Mzee Akilimali atuomba radhi, lakini amesimamishwa uanachama wa Yanga

Mzee Akilimali atuomba radhi, lakini amesimamishwa uanachama wa Yanga

Aibu kubwa kwa klabu kubwa kama Yanga kwenda kumpigia magoti Gabacholi!
Yanga ni taasisi ambayo inahitaji watu wenye uwezo wa kifedha ili itekeleze majukumu yaliyopo usoni siyo taasisi ya kihistoria eti palikuwa mahala pa kuandaa mikakati ya kudai uhuru. Hivyo kwa nyakati hizi lazima utafute watu wenye mtaji kama akina Manji, Mohammed Dewji Moo siyo tena kudhani rundo la wapenzi linaweza ndiyo maana hizi timu kwa sasa ili kupambana na akina Azam lazima zibadilike kwa kila hali. Tulio wengi ni wapenzi ambao hata hatuwezi kuchangisha pesa ya kuingia sokoni kutafuta akina Mavugo, Chirwa, Ngoma nk. Hii inatokana na vilabu vyetu kuwa na sera na mipango ambayo imepitwa na wakati ilihali wapenzi wa timu wanahitaji mambo makubwa kutoka ktk uwekezaji hafifu. Timu ikiongozwa na mwenye mtaji atakuwa na malengo ya muda mrefu siyo hawa akina Aveva ...
 
Yanga ni taasisi ambayo inahitaji watu wenye uwezo wa kifedha ili itekeleze majukumu yaliyopo usoni siyo taasisi ya kihistoria eti palikuwa mahala pa kuandaa mikakati ya kudai uhuru. Hivyo kwa nyakati hizi lazima utafute watu wenye mtaji kama akina Manji, Mohammed Dewji Moo siyo tena kudhani rundo la wapenzi linaweza ndiyo maana hizi timu kwa sasa ili kupambana na akina Azam lazima zibadilike kwa kila hali. Tulio wengi ni wapenzi ambao hata hatuwezi kuchangisha pesa ya kuingia sokoni kutafuta akina Mavugo, Chirwa, Ngoma nk. Hii inatokana na vilabu vyetu kuwa na sera na mipango ambayo imepitwa na wakati ilihali wapenzi wa timu wanahitaji mambo makubwa kutoka ktk uwekezaji hafifu. Timu ikiongozwa na mwenye mtaji atakuwa na malengo ya muda mrefu siyo hawa akina Aveva ...
Hivi Manji anao mtaji wa kuwekeza Yanga? Au anataka kuitumia Yanga?!. Juzi ameambiwa aweke hadharani mkataba wa kutumia jezi za Yanga kutangaza biashara zake ameshindwa.
 
Mbona nasikia wanachama wanataka kumpa timu Mengi na Devis Mosha hivi hizi habari zina ukweli!!!
 
Hatimae katibu wa baraza la wazee yanga ameuomba uongozi pamoja na wanachama&mashabiki wa chama kubwa hapa bongo msamaha kwa kauli zake za hovyohovyo,hayo ameyasema leo katika kipindi cha sportsHQ kupitia redio pendwa kwa sasa efm

Hivyo wanayanga wenzangu tusiwe na waswasi timu iko imara,tuendelee kutembea kifua mbele,nnauhakika manji hawezi ondoka,na kubwa tujae kesho taifa kuchukua kombe letu. Salam ziwafikie kule sharubu fc.

==============
Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga, Yahya Akilimali amesimamishwa uanachama kwa tuhuma za kumkashifu Yusuf Manji.

