Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,892
- 16,476
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu Watanzania;
Kama kuna matukio yaliouchoma moyo wangu ndani ya mwaka huu wa 2020 basi ni kifo cha huyu mzee Augustine Philip Mahiga. Huyu baba sikubahatika kuonana naye ana kwa ana lakini ndiye aliyekuwa "role model" wangu katika kupenda masuala ya kidiplomasia na siasa za kimataifa.
Siku moja ninatamani kuja kuwa mwanadiplomasia makini na mwanasiasa mstaarabu kama yeye. The guy was sincerely humble and kind, mwanasiasa muungwana na mstaarabu kweli kweli.
Roho inaniuma sana sikuweza kuhudhuria msiba pamoja na mazishi yake kutokana na changamoto ninazozipitia sasa katika maisha yangu lakini ipo siku nikienda Iringa nitapita katika kaburini lake walau nisimame dakika tano niangalie pahala alipolala huyu shujaa wangu.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO NA UIPENDE TANZANIA KAMA MZEE AUGUSTINE MAHIGA.
Ndugu zangu Watanzania;
Kama kuna matukio yaliouchoma moyo wangu ndani ya mwaka huu wa 2020 basi ni kifo cha huyu mzee Augustine Philip Mahiga. Huyu baba sikubahatika kuonana naye ana kwa ana lakini ndiye aliyekuwa "role model" wangu katika kupenda masuala ya kidiplomasia na siasa za kimataifa.
Siku moja ninatamani kuja kuwa mwanadiplomasia makini na mwanasiasa mstaarabu kama yeye. The guy was sincerely humble and kind, mwanasiasa muungwana na mstaarabu kweli kweli.
Roho inaniuma sana sikuweza kuhudhuria msiba pamoja na mazishi yake kutokana na changamoto ninazozipitia sasa katika maisha yangu lakini ipo siku nikienda Iringa nitapita katika kaburini lake walau nisimame dakika tano niangalie pahala alipolala huyu shujaa wangu.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO NA UIPENDE TANZANIA KAMA MZEE AUGUSTINE MAHIGA.