#COVID19 Mzee Makamba: Askofu Gwajima na Polepole hawavumiliki. Lazima wajue uhuru wao unaishia Bungeni

#COVID19 Mzee Makamba: Askofu Gwajima na Polepole hawavumiliki. Lazima wajue uhuru wao unaishia Bungeni

Huyu mzee naye anazeeka vibaya sana, kwa katiba ya nchi hii ilivyo, na wananchi wake walivyopiga usingizi wa Pono kuna mtu anaweza kumdharau Rais? Akiamua kumfinya mtu si anamfinya mara moja tu!! Hawa wazee wana umuhimu wao, ila kwa sasa wapumzike kwanza, TZ ya miaka ya 90s aliyoizoea yeye siyo TZ ya sasa!! Hao akina Polepole waachwe waongee, mwisho wa siku wenyewe watachoka na maisha yataendelea!! BTW, kila siku yanaibuka mambo mapya, ukizuia watu kuongelea chanjo leo kesho wataibuka watu wataongelea tozo, makato ya Luku, Ugaidi wa Mwamba, Katiba mpya, mikutano ya hadhara, dini kusajiliwa, teuzi mbovu n.k.! ukisema ujibu na kuyaweka moyoni hayo yote si utakufa na pressure kama mwendazake?? Acha watu waongee..
 
Mzee Makamba anasema Askofu Gwajima na Polepole hawavumiliki ndani ya CCM kwakuwa wamekuwa wamekuwa wakipingana na Serikali hasa kwenye swla hili la chanjo.

Mzee Makamba anasema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakimdharau sana Rais samia hivyo ametaka washughulikiwe mara moja.

Mzee Makamba anasema yeye si msemaji wa CCM lakini anashangaa ukimya wa baadhi ya Wana CCM na viongozi wa CCM hasa katika hali ya Rais kuonekana ana dharauliwa na baadhi ya wana CCM.

Mzee Makamba ametaka wana CCM kuwachukulia hatua Gwajima na Pole pole.. kwani hawavumiliki.

Chanzo: Magazeti
Wapeni KESI ya UGAIDI ndio MILA ZENU

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Mzee Makamba anasema Askofu Gwajima na Polepole hawavumiliki ndani ya CCM kwakuwa wamekuwa wamekuwa wakipingana na Serikali hasa kwenye swla hili la chanjo.

Mzee Makamba anasema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakimdharau sana Rais samia hivyo ametaka washughulikiwe mara moja.

Mzee Makamba anasema yeye si msemaji wa CCM lakini anashangaa ukimya wa baadhi ya Wana CCM na viongozi wa CCM hasa katika hali ya Rais kuonekana ana dharauliwa na baadhi ya wana CCM.

Mzee Makamba ametaka wana CCM kuwachukulia hatua Gwajima na Pole pole.. kwani hawavumiliki.

Chanzo: Magazeti
Kwaniniwachukuliwe hatua?!?! Serikalini imeshasema chanjo ni hiari Sasa tatizo liko wapi? Kama Kuna viongozi wanahamasisha chanjo ili watu wachanjwe Kuna ubaya gani Kama Kuna kundi la watu litasema chanjo ni hatari na kutoa sababu? Binafsi naipenda serikali lakini kwa hili la chanjo serikali imejichanganya mno...Kama Corona ipo na chanjo ipo kulikuwa hakuna sababu ya kusema chanjo ni hiari...je chanjo ya ndui ilikuwa ni hiari?! Je kwa chanjo zote zilizopita zilikuwa ni hiari kwa mtu kuchanjwa?
 
How come kukataa kuchanjwa mwili wangu iwe ni dharau kwa mwingine?!
Tatizo sio kukataa kuchanja ila tatizo ni wewe kukataa kuchanja halafu unaanza kudanganya na wananchi wasichanje hapo ndipo shida ilipo.
 
Mimi ninachojua chanjo ni hiari. Anayetetea kuchanja ana haki sawa na anayekataza watu wasichanje.

Hivyo, wote wapo sawa, wote haki zao ni sawa.
Hakuna anayesema chanjo ni lazima ila unapowalazimisha waumini wako waigomee unaondoa uhiari wa chanjo, unatakiwa uwaache waumini wako wajiamulie wenyewe bila kuwakataza.
 
Tatizo sio kukataa kuchanja ila tatizo ni wewe kukataa kuchanja halafu unaanza kudanganya na wananchi wasichanje hapo ndipo shida ilipo.
Kama kuna wanaohamasisha tuchanjwe lazima wawepo na wanaohamasisha tusichanje halafu sasa sie tuchague upande. It's natural. Mawazo kinzani hayapigwi rungu. Imagine kuna makanisa yanampinga Mungu na Yesu hata Muhammad, why chanjo isipingwe?!
Watanzania wana akili ya kuchagua upande sahihi.
 