Sijamtusi M/kiti kwa kusema amekurupuka. Neno hilo ni la kawaida, sikuwa na dhamira ya kumtusi, nawaomba radhi wana-Yanga- Yahya Akilimali
AKILI MALI,,,Huyu mzee hana watoto wakamshaur?namuona kama anajidhalilisha flani hivi
 
Mimi nadhani ni vizuri timu zetu ziendeshwe kibiashara zaidi,porojo za kusema timu imekodishwa kwa miaka 10 hazina msingi wowote,mpira pesa siku hizi,,
 
uploadfromtaptalk1471342538279.jpeg
 
Hivyo wanayanga wenzangu tusiwe na waswasi timu iko imara,tuendelee kutembea kifua mbele,nnauhakika manji hawezi ondoka,na kubwa tujae kesho taifa kuchukua kombe letu. Salam ziwafikie kule sharubu fc.

Nijuavyo mimi Ngao ya jamii inashindaniwa na bingwa wa Ligi Kuu na bingwa wa Kombe la Shirikisho. Kwa sasa Yanga ni bingwa wa Ligi Kuu na pia ni bingwa wa Kombe la Shirikisho hivyo TFF wanatakiwa kutukabidhi ngao yetu kisha hiyo mechi ya kesho inakuwa ni ceremonial tu, tushindwe au tushinde inabidi ngao yetu tukabidhiwe. Sijui kanuni za TFF zinasemaje katika hili lakini kwa mizania ya haki ni wazi kuwa hiyo Ngao ya Jamii ni ya Yanga kwa mwaka huu, aliitwaa ngao hiyo baada ya kuchukua makombe yote mawili hivyo kesho haitakiwi kuwa mechi ya kushindania ngao ya jamii bali ni burudisho kwa wapenda soka kabla ya ligi kuu kuanza.

CC. Jamal Malinzi (aione kwenye akaunti yake).
 
Hivi kukurupuka ni tusi ? Ndio hivyo tena wenye pesa na mamlaka wataendelea kuabudiwa
 
Huyo anataka kuutumia vibaya umaskini wa fikra wa Wanayanga. Na wenyewe wanataka kubweteka. Hatumuombei mabaya, je leo Mwenyezi Mungu akimchukua Yanga itajiendesha? Huu utumwa wa fikra ndio watu wengi wanaukataa. Haiwezekani Klabu kubwa kama Yanga iwe inaendeshwa kama SACCOS ya Manji na ukoo wake!
Mkuu mbona manji amesema kuwa anaandaa kampuni ambayo itakuja kuikodisha timu,mna haraka gani?
 
Huyo anataka kuutumia vibaya umaskini wa fikra wa Wanayanga. Na wenyewe wanataka kubweteka. Hatumuombei mabaya, je leo Mwenyezi Mungu akimchukua Yanga itajiendesha? Huu utumwa wa fikra ndio watu wengi wanaukataa. Haiwezekani Klabu kubwa kama Yanga iwe inaendeshwa kama SACCOS ya Manji na ukoo wake!
Nivizuri mtazamo wako kama huu usiambatane na majina au hisia za kibaguzi. Huu ni mtazamo wako na hata mimi siupingi haipendezi ukisemwa kibaguzi.
 
Hayo mambo ubishi ndio yalioishusha Coastal union matajiri waitaka wenyewe ubishi tu hiyoooo shuka kabisa
 
Yani yanga na mashabiki wake wameamua kubadilisha hoja kutoka kwamanji hadi kwa mzee wa watu.
 
siku hawa wazee watakapofutika duniani ndipo yanga itakapofanya vizuri. wakiwepo hawa, yanga imetawaliwa na imani za kichawi na mashindano ya wao kwa wao. kila unachokifanya wazee wanataka waabudiwe kwanza kwasababu wao ndio wazee wa mila hapo jangwani, ukienda vibaya tu unafungwa. tutatawaliwa na imani za kizee hadi lini? Mungu awape maisha marefu hata wakifika miaka 100 haina shida, ila siku Mungu atakapoamua kuwachukua hapa duniani ndipo yanga itakuwa timu bora.
 
Manji atayaweza Majungu na uchawi wa Akili mali?
 
Back
Top Bottom