Mzee Kikwete anasifiwa kwa jambo lipi hasa la maana alilofanya nchi hii?

Mzee Kikwete anasifiwa kwa jambo lipi hasa la maana alilofanya nchi hii?

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2014
Posts
4,051
Reaction score
12,954
Watanzania wengi ni watu wenye uelewa mdogo sana wa mambo. Kwa kutumia mwanya huo ndio maana CCM inaendelea kutawala nchi hii wanavyotaka.

Unashangaa watu wengi wanamsifia sana Kikwete na kumuona mtu wa aina yake na aliefanya mambo makubwa nchi hii lakini ukweli ni kwamba Kikwete kaliingiza hili taifa kwenye matatizo makubwa kuliko mazuri machache aliyoyafanya.

1. Kikwete ndio sababu nchi hii haina katiba mpya. Kumbuka alianzisha mchakato wa katiba mpya kinafiki halafu siku ya ufunguzi wa bunge la katiba akaponda maoni yaliyotolewa na wananchi kwa maslahi ya chama chake.

Hili tu lilipasa kufuta jambo zuri lolote alilolifanya Kikwete nchi hii. Watu wanalalamika Kwamba Magufuli alikua mbaya, kama tungepata katiba mpya labda Magufuli alingechaguliwa ama asingeongoza nchi anavyotaka.

2. Kikwete ndio alikuwa anasaini mikataba ya hovyo kama Dowans, Symbion nk ambayo haina exit clause. Nasikia hao jamaa wamelipwa zaidi ya Bilioni 500 za walipakodi masikini wa nchi hii.

4. Leo namuona Kikwete kama kiongozi wa waangalizi wa uchaguzi wa Afrika Mashariki huko Kenya anashauri ambae hatakubaliana na matokeo aende mahakamani huku yeye alishindwa kututengenezea hayo mazingira kwa maslahi ya chama chake.

Binafsi sioni kwa nini Kikwete anasifiwa, hastahili hata chembe ya sifa moja.
 
Kikwete peke yake ndio kawafanya wapumbavu mkashindwa kupata katiba mpya?? Ukiona nchi haijapata katiba mpya ujue watu wake ni wapumbavu kupita kiasi. Kikwete alikuwa mwanachama wa CCM na alichokifanya ni takwa la CCM na sio yeye kama Rais.

Ukiniuliza mimi nitakwambia tatizo ni nyinyi wananchi ukiwepo wewe hapo, siku mkiwa na akili timamu mtapata mnachokitaka.

Kama wanaume kibao walifyata kwa MTU mmoja miaka 6 na hata leo bado wamebambikiwa wabunge bila ridhaa yao halafu uje utuambie Kikwete mbaya wakati wabaya ni nyinyi? Kikwete alikosa nini mpaka aitake katiba mpya? Nyinyi wananchi ndio punguani wahed kabisa.

Watu wamevuruga uchaguzi akiwemo Kikwete bado mkakenua na mnkimbilia makanisani na misikitini kumsumbua Mungu wakati hilo lipo kwenye uwezo wenu, ona sasa Bunge lenu tukufu limejaa kusanyiko la wajinga na nyinyi bila aibu mnaliita Bunge.
 
SISYPHUS the King of Corinth, was once dubbed a smartest man in all of Greece.

He cheated the god of death Thanatos, and made fool of the gods of Olympus.

But like any other greedy ruler before him, he eventually ran out of tricks...

NB: Even our Sisyphus will run-out of tricks.......
 
Wewe ulitaka kikwete arekebishe makosa ya Nyerere na mkapa mbona Mkapa hakuleta hata wazo la katiba mpya, chuki chuki,
 
Utakufa na presha na inaonekana hujuwi hata maana ya katiba na katiba za wenzetu zikoje, kwani Rais wa marekani John F kenned alipokufa kwa kupigwa risasi Nani alichukua madaraka ya urais, Alipo kufa maiko satta Zambia Nani alimrithi, Alipokufa Rais wa Malawi Nani alimrithi, ulitaka Nani Apewe urais baada ya Hayati Magufuli kufariki,

Yaaani watu huku mitaani wanamkubali mh Rais Hadi wanatamani wawe wanamuona muda wote akizungumza halafu wewe unaleta chuki zako

Unamchukia mh Rais ambaye watu wengi Hadi upinzani wanamuunga mkono kwa namna anavyofanya kazi,

Huoni jitihada zake za kulijenga Taifa letu ili kila mwananchi afaidike na keki ya Taifa hili, huoni alivyo leta umoja na mshikamano hapa nchini

