Mzee Makamba: Katika umri wangu wa miaka 84 leo ndio nayaona maji ya bomba Bumbuli, ahsante awamu ya 6

Wengine walipokuwa wakisema kwa miaka 60 ya uhuru CCM imeshindwa kuwaletea wananchi maendeleo yakiwemo maji salama mliwaona wachochezi..
 
Hata hivo makamba Jr si alikuwa mbunge wa bumbuli alifanya nini sasa mbona anamwumbia kijana wake
Huyo mwanawe ni bogus kabisa na wala hana sifa ya kuwa Mbunge wa Bumbuli mara zote amekuwa akipita bila kupingwa Kwa kuwahonga pesa wapinzani wake dakika za majeruhi wajitoe,kumbuka alipiga B 2 za NSSF ndiyo zinampa jeuri
Huwa haonekani kabisa hapa jimboni hadi wakati wa uchaguzi.
 
Mbuge wa Jimbo alikuwa nani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katibu Mkuu wa CCM hukuliona hilo tatizo la maji? umekuja kuliona leo ukiwa na miaka 84?
 
mzee makamba chawa anaejua kunyonya damu
Mgosi huyu matata sana. Kwenye mtonyo hakai mbali. Kwa jk alisikika akisema "katika ufalme wako mzee usinisahau"; akaingia jpm akapiga " mtabatizwa kwa moto" akijua ni kina sisi tu hadi pale yalipo mkuta. Naona sasa katafuta pa kutokea kwa mama. Aina hii ya wazee hatufiki mbali kwani yeye la muhimu ni kufurahisha watawala ili awe karibu na chungu.
 
Haja quote na Bible au Quran kweli huyu mbabaishaji ?
 
Wazee kama hawa ndio walitufikisha kama Taifa lililokwama kiuchumi,kidemokrasia.

Kama kuna vijana wa oya,kwanini kusiwe na wazee wa......
 
Kwenye kampeni alikuwa akidanganya kuwa kwao akina mama hawabebi ndoo za maji kichwani kwani mabomba yametapakaa kijijini kwao, Magufuli anawasalimu yuko ofisini anachapa kazi.
 
Aibu sana eh

Hivi unajisikiaje kupita na vi8

La mln 400 alafu maeneo yako yana shida ya maji

Ova
 
Haja quote na Bible au Quran kweli huyu mbabaishaji ?
Mzee unasikitisha sana. Muda wote umekuwa na madaraka nchi hii, RC Dar mpaka kuwa Katibu Mkuu wa CCm, hukuona kwamba Bumbuli haikuwa na maji ndio umeona sasa yakitoka!!!? Shame on u. Tatizo Ni kushangilia shangilia tu na kulamba asali bila kukumbuka nyumbani. Mzee tulia Tegeta nyuki Makba jr unae.
 
Mzee mwongo sana huyu sijui anaizungumzia Bumbuli ya wapi huyu labda kwao Mahezangulu, Bumbuli kitambo sana maji ya bomba yapo na wala hayakuletwa na Serikali bali wananchi wenyewe walijiongeza.
Mkuu haka kazee kanafiki sana, hapo anaposema ni kwao Mahezangulu..hovyo kabisa.
 
!!! Mwanaye alikuwa anafanya nini bungeni kama bumbuli maji hayakuwepo?
 
Ni hatariiii Sana mzee kama hiyo kuongea uongo
Wajukuu watamdharau
 
Miaka yote hiyo ilikuwa na nafasi ya kuyawezesha hayo Leo unakuja na utumbo hapa. Mlikuwa mnalamba asali tuu Kwa matumbo yenu. CCM ukoo wa panya buku.!!
Mzee wa dili
Hujasikia kule club house walivo piga dili akiwa kiongoz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…