Mzee Makamba: Katika umri wangu wa miaka 84 leo ndio nayaona maji ya bomba Bumbuli, ahsante awamu ya 6

Katibu Mkuu wa CCM mstaafu analalamika, Wananchi wanalalamika,ni janga, vilio tu nchi mzima
 
Hawa wazee nongwa Sana. Wanafiki wakubwa na Mungu atawachapa viboko Hamsa! Wamekuwa kwenye madaraka from time immemorial, Leo ndiyo anaona Maji? Kulikuwa na ugumu gani kuamrisha maji yapelekwe huko? Asema mwanae awamu ya sita imemtambua na kumpa madaraka ya wizara Nyeti!
 
Mzee anapalilia mwanae asitumbuliwe! Aibu kwa familia yao iliyojimilikisha jimbo
 
Waafrika tunakuwa nyuma kimaendeleo kwa sababu hatujioni kama tumechelewa sana, 2022 hii ndio kwanza tunapongezana kwa kufanya jambo ambalo lilitakiwa kufanyika kitambo sana.
 
Nikadhani anasema leo ameona mabomba yanatoa asali Bumbuli kumbe ni maji tu, tena baada ya miaka 84! CCM imechoka sana.
Ni Rahisi sana kulaumu, Hili sio kosa la chama au serekali, bali ni tatizo kubwa la sie wananchi na haswa WAFRIKA, hatuna upendo wa Nchi au UMMA, bali tuna UMIMI sana. hata mie na wewe leo tukipewa Uwaziri cha kwanza tutafikiria tupore nini na kujitajirisha binafsi, ndugu na rafiki. shida ni fikra zetu, na tukisha ibaa tunasipeleka mali Ulaya ama Dubai kuzificha na kuwatajirisha wengine. Pesa inayofichwa kwenye mabenki ya njee zinatumika kuwaletea faida hayo mabenki na nchi zao.

Shica ya Maji ipo kila nchi za Kiafrika, Tena sasa TZ tuna Afadhali sana kuliko nchi nyingi, lakini hata hivyo bado sana. Kuna shida ya Afya, Maji, Lishe, Kazi n.k.....
 
Ina maana alishindwa hataa kuitumia nafasi yake ya ukatibu mkuu kufikisha huduma jimboni kwake?mpk anakuja kua babu?🤣
 
Wazee wajinga kama hawa, utadhani nchi ilikuwa chini ya CHADEMA mpaka 2021
 
Watawala wa Africa wengi wamelaani tupu
 
Alikuwa kiongozi miaka yote alishindwa nini kupeleka maji, shame upon him
 
Najua tunguli moja dogo ktk Ulimwengu wa ROHO ukubwa wake ni sawa na uwanja wa Mkapa,

Ndomana jini au pepo lenye ukubwa sawa na mlima Kilimanjaro linawekwa ktk Chupa linaenea, au likajipunguza USAWA wa Pete ukaiokota na kuivaa,

Pamoja na ukubwa huo ni haiwezekani kuwafunga watu zaidi ya 60 ml wasione, yaani watz wote warogwe?

Tupo MAGOTINI hawatafika 2025 wakiwa mawaziri, ni wote wanaohujumu wananchi.

Nawafutwe ktk Ulimwengu wa siasa wasahaulike kabisa. Amen
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…