Tuliona hivi hivi kwa Mzee Mwinyi alipokuwa anataka mwanae awe rais mzanzibari, mzee wa watu alijikomba komba sana kwa Magufuli.
 
Mzee Makamba anasema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakimdharau sana Rais samia hivyo ametaka washughulikiwe mara moja.
Sukuma GANG/ MATAGA hawataki kutawaliwa na mwanamke tena ni mzanzibar na ni muislamu.. wanamtazama Samia wanasema Hiiiiiii!!!!… 😄😄😄
 
Mzee Makamba anasema Askofu Gwajima na Polepole hawavumiliki ndani ya CCM kwakuwa wamekuwa wamekuwa wakipingana na Serikali hasa kwenye swala hili la chanjo.

Mzee Makamba anasema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakimdharau sana Rais samia hivyo ametaka washughulikiwe mara moja.

Mzee Makamba anasema yeye si msemaji wa CCM lakini anashangaa ukimya wa baadhi ya Wana CCM na viongozi wa CCM hasa katika hali ya Rais kuonekana ana dharauliwa na baadhi ya wana CCM.

Mzee Makamba ametaka wana CCM kuwachukulia hatua Gwajima na Pole pole.. kwani hawavumiliki.

=====

BAADHI ya viongozi waandamizi ndani ya chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, wanadaiwa kuwa na mkakati wa makusudi wa kumdharau Rais wa Taifa hilo, Samia Suluhu Hassan.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho, zinasema hatua ya viongozi wake wakuu, kunyamazia matendo ya Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima na mwenzake, Humphrey Polepole, inatafsiriwa ni dalili tosha kuwa “wanamdharau na kumpuuza,” Rais Samia.

Polepole, ambaye ni mbunge wa kuteuliwa na Rais na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, pamoja na Askofu Gwajima, wamekuwa na kampeni ya wazi ya kupinga chanjo ya corona, kinyume na maelekezo ya chama chao.

Kutokana na hayo, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Mzee Yusuf Makamba, Naibu Katibu Mkuu Bara wa NCCR-Mageuzi, Anthony Komu na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Profesa Edward Hoseah wamezungunzia kadhia hiyo na hatari wanayoiona ndani ya serikali na CCM.

Undani wake, soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Ijumaa tarehe 20 Agosti 2021.
Kuna haja ya kutenganisha kofia mbili
 
Mimi ninachojua chanjo ni hiari. Anayetetea kuchanja ana haki sawa na anayekataza watu wasichanje.

Hivyo, wote wapo sawa, wote haki zao ni sawa.
Sawa ni hiari lakini usitumie nafasi yako katika jamii kushawishi wengine wasichanje
 
Wasilazimishe watu suala la chanjo..dharau inatoka wapi? Watu wana uhuru wa kutoa maoni. Wana haki ya kuchagua what's injected into their bodies. Pole Pole na Gwajima wametoa maoni and its constitutional. Hili suala linaweza kuiumiza sana ccm wasipokuwa makini.

Those of us who are not vaccinated are choosing to stay that way because we are allowed to make that choice for ourselves. My body, my choice, am tired with this bs on social media trolling us to get experimental vaccine that is not even approved.

What studies have been done showing the long term effects?? No one has even had the vaccine that long to conduct that type of study...

..Tatizo la Askofu Gwajima ni madai yake kwamba viongozi wamehongwa, wamechomwa feki, na chanjo zina magnetic force / chip.

..Kama Askofu angepinga chanjo kwa hoja kwamba hazijafanyiwa majaribio ya kutosha kujua ubora, na madhara yake, hakuna ambaye angemlaumu.

..Askofu Gwajima angekuwa ni mwana Chadema na akatoa tuhuma alizotoa kuhusu chanjo leo angekuwa mahakamani akijibu mashtaka mabaya dhidi yake.
 
..Tatizo la Askofu Gwajima ni madai yake kwamba viongozi wamehongwa, wamechomwa feki, na chanjo zina magnetic force / chip.

..Kama Askofu angepinga chanjo kwa hoja kwamba hazijafanyiwa majaribio ya kutosha kujua ubora, na madhara yake, hakuna ambaye angemlaumu.

..Askofu Gwajima angekuwa ni mwana Chadema na akatoa tuhuma alizotoa kuhusu chanjo leo angekuwa mahakamani akijibu mashtaka mabaya dhidi yake.
Kama kuna jinai apambane na jinai yake. Ila drama za chanjo waachane nazo.
 
Back
Top Bottom