Mzazi zungumza na mwanao kila mara, dunia imeharibika hii

Mzazi zungumza na mwanao kila mara, dunia imeharibika hii

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
blended-families.jpg


Wakuu, nimewaza sana kuhusu malezi ya watoto leo. Wazazi tunapaswa kujua mabadiliko ya tabia za watoto yanategemea zaidi ukaribu walionao kwa Mzazi au Mlezi wao na kwa kiasi gani Wazazi wanazungumza kuhusu makuzi, fursa, hatari zilizo mbele yao na jinsi ya kuzikabili au kuziepuka.

Watoto wengi wanajikuta kwenye mazingira hatari ya kudhurika Kiakili, Kisaikoloji au Kimwili kwasababu hawana watu wa kuzungumza nao mambo yao kutokana na baadhi ya Wazazi kutokuwa na utaratibu wa kuwasikiliza Watoto.

Kama unatamani au kutarajia makubwa kwa Mwanao, basi ukiwa kama mzazi kuwa na utaratibu wa kuzungumza na kuwapa nafasi Watoto kusema vitu wanavyofikiria, wanavyokutana navyo kila siku Shuleni, maeneo ya michezo na makazi yao. Pia, jua aina na tabia za watu wanaoshinda nao ili kuepusha madhara yanayoweza kuepukika.

Samaki Mkunje Angali Mbichi....
 
Mkuu huu ushauri upon siku nyingi sana, nilidhani Kuna kitu kipya umeongeza kumbe hola.
 
Ulinzi tosha ni kuwaombea na kuwatolea sadaka mara kwa mara. Watakaa kwenye mstari.
Ulinzi wa Mungu ni 24hrs.
Huko unapoenda kutoa sadaka ndio wanaongoza kuwalawiti hao watoto.
 
If you want to destroy the society first start to destroy religion and then make a children away from their parents and that is whats happening now in our society but the outcome will be estimated in the future.
 
Malezi ni magumu aisee ukizungumza nao utandawazi unazungumza nao zaidi,
 
Back
Top Bottom