Mukulu wa Bakulu
JF-Expert Member
- Aug 12, 2014
- 4,051
- 12,954
Watanzania wengi ni watu wenye uelewa mdogo sana wa mambo. Kwa kutumia mwanya huo ndio maana CCM inaendelea kutawala nchi hii wanavyotaka.
Unashangaa watu wengi wanamsifia sana Kikwete na kumuona mtu wa aina yake na aliefanya mambo makubwa nchi hii lakini ukweli ni kwamba Kikwete kaliingiza hili taifa kwenye matatizo makubwa kuliko mazuri machache aliyoyafanya.
1. Kikwete ndio sababu nchi hii haina katiba mpya. Kumbuka alianzisha mchakato wa katiba mpya kinafiki halafu siku ya ufunguzi wa bunge la katiba akaponda maoni yaliyotolewa na wananchi kwa maslahi ya chama chake.
Hili tu lilipasa kufuta jambo zuri lolote alilolifanya Kikwete nchi hii. Watu wanalalamika Kwamba Magufuli alikua mbaya, kama tungepata katiba mpya labda Magufuli alingechaguliwa ama asingeongoza nchi anavyotaka.
2. Kikwete ndio alikuwa anasaini mikataba ya hovyo kama Dowans, Symbion nk ambayo haina exit clause. Nasikia hao jamaa wamelipwa zaidi ya Bilioni 500 za walipakodi masikini wa nchi hii.
4. Leo namuona Kikwete kama kiongozi wa waangalizi wa uchaguzi wa Afrika Mashariki huko Kenya anashauri ambae hatakubaliana na matokeo aende mahakamani huku yeye alishindwa kututengenezea hayo mazingira kwa maslahi ya chama chake.
Binafsi sioni kwa nini Kikwete anasifiwa, hastahili hata chembe ya sifa moja.
Unashangaa watu wengi wanamsifia sana Kikwete na kumuona mtu wa aina yake na aliefanya mambo makubwa nchi hii lakini ukweli ni kwamba Kikwete kaliingiza hili taifa kwenye matatizo makubwa kuliko mazuri machache aliyoyafanya.
1. Kikwete ndio sababu nchi hii haina katiba mpya. Kumbuka alianzisha mchakato wa katiba mpya kinafiki halafu siku ya ufunguzi wa bunge la katiba akaponda maoni yaliyotolewa na wananchi kwa maslahi ya chama chake.
Hili tu lilipasa kufuta jambo zuri lolote alilolifanya Kikwete nchi hii. Watu wanalalamika Kwamba Magufuli alikua mbaya, kama tungepata katiba mpya labda Magufuli alingechaguliwa ama asingeongoza nchi anavyotaka.
2. Kikwete ndio alikuwa anasaini mikataba ya hovyo kama Dowans, Symbion nk ambayo haina exit clause. Nasikia hao jamaa wamelipwa zaidi ya Bilioni 500 za walipakodi masikini wa nchi hii.
4. Leo namuona Kikwete kama kiongozi wa waangalizi wa uchaguzi wa Afrika Mashariki huko Kenya anashauri ambae hatakubaliana na matokeo aende mahakamani huku yeye alishindwa kututengenezea hayo mazingira kwa maslahi ya chama chake.
Binafsi sioni kwa nini Kikwete anasifiwa, hastahili hata chembe ya sifa moja.