Elections 2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

Elections 2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

Kitu ambacho kinawapa shida ccm toka enzi za mwalimu nyerere ni demokrasia na ukifuatilia kiundani zaidi utagundua hata nyerere mwenyewe huruhusu vyama vingi alilazimishwa ila sio kwa kupenda

Mm naona wakina mkapa ndio wapumbavu wakati mfumo wa vyama vingi unaanzishwa wenyewe walikuwepo na walikua wanafanya kazi serikilini inamaana hadi walikubali vyama vingi viwepo walikua hawajui kwamba ni upumbavu na kama wenyewe ndio walihusu huo upumbavu basi wenyewe ccm ndio wapumbavu walitengeneza mtego wenyewe na umewashika wenyewe maisha ndivyo yalivyo
 
Sasa hivi "wapumbavu na ulofa" ndiyo wimbo kila sehemu. Kwanini hatupewi ilani zao ili tubadilishe wimbo huu!
 
Tatizo magufuli alikuwa mtu wa mkapa kwenye uchaguzi wao wa dodoma, alimpigia debe hadi akaibuka kidedea. Sasa asipokuwa rais itaonekana yeye ndio amekiangusha chama. Ndio maana ana hasira kali kwa lowasa/ukawa anaona wanataka kumuharibia. Kumbe ndio anamuharibia mtu wake.
 
Sasa hivi "wapumbavu na ulofa" ndiyo wimbo kila sehemu. Kwanini hatupewi ilani zao ili tubadilishe wimbo huu!

Wakishindwa kutekeleza hiyo ilani # post25oct ,inabidi tunanyamazie tu ,maana tukiwauliza watasema twende mahakamani.
 
Mpumafu huwajuwa wapumbafu wenzie,

Mpumbafu wa kwanza Tanzania alipachikwa nafasi ya urais mwaka 1995, wa pili alitoa matusi kwenye mkutano na watatu aliwakaribisha wawekezaji wanaoiba rasilimali zetu.

TANZANITE: Inatoka kwetu (Tanzania tumeuza 35bil, Kenya 300bil na India 500bil) zote hizi huchimbwa kwetu la ajabu wale tuliowaita na kuwagawia vitalu wanafaidi kuliko wazawa!

SHAME ON YOU!
 
Hivi mkiitwa wapumbafu na malofa mtakataa? Mnatumia mda mwingi kujadili maneno mawili ya Nkapa badala ya kujadili hoja za Magufuli, au mmeona kuongea point tupu mmekosa cha kumkosoa?Punguzeni ULOFA basi
Tatizo lako wewe ni mvivu wa kusoma na kufikiri! Jaribu kusoma hiki kigongo cha mkuu sana Mag3
John Joseph Pombe Magufuli kwa mara ya kwanza aliteuliwa na Raisi Benjamin William Mkapa kuwa Waziri mdogo wa Ujenzi mwaka 1995 hadi 2000 alipoteuliwa kuwa Waziri kamili wa Ujenzi. Wadhifa huo aliendelea nao hadi mwaka 2006 alipoteuliwa na Raisi Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Waziri wa Ardhi na Nyumba mwaka 2006.

Mwaka 2008 aliteuliwa kushika wadhifa wa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi hadi mwaka 2010 alipohamishiwa tena Wizara ya Ujenzi. Kwa kifupi ni kwamba John Pombe Magufuli ameshikilia nyadhifa mbali mbali ngazi ya Uwaziri kwa kipindi cha miaka ishirini katika awamu zote mbili toka tuingie kwenye mfumo wa vyama vingi.

Kwa miaka kumi na tano John Pombe Magufuli ameshiriki katika vikao vyote vya Baraza la Mawaziri na ameshiriki katika vikao vyote vya juu vya chama tawala CCM. Kwa maneno mengine ni kwamba hakuna maamuzi serikali ilichukua wala mikataba serikali iliingia bila ushiriki wa John Pombe Magufuli ama moja kwa moja au kwa kuwakilishwa.

Ni katika kipindi hiki cha miaka ishirini ndipo tumeshuhudia mambo ya ajabu kweli kweli ndani ya taifa hili, tumeshuhudia kashfa baada ya kashfa hadi neno hili limepoteza maana. Pia ni katika kipindi hiki tumeshuhudia uvunjaji wa katiba na vyombo ambavyo vilitakiwa kuilinda na kuitetea katiba lakini hakuna hatua iliyochukuliwa dhidi ya wahusika.

