Pre GE2025 Mzee Kikwete asikitishwa na Migogoro ya Uchaguzi adai aliyeshinda hatangazwi aliyeshindwa anatangazwa

Pre GE2025 Mzee Kikwete asikitishwa na Migogoro ya Uchaguzi adai aliyeshinda hatangazwi aliyeshindwa anatangazwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Jakaya Mrisho Kikwete, kama raia (ukiondoa urais na vyeo vingine alivyopitia), ni mtu muungwana, msikivu na mwenye mawazo huru.
Hata hivyo, kiongozi bila watu ni kama mamba nje ya maji (nguvu ya mamba kwenye maji na ya kiongozi kwa watu wanaomshabikia na kumlinda).
Katika kundi la binadamu, kuna tofauti kifikra (wapo wenye fikra za kinyama kama mbwa na wengine wenye utu), na wote hao huwazunguka viongozi na hutumika, kila mmoja kwa umuhimu na nafasi yake.
Changamoto kubwa hutokea pale ambapo nafasi zinazohitaji watu wenye utu hupewa wenye unyama.
Mpangilio usipokuwa mzuri, kiongozi aweza kuzidiwa nguvu, hata kama ana nia nzuri. Vivyo hivyo kiongozi muovu aweza kupatikana.
Kikwete ana la kujitetea. Aliharibu mchakato wa katiba mpya kwa hotuba yake ya upande mmoja kwenye bunge la katika. Yeye angewaachia wajumbe waamue na sio kuonesha msimamo wake. Pia kitendo chake Cha kutuma jeshi Zanzibar kwenye uchaguzi wa 2015 ilikuwa ujinga wa Hali ya juu. Vuai na CCM yake walikuwa wameitisha conference na kupinga matokeo ya kushindwa, ghafla jeshi likaongezwa Zanzibar na Jecha akazungukwa na wanajeshi na kushindwa kumtangaza Maalim Seif kuwa Rais. Mwisho wa siku wakatafuta sababu za kijinga eti wajumbe hawaelewani na maalim kajitangaza mapema.
 
Ni kipindi cha JK ndipo tumeshuhudia idadi kubwa ya wabunge wa upinzani bungeni (Kambi imara ya Upinzani)........kwenye hili hongera, kwa kiasi kikubwa JK ni mwanademokrasia

japo kwa Zanzibar ilikuwa tofauti labda kwa kuwa miaka nenda rudi Zanzibar ni koloni la Tanganyika uchaguzi wa 2015 angetangazwa alieshinda Maalim Seif ingeleta shida kwenye issue ya muungano
 
Wapi kasema uongo? Yeye alikuwa Rais wa nchi kwa miaka 10 mfululizo kwahiyo anajua yote haya aidha alipokuwa mamlakani ama hata baada ya kutoka maana ana vyanzo vingi na vya kuaminika vya kumpa taarifa.
Ni mnafiki tu. Katuma jeshi Zanzibar 2015 kuzuia Maalim asitangazwe. Na kweli hakutangzwa.
 
Ni kipindi cha JK ndipo tumeshuhudia idadi kubwa ya wabunge wa upinzani bungeni (Kambi imara ya Upinzani)........kwenye hili hongera, kwa kiasi kikubwa JK ni mwanademokrasia

japo kwa Zanzibar ilikuwa tofauti labda kwa kuwa miaka nenda rudi Zanzibar ni koloni la Tanganyika uchaguzi wa 2015 angetangazwa alieshinda Maalim Seif ingeleta shida kwenye issue ya muungano
Kwanini iwe shida?. Ule ulikuwa uhuni.
 
Kikwete alivyo mnafiki ataandika kitabu akiomba Radhi kuzuia Maalim Seif Kutangazwa Rais wa Zanzibar 2015.
 
Ameyasema hayo kwenye kongamano la viongozi wa Africa katika kuadhimisha miaka 20 ya Kamisheni ya Amani ya AU Mjini Dar es Salaam, Tanzania.

Sitaki kuongeza maneno, mwenyewe huyu hapa

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema miongoni mwa sababu za kuwepo kwa migogoro kwa nchi za Afrika ni kutozingatiwa kwa miongozo ya uwepo wa uchaguzi ulio huru na wa haki.

Kikwete ameyasema hayo leo Mei 25, 2024 jijini Dar es Salaam katika mjadala uliokuwa sehemu ya mkutano wa maadhimisho ya miaka 20 ya Baraza la Aamani na Usalama la Umoja wa Afrika (PSC).

Amesema migogoro mingi ya ndani ya nchi za Afrika inahusiana na upungufu wa kiutawala.

“Inaweza kuwa demokrasia, ambapo inafikia watu wanakosa imani na demokrasia, kunakuwa na chaguzi ambazo hazijaratibiwa vizuri.”

“Aliyeshinda hatangazwi na aliyeshindwa anatangazwa kuwa mshindi. Yote ni kwa sababu ni upungufu wa kiongozi, kukosekana usawa, ubaguzi, ukabila na upendeleo,” amesema Kikwete.

Amesema watu wanapokosa haki zao huamua kuzipambania na ndipo inapozuka migogoro.

Mwananchi

Toa maoni yako
HUYU NINACHOCHUKIA NI KUWA NI MNAFIQ NA HANA AIBU KABISA.YAANI UNAFIQ UPO DAMUNI.NI SEHEMU YA MAISHA YAKE
 
Kosa lake lipi hapo kwa kauli hiyo hadi mumtukane?
Jamani jifunzeni kutafakari kilichosemwa siyo chuki dhidi ya mtu.
Huu ni nwanzo mzuri hata kana huko nyuma hakuyazingatia hayo.
Kikwete ni sehemu ya mifano hai ya chaguzi za kishenzi hapa barani Africa. Kama anachokisema anamaanisha angekuwa anajitokeza kutaka tume huru ya uchaguzi dhidi ya chama chake. Kinyume na hapo ni kutaka sifa zisizo na tija kwa kufurahisha genge.

