Pre GE2025 Mzee Kikwete asikitishwa na Migogoro ya Uchaguzi adai aliyeshinda hatangazwi aliyeshindwa anatangazwa

Pre GE2025 Mzee Kikwete asikitishwa na Migogoro ya Uchaguzi adai aliyeshinda hatangazwi aliyeshindwa anatangazwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ameyasema hayo kwenye kongamano la viongozi wa Africa katika kuadhimisha miaka 20 ya Kamisheni ya Amani ya AU Mjini Dar es Salaam, Tanzania.

Sitaki kuongeza maneno, mwenyewe huyu hapa

Screenshot_2024-05-25-16-32-50-1.png
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema miongoni mwa sababu za kuwepo kwa migogoro kwa nchi za Afrika ni kutozingatiwa kwa miongozo ya uwepo wa uchaguzi ulio huru na wa haki.

Kikwete ameyasema hayo leo Mei 25, 2024 jijini Dar es Salaam katika mjadala uliokuwa sehemu ya mkutano wa maadhimisho ya miaka 20 ya Baraza la Aamani na Usalama la Umoja wa Afrika (PSC).

Amesema migogoro mingi ya ndani ya nchi za Afrika inahusiana na upungufu wa kiutawala.

“Inaweza kuwa demokrasia, ambapo inafikia watu wanakosa imani na demokrasia, kunakuwa na chaguzi ambazo hazijaratibiwa vizuri.”

“Aliyeshinda hatangazwi na aliyeshindwa anatangazwa kuwa mshindi. Yote ni kwa sababu ni upungufu wa kiongozi, kukosekana usawa, ubaguzi, ukabila na upendeleo,” amesema Kikwete.

Amesema watu wanapokosa haki zao huamua kuzipambania na ndipo inapozuka migogoro.

Mwananchi

Toa maoni yako
 
Ameyasema hayo kwenye kongamano la viongozi wa Africa katika kuadhimisha miaka 20 ya Kamisheni ya Amani ya AU Mjini Dar es Salaam, Tanzania.

Sitaki kuongeza maneno, mwenyewe huyu hapa

View attachment 2999185View attachment 2999187

Toa maoni yako
Teh teh 😃 😃 hii michezo imefanyika Sana hapo Zanzibar miaka yote, hata mwaka. 2015 wakati anaachia madaraka lilitokea hilo....ila alibakia kimya tu, Sasa ndio busara zimerejea.
 
Teh teh 😃 😃 hii michezo imefanyika Sana hapo Zanzibar miaka yote, hata mwaka. 2015 wakati anaachia madaraka lilitokea hilo....ila alibakia kimya tu, Sasa ndio busara zimerejea.
Inashangaza sana!
 
Yupo Kailima na Dr Mahera, sasa hatujui wanamwakilisha nani

Mahera atabakia kuwa mfalme wa mashetani yote kwenye chaguzi. Lagacy yake katika ushetani wa kuharibu ucjaguzi, sijui kama kuna binadamu ataweza kuivunja.

Huyu mtu angekuwa hata utashi mdogo sana, asingekuwa anajitokeza kwenye tukio lolote linalohusu demokrasia. Huyu siyo mwumini wa demokrasia kabisa.
 
Back
Top Bottom