Mzee Kikwete anasifiwa kwa jambo lipi hasa la maana alilofanya nchi hii?

Watanzania wengi ni watu wenye uelewa mdogo sana wa mambo. Kwa kutumia mwanya huo ndio maana CCM inaendelea kutawala nchi hii wanavyotaka...
Aliacha kajenga MOI ndugu zetu wengi wanapopata ajali za bodaboda na kuvunjika miguuni huenda pale kutibiwa.

Alituachia mradi wa mwendo kasi unaouhudumia jiji la Dar kwa sasa, JK hana siasa za mitandaoni za kujibizana na watu lakini kuna mengi sana aliyafanya.

JPM alijituma pia, lakini yapo mengi mabaya yanayokwenda sambamba na awamu ya tano. Mfano ni kule Arusha kuna ofisi moja ya serikali ilikuwa ikifanya siasa za enzi za Mwalimu Nyerere za kufuatilia ni kina nani wanaisema vibaya serikali.

Wanalipwa mishahara ya serikali ambayo ni kodi ya wananchi halafu wananyanyasa hao hao wananchi!. JK hakuwa akiyafanya hayo kwani hakuona faida ni ipi kwa watendaji wa serikali kuonea wananchi hao hao wanaolipa kodi na kuwezesha kuwepo kwa hizo mamlaka.
 
Hivi hapo amemtukana au kuonesha chuki kwa Kikwete?Yeye ameuliza maswali yanayomtatiza.Umpe majibu aridhike na siyo umjibu kwa maswali ambayo unamtwisha tena mzigo wa kusaka majibu.
Nimeshamjibu na kumpa majibu na bila Shaka ameyapata na ameridhika Sasa,
 
Kikwete ndio sababu nchi hii haina katiba mpya.
Yaani ka mtu kamoja tu! na mkakubali mka-mpa Kura....basi anastahili awaburuze! cha kufanya funga kopo lako hilo la gongo make umeamua kuturopokea tuu hapa...kwa nini hukumpinga au ulikuwa umeukalia???

nyie ndo mijoga mnajificha nyuma ya key board jitokeze paleeee useme km Wakurya! wao walizipiga kavukavu mpaka wakapewa jina Kanda Maalum!!!..... mpaka leo!! Kwenda Kenya Rukhsa! Biaashara Rhuksa!

UCHAGUZI HURU KOTEKOTE HKN WIZI MARA
 
Yapo MAZURI alifanya, upinzani ulishamiri , alisaidia kutatua Mgogoro wa KISIASA KENYA, pesa mtaani ilipatikana chafu na safi. nk,nk.

Bt sitomsahau Kwa haya;

1. Kuuvuruga mchakato wa KATIBA.

2. Kupromote wanawake ktk uongozi wake, Hadi akasaidia sa100 Jina lake kuchomekwa kiaina.

3. Nchi ikifika mahala ikawa ghala la kutunza na kusambaza mambo ya USINGIZI Kwa vijana. Walilala sana sana.

4. Gasi iliuzwa mara mbili Kwa WATEJA tofauti, na mikataba mibovu kibao, ufisadi ulitamalaki. Richmond nk.

5. Mikopo ya wanafunzi vyuo vikuu iliongezeka, degree zilijaa mtaani, bila kisahau vyeti feki.

6. Mabomu yalilipuka mbagala na yalijirudia tena.

7. Awamu yake ya pili, chama kilichukiwa kiasi kwamba viongozi waliogopa kuvaa sare za Chama Kwa kuhofia kuzomewa .

8. Udhaifu wa Serikali yake ulilazimika watuletee Dictator. Ni Yeye!!!!

Tunashukuru Kwa muda wake. Aje tu DICTATOR mwingine, maana Awamu ya 4 na 6 ni kama zinafanana.
Ameeen.
 
Muacheni bhana mtu azeeke kwa amani .
Mnamusema muzee wawatu ish muacheni kama amewaeza shauri zenu na nyie muwezeni .
Watu wengine mnakera saa zote kazi kuandama watu kwani alipokuwa raisi alikuusu nini??
Raisi hakunyimi kula bidii yako ndio matunda yako.
 
Hatuna Cha kumfanya, tunamsema tu, Kwa MAZURI na mabaya maana ni mtu Kwa upande mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…