Mikutano ya aina hiyo huwa naiona haina tija, maana watu hushiriki kuongea mambo wasiyoyatekelaza Wala kuyaamini.
 
Huyu Mzee ni snitch ndio maana aliwahi kukimbia kule Monduli kwenye chuo Cha kijeshi sababu ya unafiki.
Huyu angalau alijitahidi tulikuwa na bunge imara lenye kuibua hoja nzito. Katika miaka yake kumi zaidi ya asilimia 60 ya watumishi wa umma wa sasa waliajiriwa. Ukimuona mtoto wa maskini ameajiriwa serikalini basi wengi wao ni kipindi chake.
 
Kikwete ana la kujitetea. Aliharibu mchakato wa katiba mpya kwa hotuba yake ya upande mmoja kwenye bunge la katika. Yeye angewaachia wajumbe waamue na sio kuonesha msimamo wake. Pia kitendo chake Cha kutuma jeshi Zanzibar kwenye uchaguzi wa 2015 ilikuwa ujinga wa Hali ya juu. Vuai na CCM yake walikuwa wameitisha conference na kupinga matokeo ya kushindwa, ghafla jeshi likaongezwa Zanzibar na Jecha akazungukwa na wanajeshi na kushindwa kumtangaza Maalim Seif kuwa Rais. Mwisho wa siku wakatafuta sababu za kijinga eti wajumbe hawaelewani na maalim kajitangaza mapema.
Rais bila watu hakalii kiti hata kwa siku moja, atafurushwa tu.
Rais hutegemea kundi lililomzunguka na kumlinda (likiwa ovu, uovu utatamalaki na kinyume chake ni sawa).
Kwa hiyo, ni muhimu kujenga watu, jamii na taifa katika maadili kuanzia watoto badala ya kusubiri kutegemea mtu mmoja ambaye aweza kugeukwa na kufukuzwa na waovu wakiwa wengi.
Zipo (atake asitake za kimya kimya nyingi kuliko za wazi kama enzi za Magufuli) na Viongozi hukubaliana nazo vivyo hivyo kulingana na zilivyokuja.
 
Tusimubeze anao ushahidi, ameshiriki hili, walio nyanganywa ushindi wengine walikuwa marafiki zake, amewazika, watamzika waliobaki hai kama atawatangulia. Ni ujumbe kwa wasimamia uchaguzi wa leo/kesho kujisahihisha. Wezi wa jana kukemea wezi wa leo/kesho siyo vibaya.
 
Kikwete ana la kujitetea. Aliharibu mchakato wa katiba mpya kwa hotuba yake ya upande mmoja kwenye bunge la katika. Yeye angewaachia wajumbe waamue na sio kuonesha msimamo wake. Pia kitendo chake Cha kutuma jeshi Zanzibar kwenye uchaguzi wa 2015 ilikuwa ujinga wa Hali ya juu. Vuai na CCM yake walikuwa wameitisha conference na kupinga matokeo ya kushindwa, ghafla jeshi likaongezwa Zanzibar na Jecha akazungukwa na wanajeshi na kushindwa kumtangaza Maalim Seif kuwa Rais. Mwisho wa siku wakatafuta sababu za kijinga eti wajumbe hawaelewani na maalim kajitangaza mapema.
Aiseeee
 
Tusimubeze anao ushahidi, ameshiriki hili, walio nyanganywa ushindi wengine walikuwa marafiki zake, amewazika, watamzika waliobaki hai kama atawatangulia. Ni ujumbe kwa wasimamia uchaguzi wa leo/kesho kujisahihisha. Wezi wa jana kukemea wezi wa leo/kesho siyo vibaya.
😆😆😆😆😆
 
Ameyasema hayo kwenye kongamano la viongozi wa Africa katika kuadhimisha miaka 20 ya Kamisheni ya Amani ya AU Mjini Dar es Salaam, Tanzania.

Sitaki kuongeza maneno, mwenyewe huyu hapa

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema miongoni mwa sababu za kuwepo kwa migogoro kwa nchi za Afrika ni kutozingatiwa kwa miongozo ya uwepo wa uchaguzi ulio huru na wa haki.

Kikwete ameyasema hayo leo Mei 25, 2024 jijini Dar es Salaam katika mjadala uliokuwa sehemu ya mkutano wa maadhimisho ya miaka 20 ya Baraza la Aamani na Usalama la Umoja wa Afrika (PSC).

Amesema migogoro mingi ya ndani ya nchi za Afrika inahusiana na upungufu wa kiutawala.

“Inaweza kuwa demokrasia, ambapo inafikia watu wanakosa imani na demokrasia, kunakuwa na chaguzi ambazo hazijaratibiwa vizuri.”

“Aliyeshinda hatangazwi na aliyeshindwa anatangazwa kuwa mshindi. Yote ni kwa sababu ni upungufu wa kiongozi, kukosekana usawa, ubaguzi, ukabila na upendeleo,” amesema Kikwete.

Amesema watu wanapokosa haki zao huamua kuzipambania na ndipo inapozuka migogoro.

Mwananchi

Toa maoni yako
Kwahiyo we mzee ndio unataka umuunge mkono mkojani ili akishindwa atangazwe mpinzani wake au!!?
 
Back
Top Bottom