Hatimae katibu wa baraza la wazee yanga ameuomba uongozi pamoja na wanachama&mashabiki wa chama kubwa hapa bongo msamaha kwa kauli zake za hovyohovyo,hayo ameyasema leo katika kipindi cha sportsHQ kupitia redio pendwa kwa sasa efm
Hivyo wanayanga wenzangu tusiwe na waswasi timu iko imara,tuendelee kutembea kifua mbele,nnauhakika manji hawezi ondoka,na kubwa tujae kesho taifa kuchukua kombe letu. Salam ziwafikie kule sharubu fc.
==============
Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga, Yahya Akilimali amesimamishwa uanachama kwa tuhuma za kumkashifu Yusuf Manji.
Sijamtusi M/kiti kwa kusema amekurupuka. Neno hilo ni la kawaida, sikuwa na dhamira ya kumtusi, nawaomba radhi wana-Yanga- Yahya Akilimali