Mzazi mwenzangu hahudumii mtoto; nataka nimpeleke mahakamani

Siku hizi humu jukwaani kumejaa watoto wadogo sana wanaotumia sehemu ndogo sana ya akili zao kujibu au kutatua mambo......utalifahamu hilo kupitia majibu yao.....

Kuachana na mwenza ni vitu vya kawaida kutokana na changamoto kadhaa ambazo pengine zimeshindwa kutatulika na wawili hao wakamua kwa amani na usalama kila mmoja aishi maisha yake......

Lakini kutengana na mwenza hakuondoi uwajibikaji wako kama mzazi juu ya mtoto au watoto wenu.....kwa maana ya kuhakikisha watoto au mtoto anapata huduma sitahiki kulingana na uwezo au kipato Cha mzazi wake.......

Vijana wengi wakichana na mwenza wanatoa sababu zisizo na kichwa wala miguu ili kuepuka uwajibikaji kama baba wa mtoto......na ndio maana mamlaka au taasisi zinazosimamia Hilo kwa manufaa na maslahi ya mtoto na sio mama.......

Unapoachana na mkeo jukumu la kumuhdumia mwanamke ndio linakoma hapo na linabakia la watoto au mtoto wako........

Ewe Binti kama una hakika uwezo wa kuhudumia kwa maana ya kipato anao basi fuata taratibu ili alazimishwe kufanya hizo na mamlaka kama ameshindwa kuwajibika kwa khiyari yake........

Guys hivi mnajenga taswira gani kwa watoto wenu hapo mbeleni angali anashuhudia mnavyokimbizana mahakamani au kwenye korido za ustawi wa jamii na mama yake ili kukulazimisha wewe kumhudumia......hivi unadhani mtoto atakuthamini kama baba.....??

Vijana msitumie mzigo wa malezi ya mtoto kama njia za kuwaadhibu wanawake mlioachana nao.....wajibika kama baba ili kuendelea kujenga uhusiano mzuri na watoto wenu.......maneno mabaya atakayolishwa na mama yake kwa hasira na visirani vinazimwa na matendo mema kwake..,....
 
Kesi Kama hii ukikutana na wanaume wa Aina yangu ni kujitafutia tuu chuki tena Kama hatukuachana vizuri.

Kama hutaki kuishi na mwanao basi Mpeleke Mahakamani,

Mtoto wa miaka 9 Kama umeshindwa kumlea si umuachie Baba yake.
Kinachokufanya umng'ang'anie ni nini wakati huwezi kumtunza,
 
Itakuwa alaidanganywa na njemba huko kuwa usijali nitakuhudumia mpenzi...sasa jamaa ndio kala mbususu kajisepea zake๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ
Just an assumption ppl!
 
Kuna Mwanamke nilizaa naye aisee, Kila siku anataka Hela, Kuna siku akasema mtoto anahitajika kutoa Hela ya research shilingi laki Moja, nikauliza mtoto wa darasa la tatu anafanya research ya nini?

Wamama wanazingua sana
 
MRudishe kwa baba yake
 
๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ Aisee yaani wanawake kwa kutusema sie wanaume suruali ila wao sijui tuwaite wanawamke mbususu tuu ama....mtoto ulie mtoa kwenye mbususu yako mwenyewe unashindwa kumsomesha kweli una akili au matope humo kichwani
Darasa la nne hamna ada, sijui huyo dada anafeli wapi? Kama kampeleka private school, je alijadiliana na mzazi mwenza kabla? Au aliona mtoto wa shosti wake anachukuliwa na school bus naye akatamani?
 
Tamaa gani hapo sasa? Unajua sababu za wao kuachana au mnaelezea hisia zenu za masahibu yenu? Mmevurugwa akili hata hamuwazi kujenga ni kubomoa tu kumewajaa vichwani. Ni malezi mabovu mlopitia au mna shida gani?Tafuteni dawa kabla hamjaokota makopo.
Huyu ndio mbomoaji asie kuwa na ufikirio kielekea mtoto.
Umeolewa, sasa unaachika vipi wakati unajua huwezi kumudu gharama za kumpeleka shule mwanao? Ni ubinafsi kujifikkria mwenyewe tuu hakufikiria kuhusu mtoto.
 
