ya kupoteza muda, wazazi wasio jielewa ndio hao wasiojua dunia iko wapi wanalazimisha watoto waishi zama za ujima za miaka 20 iliyopita wakidhani elimu bado ni ile ile.

Huyo mzazi wako asipokuelewa mtafute mtu mzima mwenye busara amueleweshe ajue mambo yako vipi, ni vilaza pekee hupeleka watoto A-level kwenda kupoteza muda, na ukiwauliza elimu ya 5&6 ina manufaa yapi, hawajui zaidi ya kukalili ujinga.

Ni wakati sasa wa kufuta huu mfumo mbovu wa kupoteza muda masomoni ktk mambo yasiyo na maana.

Nenda chuo ukapate maarifa& vyeti, ikishindikana nenda hata VETA na sio hiyo takataka ya 5&6
Nanukuu: Nenda chuo ukapate maarifa& vyeti, ikishindikana nenda hata VETA na sio hiyo takataka ya 5&6.
1.Akienda Chuo sio lazima (Guarantee)atapata cheti kwani kuna kufeli au kufukuzwa vilevile.
2. Akipata cheti say Diploma ina maana ametumia 2 yrs. tayari. Usisahau Hakuna ajira. Tuseme amebahatika kupata ajira. Akiajiriwa atafanya kazi kwa 3yrs. ndipo aweze kuruhusiwa (eligible for further studies) kwenda Chuo kikuu.
Wakati huo muda wa 5 yrs yule aliyeenda Degree just after F6 atakuwa ameshamaliza kusomea e.g. Udaktari, Uhandisi n.k. Huyo mwenye Degree akiajiriwa, anazo fursa nyingi zaidi ya mwenye diploma.
Kuwa na cheti cha Diploma kunamnyima fursa nyingi e.g. nafasi ya uongozi au kupewa madaraka katika kitengo, hatakuwa na qualifications za kuomba Scholarships nje ya nchi au hata ndani ya nchie.g. zile ambazo ni Donor funded programmes lakini mwisho wa yote ni pale vigezo vya kuwepo katika ajira vikibadilika.Tunao uzoefu kwa waliokuwa na cheti(Certificate) katika fani ya Kilimo na Mifugo -walitakiwa wakasome au kupunguzwa kazini retrenchment.
Huenda ikafika siku isiyo na jina Diploma nayo ikaonekana haikidhi viwango. Utakuwa mgeni wa nani na ka-diploma kako?
Huko Private Sector sio haba. Uwe na cheti hata degree kama huna mjomba huko ujue hung'ati kitu hapo.
Kwa kifupi ni kwamba Degree bado ina hadhi yake na uwanja mpana zaidi asikudanganye mtu.
 
Huko Advance anapata nini? Cheti cha form6 ni wapi utakitumia kupata kazi? elimu ya form6 inakupa ujuzi gani zaidi ya takataka za kukalili ambazo hazina impact katika maisha ya uhalisia, ifike wakati tuelewa hii elimu yetu haswa 5&6 haina umuhimu wowote zaid ya kupoteda muda, ni bora upate ujuzi hata wa kubeba zege kuliko kujaza manots kichwani yasiyo na faida.
Kuna faida na hasara, so ni kiasi cha kuvipima hivyo viwili. Ningeshiriki mjadala huu, ila naona wengi mnaandika bila hoja
 
Nilimsikiliza mzazi wangu na mpaka leo najutia baada ya kumaliza akaniambia alikuwa haelewi form 5 na 6 sio muhimu.Ila kabla tulibishana Sana mpaka akaniambia Mimi ni mbishi nikiharibikiwa ndyo Huwa nakubali.


Kataaa Kataaa Kataaa nenda huko unakokutaka baada ya Miaka 3 kuisha utanikumbuka na utajipongeza.
 
Kwenda A level ni kupoteza mda. Ila kusomea designing kwa nchi kama yetu ili upige pesa you have to be the best in what you do, otherwise ni heri kwenda chuo kusoma technical specialties. There are varieties of choices as a technician.
 
Nilimsikiliza mzazi wangu na mpaka leo najutia baada ya kumaliza akaniambia alikuwa haelewi form 5 na 6 sio muhimu.Ila kabla tulibishana Sana mpaka akaniambia Mimi ni mbishi nikiharibikiwa ndyo Huwa nakubali.


Kataaa Kataaa Kataaa nenda huko unakokutaka baada ya Miaka 3 kuisha utanikumbuka na utajipongeza.
Mhhhh. Mkuu; Inaweza kuwa ndo mwanzo wa mikosi e.g. Mzazi anaweza kuzira kumlipia, huko unakomshauri aende mambo yanaweza yasimwendee vizuri kwa kukosa baraka ya mzazi n.k. Bora ungemshauri afanye kumbembeleza mzazi kwa hoja zenye mashiko ili aridhie na sio kukaza shingo.
 
Asante sana kwa maana nyakati hizi advanced imekuwa ngumu Sanaa nimeenda pre form five nimechoka mapemaaa mambo ni mengi yanaumiza kichwa
Acha uvuvi binti, hakuna ugumu wowote soma binti .....somaaa bila kukoma
 
Back
Top Bottom