Elections 2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

Elections 2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

Wapumbavu na malofa waliopoteza wapendwa wao kwa kukosa hela ya kuhonga hospitalini!
 
ila issue ya kuweka namba hapa sio nzuri sana

Mods wa hii forum hawaaminiki kabisa

wape watu email yako na wakutumie huko

Au toa ya kwako watu wakutumie huko boss
 
Wapumbavu na malofa waliopoteza wapendwa wao kwa kushinda kumudu gharama za matibabu!
 
That is too LOW from you..again.
Lazima uwavutie watu wajadili sera zako ili zifahamike na wengi na watu wajue umejipangaje.
Lodilofa amesababisha watu wasijadili sera wala shopping list yake. Hiyo sio positive point unless you encourage watu kumpitisha mtu wasiejua anataka kufanya nini KIPYA na kwa namna gani ambayo wenzake walishindwa.

Shopping list yake ni ileile ya Mkapa na JK, 20 years ago, na anashangaa kwamba hayo hayajafanyika.

Atueleze....Afya vipi?...., dispensary nchi nzima anafikiri ni sawa na peremende?
View attachment 280076

Safi kabisa mkuu

Naomba niibe picha yako tafadhali niitume kwenye magroup mia sita

na kwenye kila thread ya mafisadi
 
Hivi mkiitwa wapumbafu na malofa mtakataa? Mnatumia mda mwingi kujadili maneno mawili ya Nkapa badala ya kujadili hoja za Magufuli, au mmeona kuongea point tupu mmekosa cha kumkosoa?Punguzeni ULOFA basi

Malofa ni wananchi wote wa kawaida pamoja na wewe. Huo ndiyo ujumbe alioutoa Mzee Nkapa kama hukuupata sawasawa. Sasa wewe unatukanwa kwa vile tu uko CCM huoni kuwa umetukanwa. Poor you ... Wewe utakuwa ni zaidi ya Lofa!!
 
Ni msemo ulitolewa na Mzee Mkapa katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CCM.

Tangu kutolewa msemo/sifa/tusi hili, nimejaribu kupitia katika mitandao mingi ya kijamii...nimeona watu wengi mpaka wagombea wa udiwani na ubunge kupitia ukawa wakijadili "sifa/tusi" hili kwa wingi sanaaa (posts/ comments).

Tumejikuta tukisahau, dhima, malengo, mikakati, sera, taratibu na mambo mbalimbali ya kuwaeleza wananchi juu ya ukawa.

Tunamaliza muda mwingi kujadili hoja ya sifa/ msemo wa mzee huyu. tukiacha kutambua muda wa kampeni ni mchache sanaa wao wameanza kuzurura sasa mikoani...sisi tunashinda kwenye mitandao tukisema tuuuuuuu, wakat ni 15% ya watanzania wenye sifa ya kupiga kura ndio utumia mitandao.

Mwisho naomba turudi kwenye kuelemisha mwananchi nia ya ukombozi wa pili kupitia ukawa.
 
attachment.php
 
Hofu ya watawala wetu ccm; Wapo radhi kufanya chochote ili mradi waendelee kuwepo madarakani kwasababu ya kulinda masilahi yao ya utajiri waliojilimbikizia kwa sababu wanahofu upinzani ukishika dora wa watachukuliwa hatua za kisheria.
Hofu ya Makada wa ccm wanaokihama chama kwenda upinzani inawanyima usingizi hofu inapanda maana hawa makada walikuwa ni viongozi wakubwa ndani ya serikali ccm wanayajua mambo mengi ni jinsi gani taifa linaibiwa wanainchi tukiachwa masikini wakutupwa na watoto wa vigogo wakineemeeka na kutunza fedha ughaibuni.
Kauli (wapumbavu na malofa) ya Rais msitaafu benjamini w mkapa nikauli ya kihuni ambayo haipaswi kutolewa na kiongozi mkubwa kama yeye.
WATANZANIA TUBADILIKE TUNAHITAJI MABADILIKO YA KIMFUMO SERA ILI TWENDE NA WAKATI TANZANIA BILA CCM NI TANZANIA MADHUBUTI ITAKAYO WAJALI WOTE NA KUGAWANA SUNGURA WETU KWA MLINGANYO SAHIHI MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA
 
Jana mzee Mkapa alimwaga radhi, CCM nayo ikamwaga radhi.

Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, alipopata wasaa wa kuhutubia maelfu ya wanachama wa CCM waliokuwa uwanjani wa Jangwani, alirusha kijembe kwa wapinzani na kusema wanaosema wanatafuta ukombozi ni wapumbavu na malofa.

“Kuna vyama vinajifanya vinataka kuleta ukombozi, ukombozi uliletwa na ASP na TANU, hao wanaojiita vyama vya ukombozi ni wapumbavu, … ni malofa, nchi hii ilikwisha kombolewa na sasa inaendelea kuikomboa kwa kupambana ana umasikini, ujinga na maradhi na ndo kazi imekuwa ikifanywa na serikali zote zilizopita kuanzia ile ya awamu ya kwanza na hii inayokuja itafanywa na serikali ya Dk. Magufuli,” alisema.

