Mzee Kinana, chama kinachojali wanyonge na masikini kisingekubali tozo kama hizi. Hii sio CCM aliyoiasisi Mwl. Julius

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Kwamba hata mama aliye kijijini anakatawa tozo akitumiwa pesa na mwanae anayeishi mjini? Kwamba hata mwalimu wa shule anyefundisha kijijini kwenye mazingira magumu ya kijijini anakatwa kodi ya PAYE, na hata akitoa mshahara wake benki anakatwa kodi!

Mzee kinana CCM hii iko vipi? Ni mali ya wanyonge? Usawa na utu gani unauhubiri?

 
CCM ilikufa 5. 11. 1985
 
Bado mtu anaweza kuwa mtumwa ndani ya nchi yake
 
CCM ilikufa na Nyerere wake, sasa tu Chama la wapigaji binafsi wanaokula kwa urefu wa kamba zao
 
Karibu katika makala yangu kunipigia kura , Tanzania yenye sura mbili kwenye sura moja
 
Kuwakataa watu wa vipato vya chini na kukumbatia mabeberu kunaondoa dhana nzima ya alama ya jembe na nyundo kwenye bendera ya chama.

Yanayoendelea sasa ni usaliti dhidi ya raia wenye nchi yao.
 
Kuwakataa watu wa vipato vya chini na kukumbatia mabeberu kunaondoa dhana nzima ya alama ya jembe na nyundo kwenye bendera ya chama.

Yanayoendelea sasa ni usaliti dhidi ya raia wenye nchi yao.
Mkuu umeongea point muhimu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…