Hapo hawezi kupata kitu Kwa sababu kama ni haki ya mtoto kupata Elimu serikali ipo imetoa Elimu Bure na hakuna kifungu kinasema elimu iwe na ubora wa kiwango gani, lakin Mzazi mwenzie amesema hana uwezo wa kusomesha huko English medium kamruhusu auze nyumba, kumbe hata nyumba kaachiwa maana yake hajataka wagawane Mali maana kungekuwa na kugawana wangeuza wagawane pasu kwa pasu ndioo suala la malez ya watoto lianze. Huyo mwanamke hana akili ashaona amepoteza hivyoo anataka afosi kingi kupitia mtoto, na huyo aliyemoa jeuri atakuwa ameingia mitini
 
Kuna Mwanamke nilizaa naye aisee, Kila siku anataka Hela, Kuna siku akasema mtoto anahitajika kutoa Hela ya research shilingi laki Moja, nikauliza mtoto wa darasa la tatu anafanya research ya nini?

Wamama wanazingua sana

Mwanamke akiwa mkorofi unamfanyia umafia ndio dawa Yao hiyo.
Kwa maana hata ukienda vile atakavyo bado atamwambia mtoto kuwa humjali na humtunzi.

Ukishakuwa Korofu mwanamke atakuheshimu tuu kivyovyote iwe kisheria au kihunihuni/kimtaani.

Tena huyo wa miaka 9 ndio Kabisa
 

Hapa amekuja kuuliza kama aende mahakamani, mtoa mada nenda...ukikosa ndio umpeleke mtoto shule ya serikali. Nani asiyetaka mtoto wake aongee ngeli au aone uone mtoto wa mwenzio anaongea ngeli wakati wako haongei... ๐Ÿ˜† ๐Ÿ˜† na wakati unajua au unaona mzazi mwenzio ana uwezo wa kumpeleka mtoto?!...kusema tu 'sina uwezo' haitoshi...anahitajika ku verify mahakamani...mtoa mada nenda mwaya...mbivu na mbichi utazijua huko huko
 
Hicho ndio ninachokiona Kwa ndugu mtoa mada
 
Darasa la nne hamna ada, sijui huyo dada anafeli wapi? Kama kampeleka private school, je alijadiliana na mzazi mwenza kabla? Au aliona mtoto wa shosti wake anachukuliwa na school bus naye akatamani?

Huko kwa baba yake ndio kuna guarantee mtoto ataenda private school. Hilo libaba lisiloona mtoto wake ndio victim au mtoto wake ha deserve kwenda international school wakati ana uwezo...ni limwanaume suruali nalo.

๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Limwanaume suruali ndio limekuzalisha kumaanisha na wewe ni hamnazo tuu!

Sio lazima mtoto aende Private,

Yaani ukifika Mahakamani au ustawi wa jamii usijeongea mambo ya kipuuzi kama hayo Utaonekana kichwani ni chenga/cherema.
Ustawi wataona ndio maana uliachwa Kwa akili matope.

Mtoto anamiaka 9 amekushinda peleka Kwa Baba yake. Hutaki lea uwezavyo.

Mnajifanya mnaupendo Kwa watoto kumbe ujinga na upumbavu tuu.

Tangu lini upendo ukazidi Uwezo Kama sio akili za kijinga.

Baba yake labda anawatoto WA nje wengine wanne unafikiri ustawi wa jamii atasemaje,
Kipato changu ni 500,000 Kwa mwezi ninawatoto WA NNE, uwezo wangu ni Kutoa elfu 60.
Kama ataiona ndogo anipe mwanangu nilee.

TATIZO Lenu wanawake mnadhani nikizaa na wewe basi kwengine sina watoto. Hivyo unadhani mtoto wako ndio spesho.

Mtoto anayefaidi pesa ya Baba yake mara nyingi ni Yule anayetoka Kwa mwanamke anayejielewa/anayemheshimu Mume
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