Mzee niliyemzoea kwa hoja zenye mashiko na takwimu akageuka mlevi asiyejiheshimu.

Kweli ufalme wa CCM umefitinika.Kati ya mambo ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakiitofautisha brand ya CCM na Upinzani ni kule kutumia lugha zenye staha,kuhubiri amani na kuiishi.Jana rasmi CCM imevunja ndoa yake na sifa hizi.

Sasa tunaanza kupata picha tukimtazama Makonda, baadae Nape,Wasira,Kamani,Job Ndugai na sasa Mkapa tunaona CCM mpya inayozaliwa; brand ya ngumi,matusi na lugha za mihemko.

Mimi niwaambie tu,busara na hekima ni tunu ila ujinga hafundishwi mtu.Ni suala la kuamua tu!

Magufuli karibu UKAWA,you are a good manager but not a leader.

BURIANI CCM!



AqHkJ5rEwFO_ZNrUHijKrDNxdNZz2VrN9GFjD9U0kexD.jpg
Nakuongezea na wewe acha upumbavvu maana una ugonjwa wa kusahau mpumbavu mkubwa tena uwe na heshima kwa viongozi wako inaonekana wewe hata wazazi wako umewashinda
 
Last edited by a moderator:
Hofu ya watawala wetu ccm; Wapo radhi kufanya chochote ili mradi waendelee kuwepo madarakani kwasababu ya kulinda masilahi yao ya utajiri waliojilimbikizia kwa sababu wanahofu upinzani ukishika dora wa watachukuliwa hatua za kisheria.
Hofu ya Makada wa ccm wanaokihama chama kwenda upinzani inawanyima usingizi hofu inapanda maana hawa makada walikuwa ni viongozi wakubwa ndani ya serikali ccm wanayajua mambo mengi ni jinsi gani taifa linaibiwa wanainchi tukiachwa masikini wakutupwa na watoto wa vigogo wakineemeeka na kutunza fedha ughaibuni.
Kauli (wapumbavu na malofa) ya Rais msitaafu benjamini w mkapa nikauli ya kihuni ambayo haipaswi kutolewa na kiongozi mkubwa kama yeye.
WATANZANIA TUBADILIKE TUNAHITAJI MABADILIKO YA KIMFUMO SERA ILI TWENDE NA WAKATI TANZANIA BILA CCM NI TANZANIA MADHUBUTI ITAKAYO WAJALI WOTE NA KUGAWANA SUNGURA WETU KWA MLINGANYO SAHIHI MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA
 
Hofu ya watawala wetu ccm; Wapo radhi kufanya chochote ili mradi waendelee kuwepo madarakani kwasababu ya kulinda masilahi yao ya utajiri waliojilimbikizia kwa sababu wanahofu upinzani ukishika dora wa watachukuliwa hatua za kisheria.
Hofu ya Makada wa ccm wanaokihama chama kwenda upinzani inawanyima usingizi hofu inapanda maana hawa makada walikuwa ni viongozi wakubwa ndani ya serikali ccm wanayajua mambo mengi ni jinsi gani taifa linaibiwa wanainchi tukiachwa masikini wakutupwa na watoto wa vigogo wakineemeeka na kutunza fedha ughaibuni.
Kauli (wapumbavu na malofa) ya Rais msitaafu benjamini w mkapa nikauli ya kihuni ambayo haipaswi kutolewa na kiongozi mkubwa kama yeye.
WATANZANIA TUBADILIKE TUNAHITAJI MABADILIKO YA KIMFUMO SERA ILI TWENDE NA WAKATI TANZANIA BILA CCM NI TANZANIA MADHUBUTI ITAKAYO WAJALI WOTE NA KUGAWANA SUNGURA WETU KWA MLINGANYO SAHIHI MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA
Amen, mungu ibariki people's power.
 

MALOFA wote na WAPUMBAVU wote, Tuhakikishe ULOFA na UPUMBAVU wetu unakuwa Historia Jumapili ya Oktoba 25, 2015

Kuna msemo unasema 'Do not underestimate the power of stupid people in large groups', Ninaimani Mkapa aliyakumbuka haya kabla ya kuita watu ni wapumbavu na malofa!
 
Mpumbavu na Lofa ni yule aliyeuza Benki kwa bei ya kutupa!
 
Salaam.

Kampeni za uchaguzi zimefunguliwa na sasa Kumekucha Tanzania!

Nipende kuwapongeza wanaCCM kwa kufungua rasmi kampeni yao hapo jana (23.08.2015) lakini kwa namna mpya ya kejeli, vijembe, matusi(vilivyokataliwa na tume) kutawala ufunguzi huo. Nilishtushwa na kauli za viongozi wa CCM kama vile Mh. Benjamin W. Mkapa kutukana hadharani. Mengi yamesemwa ikiwa ni pamoja na kusema "upumbavu na ulofa" si tusi. Nabaki najiuliza hata kama si tusi hakuna maneno makali ya kutumia tofauti na hayo, hasa kwa Rais mstaafu? Nakumbuka Mh. Tundu Lissu aliwahi kutamka maneno hayo Bungeni(haikuwa hekima), kwa kuwa alikosea basi ndiyo inahalalisha matumizi yake? leo inaonekana kama mtindo!

