Mzee Kikwete aweka rekodi sawa, Uchumi wa Kati waliopanga na Mkapa ni wastani wa dola 3,000 kila Mtanzania

Hujanielewa au ni ushabiki tu?
Tazama capital aliyoikuta mwenzio na alipoifikisha kisha linganisha na ulipoikuta wewe na ulipoifikisha halafu udraw conclusion.
 
Hata wewe umekumbwa na upepo wa kichadena tayari!

Magufuli akishangilia taarifa WB hakusema kwamba tayari wameshafikia dola elf 3 kabla ya 2025
Hayo ni mawazo yangu,jitahid kuwaheshim ambao wanatofautiana na wew itakuongezea muda wa kuishi
 

Give us a break!! Internationa figure ya kwenda kubembea Jamaica ukitumia kodi za nchi maskini, Rais mzima? Ama zile fedha za kugharamikia kubembea na kupiga picha na bozi tu meni zilipatikana kupitia misaada ya diplomasia ya bakuli la kuombaomba?
 
Fanya hesabu hii halafu utasema kama wewe ni kiazi au la:
54 - 30 =
Halafu linganisha na
64 - 54 =

Ukipata majibu na maana yake ,,, jiite jina linalokupendeza moyoni mwako.
Ipo kazi, na hamuwezi patana, kila mtu anazungumza chake bila kujua, wote wanafikiri mnazungumza kitu kimoja.
 
Hujanielewa au ni ushabiki tu?
Tazama capital aliyoikuta mwenzio na alipoifikisha kisha linganisha na ulipoikuta wewe na ulipoifikisha halafu udraw conclusion.
Mimi nimekuelewa wewe ndio ujaelewa ndio maana nika kwambia mtazamo wako ni simple.

Ni hivi inafikia sehemu ili size ya uchumi ukue serikali inabidi ifanye investment zingine kubwa kwanza.

Kwa maana hiyo kuitoa nchi kutoka size ya 32.5 mpaka 50 billion na ikashuka maana JK kaicha kwenye 45 billion Magufuli ndio akaurudisha tena kwenye 50 billlion na kuendelea. Kwenda mbele inabidi ufanye investments zingine.

Ungekuwa umesoma au kujisomea uchumi ungeelewa kuna dhana wanaita ‘Production Possibility Frontier’ you can only produce certain output given the resources. Kwa ivyo ili kukuwa zaidi inabidi ufanye investment za infrastructure, elimu, afya etc sehemu nyingine ili kuvutia uwekezaji ndio output size ya uchumi ikue. Hizo efforts zinakuwa hazipo reflected kwenye size ya uchumi.

Ndio maana nakwambia mtazamo wako simple huna tofauti na huyu jamaa 👇

 
Wewe ndiyo mpumbav kikwete alitupatia nafasi ya kumjua yey Ni Nani ndiyo maana tukagundua Ni fisadi
 
Ha ha ha nimekuelewa ,Tatizo la watanzania wengi ni elimu,maarifa ,maarifa maarifa

Wangejua ...tungekua mbali sana
 
Hawezi! Hata kufanikisha ifike USD 1200 hatoweza kutokana na kukuru kakara zake!
Huyu jamaa hata chemistry sijui alikua anafanyaje

He is not smart...kila kitu anatumia nguvu

Mkapa analysts wanasisitiza alijenga taasisi (economic structures),angekua anatumia akili angepata ujumbe hapo wakati anafikiria kununua midege na ujenzi huku per capital income ikiwa ndogo
 
Poleni bana.
 
Wakati Tanzania tuna vivutio vya utalii, madini, ardhi nzuri ya kilimo, maji ya moyo na ziwa kwa uvuvi na umwagiliaji.
Mimi nasubiri jpm astaafu mje kumsifu tena.

Unajua tatizo lenu ni moja tu,huwa mnachelewa kuona ila huwa ni lazima muone[emoji16][emoji16]
 
Hii singo imeshachuja long time kitambo. Tungeni nyingine ya kuhadaa wananchi ila mjue kitaani hali ni ngumu
 
Tunavyodanganyana hivyo... eti hazina palikuwa pamekauka!! Kama hazina palikuwa pamekauka, unataka kusema wafanyakazi walikuwa hawalipwi mishahara?!

Kama hazina palikuwa pamekauka, unataka kusema wanafunzi vyuo vikuu walikuwa hawapati mikopo na grants zingine?

Kama hazina palikuwa pamekauka, unataka kusema shughuli za serikali zilisimama?

All in all, wakati nafahamu Wafuasi wa JPM hamna utamaduni wa kutafuta taarifa wenyewe na ndio maana inakuwa rahisi kudanganywa, ningekushauri spend few minutes na ku-Google the following Keyword " BOT Economic Overview 2015/2016" ambako utapata BoT's Annual Report, na sehemu ya ripoti inasema:-


Sasa how come unadai Hazina ilikauka wakati as of June 30, 2015 kulikuwa na Foreign Reserve ya USD 4.402 Million wakati hiyo ni zaidi ya TSh. TRILLION 9?! Yaani Hazina yenye zaidi ya shilingi Trilioni 9 ndo ilikuwa imekauka?!