John Pombe Magufuli kwa sasa ameteuliwa kuwa mgombea wa Uraisi kupitia CCM na moja katika ahadi zake za mwanzo kabisa ni kuendeleza walikofikia waliomtangulia. Sera anazoahidi kuzitekeleza ni zile zile za waliomtangulia lakini cha ajabu ni pale anapotuomba wananchi kumuamini kwa kuwa yeye, tofauti na waliomtangulia, ni mtendaji.

Mpaka hapo sina ugomvi na John Pombe Magufuli lakini ugomvi wangu naye unakuja pale anapoanza kushangaa kama vile hajawahi kuishi hapa nchini. John Pombe Magufuli anashangaa tulivyoweza kufika hapa tulipo, anashangaa chombo gani hicho kimetufikisha hapo na kwa nini wananchi tulikubali tufikishwe hapo na chombo hicho.

John Pombe Magufuli anashangaa tembo wetu kuuawa na pembe kusafirishwa kwa ndege kwenda China,
anashangaa nchi kukosa hata kiwanda kimoja cha Kusindika nyama na samaki, anashangaa wauzaji wakubwa wa Tanzanite kuwa Kenya na India, anashangaa hospitali zetu kukosa dawa hadi viongozi wanakimbilia kwa babu kupata kikombe au Ulaya kwa matibabu...

John Pombe Magufuli hakushangaa alipokuwa Waziri, hakushangaa alipoenda Samunge kubugia kikombe, hakushangaa alipouza nyumba za serikali, hakushangaa ripoti ya CAG ilipomtuhumu na upotevu wa mabilioni, hakushangaa alipovunja makazi ya watu na kuwaacha "homeless", hakushangaa wezi wa EPA walipoombwa kurudisha walichokwiba, hakushangaa...

John Pombe Magufuli hakuweza kuuliza kulikoni akiwa kwenye Baraza la Mawaziri, akiwa na Mwenyekiti wake wa chama, akiwa na watendaji wenziwe serikalini na wizarani, akiwa kwenye kikao cha Kamati Kuu...hapana alisubiri siku anapewa upendeleo maalum kupeperusha bendera na kuomba kura zetu, ashangae waliyoyatenda wakiwa madarakani.

John Pombe Magufuli anataka kuwa Raisi wa nchi hii awamu ijayo, anataka tuamini kuwa wengine wote wanaoomba nafasi hiyo hawafai akiwatuhumu kuwa na uroho wa madaraka. Kwa miaka ishirini amekuwa sehemu ya uozo tunaotaka kuuondoa lakini leo ana ujasiri wa kutuomba tumuamini, anaahidi kutotuangusha na kweli wapo wanaopiga vigelegele!

Wanawakandia waliofunguka macho na kuachana na genge lao, wanawatukana wananchi waliowachoka, wanawakebehi wasiokubaliana na unafiki wao, wanaapa hawaachi madaraka hata kwa miaka mia, wanatamba vyombo vyote vya dola wanavimiliki na wanadai ushindi ni wao hata kwa goli la mkono! Wanachosahau ni ni kuwa historia haiko upande wao!

 
Ninaomba Moderators msiutoe huu uzi wala kuuunganisha.

Angalizo: Uzi huu nimecopy toka mchango wa mdau mmoja humu jf anayetumia ID K.Msese

[h=1]Mada moto live on Channel Ten: Yaliyojiri mwisho wa wiki kuelekea uchaguzi mkuu[/h]Dhumuni langu ni ujadiliwe kama Tread iliyosimama yenyewe kwani mm binafsi nimeona umuhimu huo naimani nawe pia utaona hivyo.

Jisomehe mwenyewe.


>>>>>nimeyatoa haya maeno kuleeee/........


Aliyeitwa msafi, ndiye aliingia Ikulu na kuanza kutelekeza usafi. Akaanzisha kampuni ya biashara – ANBEM Co. Limited – kwa kutumia rasimali za umma.


----------- Akabinafsisha mashirika ya umma, mithili ya shamba lisilo na mwenyewe.

------------ Akaruhusu na, au kunyamazia ukwapuzi wa mabilioni ya shilingi serikalini na ndani ya Benki Kuu ya taifa (BoT).

------------- Miongoni mwa fedha zilizoibwa, ni pamoja na zile zilizochotwa kupitia akaunti ya madeni ya nje (EPA), katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2005.

----------- Hapa ndiko kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd., ilipewa “zawadi” ya kiasi cha Sh. 70 bilioni kati ya Sh. 130 bilioni zilizochotwa BoT.

