Mzee Juma Duni Haji: Wanaotaka Mbowe aendelee kusota Mahabusu wako Ulaya

Mzee Juma Duni Haji: Wanaotaka Mbowe aendelee kusota Mahabusu wako Ulaya

Ukiondoa wanao mshikilia sidhani kama kuna mtu ambae hataki Mbowe atoke. Tofauti ni namna atakavyotoka. Chama chake kinasema kwa sababu hajafanya kosa lolote basi DPP atangaze tu kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hivyo ataachiwa. Wengine wanasema kuwa aombe msamaha tu hata kama anajua kuwa hajafanya kosa ili atoke. Shida ya kuomba msamaha ni inamaanisha umekiri kuwa umetenda kosa uliloshitakiwa. Kwa sababu hiyo Mbowe atajulikana kuwa ni gaidi kwa kwenda mbele. Sidhani kama kuna watu wanakataa watu kufanya wanaloweza ili Mbowe aachiwe mradi tuu hawamlishi maneno kuwa ameomba msamaha. Ingekuwa hawataki atoke wasingefanya jitihada kubwa kuomba mataifa ya nje kuishinikiza serikali imuachie Mbowe. Au wasingeendelea kupaza sauti kuwa " Mbowe sio Gaidi".

Amandla...
Unfortunately kwa katiba yetu ilivyo, DPP hashinikizwi. Ukiona DPP anashinikizwa huo ni uvunjwaji wa katiba mwingine tunaoukataa.
Kwa nini tusiache mahakama ifanye kazi yake na kama hana hatia mahakama itamuachia tu. Au hatuna imani na mahakama?
 
Mkuu kuna faida ya Mbowe kuwepo mahabusu ,michango ni mingi saaana hadi Mbowe anajenga mji wake pale machame ,wewe uliona wapi mfungwa anajenga ? Ndio ujue kwa nini nae anajifanya kungangania mahabusu mkuu
Acha uongo usio na faida.mbowe ang'ang'anie mahabusu kwani kajifunga mwenyewe.propaganda mfu kama hizi hazina faida kwako binafsi ata kwa familia yako.ata ivyo jenga nawewe mji wako tukuone.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Unfortunately kwa katiba yetu ilivyo, DPP hashinikizwi. Ukiona DPP anashinikizwa huo ni uvunjwaji wa katiba mwingine tunaoukataa.
Kwa nini tusiache mahakama ifanye kazi yake na kama hana hatia mahakama itamuachia tu. Au hatuna imani na mahakama?
Hatuna imani na Mahakama. Na tumeona DPP akifanya vitu visivyoeleweka kama kumfutia kesi Nusra usiku wa manane ili akaapishwe ubunge. Tunajua hana integrity ya kuamua mwenyewe bila kusukumwa kidogo.

Amandla...
 
Hatuna imani na Mahakama. Na tumeona DPP akifanya vitu visivyoeleweka kama kumfutia kesi Nusra usiku wa manane ili akaapishwe ubunge. Tunajua hana integrity ya kuamua mwenyewe bila kusukumwa kidogo.

Amandla...
Kama hatuna imani na mahakama, kisha tukawa hatuna imani na DPP, na pia kama hatuna imani na Viongozi, basi the only solution ni Peoples power, Ingizeni watu barabarani la sivyo kelele za chura hazimzuii mtu kulala usingizi
 
Mkuu kuna faida ya Mbowe kuwepo mahabusu ,michango ni mingi saaana hadi Mbowe anajenga mji wake pale machame ,wewe uliona wapi mfungwa anajenga ? Ndio ujue kwa nini nae anajifanya kungangania mahabusu mkuu
Kumbambikizia kesi mfanye ninyi halafu mnasema anang'anga'ania mahabusu!!!Akili za wapi?Mwambieni DPP amuachie bila masharti!
Pili,Mbowe sio mfungwa kama usemavyo,ni mtuhumiwa ambaye Yuko mahabusu!Suala la kujenga(kama ni kweli),sioni tatizo kwani uwezo Huo anao!Usitake umasikini wako ndio uwe kipimo Cha kila mtu!
 
Wanafiki wanaojifanya wanampenda sana mbowe wameibuka tena.Kesi ya mbowe iko wazi kua niyakubumba wala haiitaji mbwembwe au mtu kutafutia sifa zakisiasa.Na jukumu la kumaliza kesi liko mikononi mwa serikali yenyewe.sasa huyo Duni yeye ni nani hasa.Alishindwa kupambania mashehe wenzake wazanzibar kipindi wanasota magereza miaka na miaka ndo aje ampambanie mbowe.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Wewe na huyo Mzee wako Duni hamna akili au kama mnazo basi ni duni kama jina lake. Hamumjui Zitto Kabwe nyie wapemba,huyo amesha kuuzeni kwa CCM. Kazi yote aliyofanya Maalim Seif enzi ya uhai wake imefutwa na huyo Mrundi Zitto Kabwe.
Zitto kabwe sio chochote Zanzibar ata akiamua kusepa anasepa haondoki na chochote., Zanzibar wanachoringia ni base kubwa sana ambayo imejengwa na maalim seif miaka nenda miaka rudi ambayo ni rasilimali watu.