Na wakati unadai JK kaacha hazina pamekauka wakati alikuta PAMEJAA, Global Economy wanatueleza Mkapa aliacha nini pale Hazina:-


Kama ulisoma Statistics na Histogram angalau O-Level, utaona hapo wanaonesha 2005 ambayo Mkapa kaondoka madarakani, aliacha reserve ya roughly USD 2 Billion!!!

Sasa how come unadai JK alikausha Hazina wakati alikuta IMEJAA, and at the same time, data zinaonesha JK alipandisha Hazina from roughly USD 2 Billion to USD 4.4 Billion?!

That's one, but second, what did you just say?! JPM ndie kaipaisha nchi kwenye uchumi wa kati?! Kaipaisha kutoka hatua ipi na yeye kaipaisha kwa kiasi kipi?!

Tuangalie huo Uchumi wa Kati ambao World Bank walitangaza takwimu zake, tunaona mtu ambae unadai aliacha Hazina ZERO, huku akiwekeza kwenye ANASA, alipandisha GNI per capita from USD 720 in 2010 hadi USD 980 in 2015... yaani ongezeko la USD 260!!



Lakini hadi ripoti inatolewa, mwezi July under JPM, ndo kwanza kwa muda wote huo JPM alikuwa ameitoa Tz from USD 980 to USD 1080... yaani ongezeko la USD 100 TU kwa muda wote aliokaa madarakani!!!

Na kwa kuangalia GNI Growth kuanzia kipindi cha Mkapa hadi sasa, World Bank wanakupa takwimu zao hapa chini:-



Sasa huo ubora wa JPM kumlilinganisha na waliomtangulia unaupima kwa kutumia vigezo gani wakati takwimu ndo hizo hapo zinaonesha kapandisha for only USD 100 kwa muda wote aliokaa madarakani?!

Kwa upande mwingine, unadai eti JPM kafufua mashirika ambayo yalikufa!!!!

Shirika gani kwa mfano?! Loss Making ATCL aliyoinunulia ndege za over TZS 1 Trillion, and later:-


Yaani ndo ufufuaji wa mashirika unaousema huu?! Yaani una-invest millions of dollars without a comprehensive business plan ndo unaita kafufua mashirika yaliyokua maututi wakati kaiingizia nchi hasara zisizo na maana, matokeo yake, anaamua kuihamishia Ofisi ya Rais ili CAG asitie mkono:-


Na taarifa hiyo inaendelea kusema kwamba:-
Yaani JPM katumia zaidi ya Sh Trillion 1 kununua ndege, na hadi habari hiyo inatolewa April 2019 shirika lilikuwa halijakaguliwa, na hapo hapo bado JPM anaomba more TZS 500 Billion, halafu unakuja hapa kudai eti "kafufua mashirika yaliyokuwa maututi"!

Kwanini Agency ambayo ndiyo mmiliki wa ndege za ATCL ameihamishia Ikulu?! Kwanini haijakaguliwa?!

Again unadai Magufuli kwenye miundombinu!! Miundombinu ipi wakati kama suala ni barabara nyingi ni za tangu awamu zilizopita, na hata alizozindua yeye kwa mara nyingine zilikuwa zimeanza kujengwa tangu awamu iliyopita?!

Flyovers ingawaje ni kitu kidogo sana lakini Wafuasi wa JPM mmekuwa mkitumia suala la flyover kama moja ya success ya JPM wakati ukweli ni kwamba, mpango wa Flyover ulianza way back in 2007 serikali walipoiomba Japan kujenga Flyover TAZARA na Ubungo!!

Baada ya hapo, Japan, kupitia JICA wakafanya pre-feasibility study kujiridhisha ikiwa kuna uhitaji wa Flyover lakini wakafikia conclusion kwamba, by the time ilikuwa inahitajika zaidi BRT lakini in the near future, from 2015, suala la Flyover litakuwa halikwepeki:-

From pre-feasilibility, zikaja feasibility studies nyingine, na hadi JK anaondoka madarakani, Serikali ya Japan tayari ikawa imeshatoa fedha za ujenzi, na JPM akaja tu kuifanya kazi anayoiweza zaidi:- UNYAPARA wa kusimamia ujenzi wa Flyovers!

Source: JICA

So, endeleeni kudanganyana wenyewe kwa wenyewe na habari zenu za kuokoteza vichochoroni, huku source zenu zingine, zikiwa ni wanasiasa wakati mnatembea na libraries mikononi mwenu!!!
 
Yeye mwenyewe kabemenda miundombinu yake mpaka basi halafu anajitetea upuuzi. Uchumi ni miundombinu na yeye miundombinu aliibemenda anategemea nini. Mipango siyo matumizi. Atuambie yeye alifanyaje kama si utapeli anafanya.
Two wrongs don't make it right.
Tapeli + tapeli = Matapeli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…