------------ Ushahidi juu ya Mkapa kushiriki au kunyamazia wizi katika akaunti ya EPA, uliwekwa hadharani na Bhyidinka Michael Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi Law Chambers ya Dar es Salaam.

---------------- Sanze ndiye alishuhudia mkataba kati ya Kagoda na serikali. Wakili huyo anakiri kuwa ni yeye aliyeshuhudia mikataba ya Kagoda na makampuni mengine ya nje.
--------------
--------- ------Mbali na fedha zilizoibwa katika akaunti ya EPA, mabilioni mengine ya shilingi yalikwapuliwa na makampuni ya Tangold Limited, Deep Green Finance Limited, Meremeta na Mwananchi Gold Ltd.
-------- Hakuishia hapo. Ni Mkapa aliyeingiza nchini kampuni ya kigeni kutoka Afrika Kusini – Net Group Solutions – ili kuikabidhi shirika la umeme la taifa (Tanesco), kuvuna wasichopanda.

-------------------- Kazi ya Net Group ndani ya shirika la umma, haikuwa kuzalisha; kuwekeza mtaji; au kutafuta vyanzo vipya vya umeme. Kazi ya kampuni ya “makaburu’ ilikuwa kukusanya mapato na kukamua wananchi.

------------ Katika kipindi cha miaka saba ya mkataba kati ya serikali na Net Group, Tanesco ikashindwa kuzalisha umeme unaoendana na mahitaji. Ikashindwa kuwekeza katika miradi mipya ya umeme.

--------------- Matokeo yake, miundo mbinu ya umeme ikachakaa. Taifa likatumbukia katika giza la milele na milele. Tanesco iliyokuwa imara, haraka ikatumbukia katika mikataba ya kinyonyaji ya kuzalisha umeme wa dharula.

------------ Tanesco iliyokuwa inajiendesha kwa faida, ikatumbukia katika madeni makubwa yanayohatarisha hata uhai wa shirika lenyewe.

----------------- Miongoni mwa mikataba ya kinyonyaji ambayo imefungwa kutokana na shirika kutafunwa na kampuni iliyoletwa na Mkapa, ni pamoja na mkataba wa kinyonyaji wa kuzalisha umeme wa Richmond na dada yake Dowans.

------------------ Makampuni mengine, ni Aggreko; Symbion; Songas na “ndoa ya mkeka” iliyofungwa kwa mara ya pili kati yake na kampuni ya Independent Powel Tanzania Limited (IPTL).

--------------- Mkataba wa kwanza kati ya IPTL na serikali ulifungwa Septemba 1994. Katika mkataba huu, serikali ilijifunga kulipa IPTL kiasi cha Sh. 6 bilioni kwa mwezi kwa umeme usiokuwepo.

--------------- Januari mwaka huu, mkataba mpya kati ya Tanesco na IPTL kupitia anayeitwa mmiliki mpya, kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP), ulifungwa katika mazingira yaliyosheheni utata.

------------- Taarifa zinasema, mkataba kati ya Tanesco na PAP, hauna tofauti yoyote kubwa na mkataba kati ya Tanesco na IPTL.

----------------- Ni Mkapa na utawala wake waliobinafsisha mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya na kuumilikisha kwa watu waliokaribu na rais. Bunge la Jamhuri lilielezwa na Mtendaji Mkuu wa Kiwira Coal and Power Limited (KCP), Francis Tabaro, kuwa mgodi huo ulikuwa ukimilikiwa na watu walio karibu na Mkapa.

--------------------- Waliotajwa kwa mujibu wa taarifa hizo, ni mtoto wa kuzaa wa Benjamin Mkapa, Nick (Nicholas) Mkapa na mkewe Foster Mkapa. Hawa wanamiliki kampuni ya Fosnik Enterprises, moja ya makampuni yanayomiliki mgodi.
-------- Mkurugenzi mwingine ambaye pia ni mmiliki ametajwa kuwa ni D. Maembe.

-------------------- Kampuni ya Mkapa ni miongoni mwa makampuni manne yaliyoungana na “kumilikishwa” mgodi wa Kiwira ambao ulikuwa mali ya serikali kwa asilimia 100. KCP ilianzishwa Julai 2005.

--------------- Si hayo tu. Akiwa ikulu ya magogoni, Mkapa alimpa mkewe, Anne Mkapa, mamlaka ya kukusanya fedha na kuendesha kinachoitwa, “Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote” (EOTF). Akautumia mfuko huo, kujilimbikizia mali nyingi.