Unamlaumu mh Jakaya kikwete, Hivi mh kikwete ndiye aliyewatoa bungeni upinzani bunge la katiba, si walitoka wenyewe, unamchukia mtu aliyeshamilisha demokrasia hapa nchini, unamtukana mtu aliye fanya vyombo vya habari vikawa vinaandika habari bila mipaka bila bugudha

Acha chuki kwa mh Rais mstaafu, utaumiaa Sanaa moyo wako maana mh Kikwete utaendeleaa kumuona akiendelea kuaminiwa na jumuia za kimataifa
 
Utakufa na chuki zako binafsi na upumbavu wako..

Habari njema ni kwamba hakuna kitu utaweza badili zaidi ya kuumia hivyo hivyo...

Mwisho JK na Kinana ndio magwijinwa siasa za Tanzania na JK ni Mwanadiplomasia mashuruhi hapa Africa.
Kijana, jitahidi kujenga hoja, personal attacks hazina mashiko!
 
SISYPHUS the King of Corinth, was once dubbed a smartest man in all of Greece.
He cheated the god of death Thanatos, and made fool of the gods of Olympus..
But like any other greedy ruler before him, he eventually ran out of tricks...

NB: Even our Sisyphus will run-out of tricks.......
Mkuu hii comment una copy na ku paste

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Watanzania wengi ni watu wenye uelewa mdogo sana wa mambo. Kwa kutumia mwanya huo ndio maana CCM inaendelea kutawala nchi hii wanavyotaka...
Kwani mkuu Kikwete ndiye aliyeitunga katiba iliyopo mpaka sasa..? Mbili kikwete unamsakama eti haja fanya lolote. Mkuu upo serious kweli?

Hii nchi raisi aliye fanikiwa pakubwa katika utawala wake ni mzee kikwete. kipindi nipo chuo niliona hajafanya kitu ila baada ya kukaaa na kuwanyumbuisha sijaona anaemfikia hata kwa 50% kwa aliyo yatenda kimaendeleo katika hili taifa. Sema mzee wawatu hana ule umwamba flani.

Alitandaza lami zaidi ya awamu zote, miradi mingi unayoona inasemwa sijui sijui nini alianzisha yeye. Kwenye kampeni za 2020 nishangaa mgombea wa ccm anajinadi kwa miradi aliyofanya kikwete. Put some respect to our lovely president JK
 
Utakufa na presha na inaonekana hujuwi hata maana ya katiba na katiba za wenzetu zikoje, kwani Rais wa marekani John F kenned alipokufa kwa kupigwa risasi Nani alichukua madaraka ya urais...
Kaka umemjibu huyu mtu vzr saana. 👏🏻👏🏻👏🏻
 
Utakufa na chuki zako binafsi .

Habari njema ni kwamba hakuna kitu utaweza badili zaidi ya kuumia hivyo hivyo...

Mwisho JK na Kinana ndio magwijinwa siasa za Tanzania na JK ni Mwanadiplomasia mashuruhi hapa Africa.
Mjibu maswali yake.Ukimueleza kwamba atakufa kwa chuki au upumbavu kwa urahisi tu,haiwi!Wala hawi mpumbavu.
 
Utakufa na presha na inaonekana hujuwi hata maana ya katiba na katiba za wenzetu zikoje, kwani Rais wa marekani John F kenned alipokufa kwa kupigwa risasi Nani alichukua madaraka ya urais...
Hivi hapo amemtukana au kuonesha chuki kwa Kikwete? Yeye ameuliza maswali yanayomtatiza.Umpe majibu aridhike na siyo umjibu kwa maswali ambayo unamtwisha tena mzigo wa kusaka majibu.
 
Watanzania wengi ni watu wenye uelewa mdogo sana wa mambo. Kwa kutumia mwanya huo ndio maana CCM inaendelea kutawala nchi hii wanavyotaka...

Sijui ila nakumbuka katika utawala wake ndo walizaliwa magaidi wale wa kibiti na akashindwa kuwadhibiti had anatoka madarakan!

vituo vya polisi vilikua vinanyang’anywa silaha kila kukicha na kuuwawa!!

Mabilion ya hela za ufisadi!!
umeme ulikua kitendawili

Kifupi jamaa alileta usela nchi ikamshinda
nadhan angeendelea yale yalioko msumbiji ndyo yangekua kibiti na mtwara
 
Back
Top Bottom