Zitto akizingua zanzibar wanabaki na watu wao wanaangalia movement nyengine., Ni hivyo tu., ie. Lipumba sjui mtatiro, mapalala wote wameondoka na aila zao., zanzibar wamebaki na lao moja tu wanapambana.

Nyinyi subirini clips za tundulisu toka belgiam na canada muendeshe chama chenu,
 
Kama hatuna imani na mahakama, kisha tukawa hatuna imani na DPP, na pia kama hatuna imani na Viongozi, basi the only solution ni Peoples power, Ingizeni watu barabarani la sivyo kelele za chura hazimzuii mtu kulala usingizi
Sio kila ufumbuzi lazima utatuliwe na maandamano ya watu.Binadamu mmoja anatosha kuleta mabadiliko ya nchi.kwahiyo subiri muda utaleta ufumbuzi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kama hatuna imani na mahakama, kisha tukawa hatuna imani na DPP, na pia kama hatuna imani na Viongozi, basi the only solution ni Peoples power, Ingizeni watu barabarani la sivyo kelele za chura hazimzuii mtu kulala usingizi
Sio kila kitu kitatatuliiwa na violence. Mimi siwaelewi kwa nini kila mara mnataka Chadema waingie barabarani maana kuna njia nyingi tu za kuonyesha People's Power. Sidhani kama unazijua kelele za chura. Hata ukilala kidogo ukiamka utawakuta bado wanaendelea.

Amandla...
 
Zitto kashawaharibu hawa wazee maskini...Zanzibar huru kwisha habari yake !!

We Mzee duni, kwani Mh. Mbowe yeye anasemaje? Unataka ampigia mwanadamu magoti mwanadamu? ...una hamu usikie tena..." nimekosaa mimiii nimekosaaa saana...naomba rqdhi mimiiiii "

Utasubiri sana.
 
Lema huyo!

Serikali huwa haikosei.

Duni yuko sahihi kabisa Freeman Mbowe atolewe gerezani!

Kwa hiyo anakosea serikali lakini lawama anapewa Lema na Lissu.
Zitto kabwe sio chochote Zanzibar ata akiamua kusepa anasepa haondoki na chochote., Zanzibar wanachoringia ni base kubwa sana ambayo imejengwa na maalim seif miaka nenda miaka rudi ambayo ni rasilimali watu.

Zitto akizingua zanzibar wanabaki na watu wao wanaangalia movement nyengine., Ni hivyo tu., ie. Lipumba sjui mtatiro, mapalala wote wameondoka na aila zao., zanzibar wamebaki na lao moja tu wanapambana.

Nyinyi subirini clips za tundulisu toka belgiam na canada muendeshe chama chenu,

Usisahau hayo yote yalitokea kwasababu Maalim Seif alikuwepo. Sasa hayupo hao waliopo wanao uwezo wa kusimamia harakati?. Kwasababu kwa Viongozi waliopo naona Kama movement itapoa Kama sio kufa.
 
Kwann kikwete asiitwe mdini? kwann mzee Mwinyi asiitwe mdini? kwann Salmin Ahmed asiitwe mdini? kwann Maalimu Seif hakuitwa mdini? unafikiri hoja ya kwamba zito ni mdini,mkabila,na mlafi kasingiziwa?
Kitu ambacho sielewi ni Zanzibar kurudishwa kwenye siasa za kinafiki na Zitto kibwege sana.
 
Mama muachie Mbowe maisha yaende ulidanganywa, wachaga hatudanganyiki kwa kujikosea kwenye machief wasiotambulika kutafuta huruma ya wachaga. Hio mikoa mingine Hakuna machief hadi uje uchagani.
 
Sasa ndugu Mbowe anatokaje? Kesi inaendelea, acha ukweli ujulikane baada ya hukumu. Hii mambo ya atoke asitoke haisaidii kwa sasa. Ni nani ana uwezo wa kumtoa Mbowe mahabusu kwa sasa? Watu msijifanye mna huruma sana na Mbowe wakati yeye mwenyewe hajasema kama anaomba msamaha kwa hiyo atolewe. Tuiache mahakama ifanye kazi yake ili tuje tujadili hapa baada ya hukumu kutolewa, iwe leo, kesho au 2026.. issue ya ugaidi sio ya mchezo, tunahitaji hukumu ambayo italeta pia mafunzo kwa hapo baadae kuhusu kesi kama hizi. Ni hayo tu mkuu.

NB: Mbowe anao uhuru wa kuandika memos na barua kwa watu kama ile aliyoiandika kwa Mwamakula. Kama angetaka watu wamwombee msamaha, angeandika memo kwa Duni, au Rais mwenyewe kwa ajili ya kukiri kosa na kuomba msamaha.
mbona Mnyika kila siku anamwambia DPP aifute kesi ? Kwani hafahamu kuwa kesi ikiwa mahakamani wakuimaliza ni jaji?
 
Back
Top Bottom