Mzee Kikwete aweka rekodi sawa, Uchumi wa Kati waliopanga na Mkapa ni wastani wa dola 3,000 kila Mtanzania

Yani ulitaka barabara zisiwe na matuta?
Na kwamba hicho ndio kipimo cha ukilaza?
Mkuu Kuna nchi nyingine hapa duniani unaijua ambayo barabara zake zimejaa matuta Kama Tanzania?
 
Ungeangalia ile hotuba ya Dr. Mpango wakati anatoa hii habari ya kuingia uchumi wa kati ungejua sisi tunasema nini. Sasa kwa kuwa umekaa kusifia kuabudu kusujudu kutamka neno juhudi kama dozi ya TB basi na akili yako umeiweka mfukoni unatembea nayo!
Dr. Mpango alisema walipanga kufikia uchumi wa kati by 2025.

Kikwete anasema Mkapa aliweka lengo kwamba hadi kufikia 2025 tutangazwe uchumi wa kati tukiwa na dola elf 3 kama pato kwa kila mtanzania

Bank ya dunia imeitangaza tanznia kama nchi ya uchumi wa kati kabla ya 2025 kwa kutumia vigezo vyao.

Malengo ya kufikia pato la dola elf 3 kwa kila mwananchi bado yako pale pale na hakuna kiongozi yeyote wa selikali alishawahi kusema tumeshafikia lengo waliweka la pato la dola elf 3 kama yupo weka crip yake hapa.
 
Anajitapa kutufikisha uchumi wa kati kabla ya muda,yaani kabla ya 2025
Uchumi wa kati anatangaza Magufuli au bank ya dunia?

Kama wao walipanga kufikia uchumi wa kati kwa vigezo vya WB lakini wametangazwa kabla ya 2025 kwanini asijisifu?
 
Uchumi wa kati anatangaza Magufuli au bank ya dunia?

Kama wao walipanga kufikia uchumi wa kati kwa vigezo vya WB lakini wametangazwa kabla ya 2025 kwanini asijisifu?
Mimi nimesema ametangaza au anajitapa? Au kiswahili hujui mkuu?
 
Sio Magufuli aliyesema tuko uchumi wa kati ni World Bank, so kawaulize hao ndio mtajua
 
Mkuu Kuna nchi nyingine hapa duniani unaijua ambayo barabara zake zimejaa matuta Kama Tanzania?
Unajua lengo la kuweka matuta kwa nchi kama tanzania hasa ni nini?
 
Kwani hatujafikia uchumi wa kati kwamba anaongopa?
Hiyo haikuwa target yetu mkuu and our indicator for that is USD 3000 by 2025 unless Kama anatekeleza plan na target zilizopo kichwani mwake
 
Unajua lengo la kuweka matuta kwa nchi kama tanzania hasa ni nini?
Watu ni vilaza,madereva can not observe roads signs na wafuka kwa miguu nao ni hivyo hivyo.so matuta ndo yanatusaidia kusimamia sheria kwa sababu sisi hatuwezi sababu ya ukilaza wetu
 
Acha ramli chonganishi rais Magufuli alielezea vizuri tangu siku anarudisha form ya urais kuwa kazi ya kuipeleka nchi uchumi wa kati ilianzishwa na wa tangulizi wake. Kwenye timu ya mpira sifa anapewa mfungaji bora anayepokea pasi ya mwisho.
Nilishaandika humu mara nyingi TATIZO SIO JPM BALI NI YALE MAFISI YALIYOMZUNGUKA NA "MASHANGILIZI". Ndio hayo hupotosha na kumpa Mkuu uongo ili maslahi yao yatimie kisha hujifanya wao ndio wazalendo kuliko watanzania wengine. Inaposemwa kinyume na mapenzi yao ndipo utasikia "wasaliti... wanatumiwa na mabeberu!" Ilhali wao ndio wameifikisha nchi hapa tulipo.
 
Viwango vya uchumi wa kati wa chini na juu vimewekwa na WB. Sasa kuna watu kweli na akili zao timamu walikuwa hawafahamu hili? Leo ndio wamefahamu kwamba JK na BWM ndio walipanga?

''The World Bank classifies the world's economies into four income groups — high, upper-middle, lower-middle, and low. We base this assignment on Gross National Income (GNI) per capita (current US$) calculated using the Atlas method.''

''(MIC) According to the World Bank, middle-income countries (MICs) are defined as economies with a Gross National Income (GNI) per capita between $1,026 and $12,475. MICs are one of the income categories that the World Bank uses to classify economies for operational and analytical purposes.''

Haya majungu sijui yataisha lini, Watanzania tuwe macho na wapotoshaji.
 
Wewe ndio huelewi na hii yote inasababishwa na hasira ulizonazo kwa Magufuli personal

Hakuna mahala popote Magufuli aliwahi kusema wameshafikia malengo yao ya dola elf 3 kabla ya 2025

Alichosema yeye ni furaha aliyonayo WB kuwatangaza uchumi wa kati kabla ya 2025 waliyoikadiria wao.

Hiyo ya lengo la dola elfu 3 bado liko palepale na Jk alimwambia Magufuli ajitahidi hadi 2025 aifikie ili kumuemzi Mkapa.
Sasa hapo usichoelewa ni nini?
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]eti bonge la snitch
 
Watu ni vilaza,madereva can not observe roads signs na wafuka kwa miguu nao ni hivyo hivyo.so matuta ndo yanatusaidia kusimamia sheria kwa sababu sisi hatuwezi sababu ya ukilaza wetu
Sasa hapo kilaza nikiongozi wako au ni wewe usieelewa alama za barabarani unaenda tu kama nyumbu mpka kiongozi wako anaamua kukuwekea alama mbadala?
 
Sasa hapo kilaza nikiongozi wako au ni wewe usieelewa alama za barabarani unaenda tu kama nyumbu mpka kiongozi wako anaamua kukuwekea alama mbadala?
Kilaza ni yule aliyefikia uamuzi wa kutumia matuta kusimamia sheria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…