Mzazi mwenzangu hataki mtoto apate Elimu nzuri, nadhani hajui elimu ni kwa faida ya mtoto sio mimi wala yeye

Hata wazazi wa mzazi mwenzangu wanatamani mjukuu wao asome shule nzuri, tatzo ni mama yake....

Ila nitakwenda kuongea na Baba yake direct, Naamini atanielewa.

Kuhusu Mama yangu yeye hana tatzo kuhusu hilo, na anajua umuhimu wa elimu, hata ingekuwa ni yeye angekubali mtoto wake aende akapate elimu bora kwa kutambua kwamba huko alipo hakuna uwezo wa kupatiwa elimu nzuri.
 
Walikuja dar, wakaishi Vizuri na familia yangu, mtoto alikuwa na furaha sana, hata sasa mama yake anasema anasumbu sana anamtaka baba yake, kiufupi alizoea maisha ya huku na kuwa huru zaidi.

Sitaki au sitopenda akiishi na Baba mwingine
Makosa yanaanzia hapo. Hutaki aishi na baba mwingine kwanini hukumwoa huyo mwanamke na kama ulimwoa kwanini umevunja ndoa. Simply unachotaka kufanya ni kujimwambafai kuwa wewe ni kidume ila ina madhara kwa mtoto.
 
Makosa yanaanzia hapo. Hutaki aishi na baba mwingine kwanini hukumwoa huyo mwanamke na kama ulimwoa kwanini umevunja ndoa. Simply unachotaka kufanya ni kujimwambafai kuwa wewe ni kidume ila ina madhara kwa mtoto.
Nilipanga kumuona hata wazazi wake niliwaambia hilo, lakini alifanya mambo ya ajabu ambayo hata ingekuwa ni wewe usingekubali kuoa mwanamke wa aina hiyo.
 
Hujuia yamefikaje hapo, hujui nini sababu ya mzazi mwenzangu kuwa na jeuri wakati huu...

Hakuna kuyakayaga wala nini, maisha yanaendelea kama kawaida
Sababu yoyote ile ya kumfanya mzazi mwenzako kuwa jeuri wakati huu, ujeuri huo kukuathiri wewe leo kosa ni lako.

Hujaweza kumchunguza na kuelewa ujeuri wake kabla ya kuzaa naye. Hilo ni kosa lako.

Kama maisha yanaendelea kama kawaida, kwa nini unakuja kulialia hapa?
 
Kama maisha yanaendelea kama kawaida, kwa nini unakuja kulialia hapa?
Sio kulialia tu, hata nikitaka kupiga mayowe uhuru huo ninao, nimeandika kama wengine wanavyo andika...

Wewe ni nani unipangie sehemu ya kusema, au umevurugwa na changamoto za maisha unajaribu kupooza bichwa kwenye thread yangu?
 
Mnazaa hovyo kama simbilisi halafu kulea hamuwezi, shenztype.
 
Hatuna tena mahusiano, kila mtu anafanya mambo yake lakini bado huduma natoa, na shule ni jukumu langu ila kama akikataa atamsomesha yeye.
Kwanini unamiini kuwa akija Dar tu ndio atasoma shule bora?. Mfano hata kama kijijini hakuna shule hiyo bora, kwanini usimlipie aende akasome kwa ndugu yake yeyote mkoa wowote hata hapa Dar kama ana ndugu, halafu wewe umlipie hiyo shule bora?
Wewe inaonekana pia una shida, unataka kumchukua mtoto kwa gia ya kumsomesha shule bora.
 
Wewe inaonekana pia una shida, unataka kumchukua mtoto kwa gia ya kumsomesha shule bora.
Sasa hiyo ni shida mkuu? Hakuna ndugu yake anayeweza kukaa na mtoto, mimi pia sio kama nataka kukaa naye, ila akae na Bibi yake then asome shule nzuri.
 
We ndo una amua, ukiendekeza ujinga Kama huu utakuja teseka sana baadae, toa kauli, cha maana aiumizi mtu, kataa mijadala!
Kauli yangu ni kwamba wakimpeleka shule wanayotaka wao, gharama zitakuwa juu yao.
 
KAma una malengo ya mtoto uyo asome shule nzuri (Bus la njano) basi tuma ada ataftiwe za huko sio mpka aje Dar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…