Wazungu wanasema 'Great minds discuss ideas, average minds discuss events and small minds discuss people" Nilitegemea kwa kikosi kile pengine kutoa maneno ya busara na kutofanya kuwa kijiwe cha chuki kwa waliokatwa.(wakiwakejeli wakiokatwa, na baadhi ya waliokatwa walio ndani ya CCM kumalizia hasira zao pale kwa kuwa walikatwa)!

Wengi wa viongozi hawa hawajui maisha halisi ya mtanzania wa chini(Kama wanajua wanajua kwa namna kufikirika tu), leo hii hawa ni watu wa kufanyiwa hivi

Kauli kama "Wapigwe tu...",

"Wapinzani(Waliokwenda Upinzani) ni wapumbavu na malofa",

"Mil. 10 ni fedha ya mboga tu",

"Mkishindwa kulipa nauli mpige mbizi",

"Tutashinda tu hata kama kwa goli la mkono" na aina nyingine nyingi ya matusi, kejeli na dharau vinamdhalilisha mwanananchi!

Ninahitaji Kiongozi anayesimamia sheria, inaposemwa mwisho wa mkutano ni saa kumi na mbili jion(saa 12:00), basi na iwe hivyo lakini si saa 1231!

Ninahitaji kiongozi mwenye busara katika matamshi ya maneno na mwenye kuulinda ulimi wake!

Nahitaji kiongozi mwenye kunadi ilani yake, sera zake kwa umakini na namna nitakayoelewa na si kuponda upande mwingine(wa pili) kwasababu ya umasikini wa hoja anazoshindwa kutoa.


Tatizo wengi wa viongozi wanadhani "immunity" waliyonayo inawakinga na UHAI wao! Wananchi pia wana 'threshold' yao ya uvumilivu na hasira. Niwakumbushe tu kuwa kulikuwa na viongozi makini sana 'Nchi za watu' waliouawa tena wakiwa na Ulinzi wa kutosha kwa sababu ya kauli mbovu tu pamoja na umakini wao. Tena kwa sisi na vijana wetu(waliokwenda jeshi) na hawana ajira(ninyi mwawaita vibaka), watakaowa-assassinate, mmoja baada ya mwingine ndipo mtakapotambua 'maskini jeuri' wa nchi hii.

Wengi wanadhani bado wanaweza kupumbaza watu kwa vyombo vya habari vya ndani(Local Media) lakini niseme Afrika Mashariki sasa inaona Afrika na Dunia nzima sasa inaona kinachoendelea Tanzania(ikitazama Viongozi wakubwa wakitukana hadhari, wakistaajabu aibu kubwa ya viongozi kujiandaa kusimama kuponda upande wa pili bila ya wao kuwa na hoja).

Kwa sasa ilani ya CCM imekuwa ni UKAWA, Hoja zao ni UKAWA. Bila UKAWA CCM haitaweza kuwepo!

Hivyo basi mimi na upumbavu, ulofa wangu nikiwa 'kibaka' na 'mnywa viroba' nitaisubiri Oktoba 25, 2015 kwa Mapenzi ya MUNGU kuonyesha ubora wangu na kichinjio changu.
Hizo in dalili za utawala uliochoka kumbuka hata gadafi alifikia hatua ya kuwaita wananchi wake panya
 
Ndugu zangu watanzania,

Katika hali ya ubabe wa viongozi wa CCM na kwa kuwa wanaogopa kama wakitoka madarakani huenda wakafikishwa katika mahakama ya AICC au the Hague.

Kwa mara ya kwanza Kikwete alisikika akilalamika kwa nini mahakama ya AICC inawashughulikia viongozi wa nchi za Africa tu?! Mbona hajaona hata kesi moja inayomuhusu kiongozi wa nchi za Ulaya?!

Lakini katika kutilia mkazo kauli hiyo Rais wa Awamu ya tatu katika serikali ya Jamhuri ya Muungano Ndugu Benjamini W. Mkapa ambaye na yeye ana kashfa nyingi za kujilimbikizia mali. Ndiyo katika kuona hali ya kupelekwa AICC haiepukiki ameamua kufyatuka (sijui alikuwa kisha weka spirit kichwani?) na kuwaita wale wote wanaopigania raslimali za nchi kutumiwa na wanachi ni WAPUMBAVU NA MALOFA.

Nijuavyo mimi;

MALOFA ni watu wasiojua hali yao ya baadae kimaisha itakuwaje kwa upande wa KULA, KUNYWA, MAVAZI na HUDUMA ZA KIJAMII KWA UJUMLA.

WAPUMBAVU ni watu wanayeshindwa kuelewa jambo hata akielezwa, juha, zuzu, jura, nyange, baghami, bahau, hambe, maarasi, zebe, mbumbumbu.

ASUBUHI NJEMA

WAPUMBAVU NA MALOFA WENZANGU.
 
Back
Top Bottom