----------------- Hadi wanaondoka ikulu, siyo Mpaka wala mkewe, aliyesema fedha za kuendesha mfuko ya EOTF zilitoka wapi. Mafanikio yaliyofikiwa wala hesabu za mfuko ni siri yao.

-------- --“Mfuko wa Mama Mkapa,” ulianzishwa mara baada ya Mkapa kuingia madarakani, Novemba 1995. Kwa muda wote ambao Mkapa alikuwa ikulu, mfuko huu ulikuwa unaendeshea shughuli zake katika majengo ya Ikulu.

--------------- Hata gharama za bili ya maji, umeme, simu na mishahara ya wafanyakazi vililipwa na serikali. Misaada na michango iliyotolewa na wafadhili, mingi ilitolewa kwa kuwa mwenyekiti wake ni mke wa rais. Mfuko uligeuka, ingawa siyo rasmi, kuwa wa umma.

------------------ Hakika, kuna mengi yamefanyika chini ya utawala wake. Ameingiza nchi katika mikataba ya kinyonyaji katika uchimbaji madini katika maeneo mbalimbali nchini, ukiwamo mgodi wa Tulawaka, Bulyanhulu, North Mara na Geita Gold Mine.

---------------- Ameuza nyumba za serikali. Naye akajimilikisha baadhi ya nyumba hizo. Akaruhusu waziri wake, John Pombe Magufuli, naye kujimilikisha.

----------- Akasimamia uuzaji unaofanana na utoaji bure mashirika ya umma, ikiwamo “utoaji bure” iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC). Benki iliyokuwa na matawi nchi mzima na mtaji kedekede, iliuzwa kwa bei ya kutupwa kwa benki ya ABSA ya Afrika Kusini.

----------------- Leo hii, NBC iliyoelezwa inauzwa kwa watu wenye uwezo wa kuiendesha kuliko wazalendo waliopo, iko hoi kibiashara. Imepoteza mtaji; na sasa inaendeshwa kwa hisani ya BoT.

---------------- Ni Mkapa aliyeuza shirika la ndege la taifa (ACT); migodi na mashamba.

-------------- Katika muktadha huo, mtu mwenye yote haya, anapata wapi uhalali na ujasiri wa kutupendekezea mtu ambaye anadai ni mwadilifu? Mtu mwenye viwango vya chini vya uadilifu kama Mkapa, anawezaje kumjua mwadilifu wa dhati? Hawezi.

-------------- Ni bahati njema kuwa Nyerere alifariki dunia kabla Mkapa hajamaliza ngwe yake ya kwanza ya uongozi, Oktoba 2010. Vinginevyo, asingeruhusu Mkapa kushika madaraka kwa vipindi viwili mfululizo. Nyerere alifariki dunia 14 Oktoba 1999.

----------- Taarifa zinanukuu baadhi ya viongozi waandamizi nchini wakisema, Nyerere alikuwa amejiapiza kumzuia Mkapa kuwa rais kwa kipindi cha pili. Alimchoka.

------------- Hivyo basi, tukimjadili Mkapa na yule anayempigia chapuo, tunawaona wana sifa moja inayofanana. Wote wawili hawaheshimu utawala wa sheria. Ni wababe.

----------------------
-------------------------------- Katika kipindi cha utawala wake, Mkapa aliruhusu vyombo vya dola – jeshi la polisi; vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) vya Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU); Kikosi cha Kuzuia Magendo (KMKM) na makundi mengine ya Janjaweed – kuendesha mauaji makubwa katika Visiwani Pemba na Unguja, 26 na 27 Januari 2001.

-------------- Katika tukio hilo lililoweka doa baya taifa hili, wanakaokadiriwa kati ya watu 30 na 75 waliuawa.


----- ----------Anajua ikiwa Magufuli atafanikiwa kuwa rais, atamburuza. Atamyumbisha. Anajua chini ya Magufuli machafu yake yatalindwa. Nje ya hapo, Mkapa hana kingine cha kumsifia Magufuli.

------------ Tusikubali kuruhusu kuchaguliwa mgombea, kabla ya kukubaliana juu ya sifa za rais tunayemhitaji

Mwandishi wa Makala hii anaitwa KAROLI VINSENT anapatikana kwa namba
 
Tunaimani na magufuli katika uchapakazi,uadilifu na ufuatiliaji.......tumchague magufuli hao wengine wanamatatizo mengi katika ufanyaji kazi wao,
 
Ukawa mna kila sababu za kuitwa wapumbavu, u deserve it. Mna sifa za kuwa wapumbavu.
Mpumbavu ni mtu ambaye hafundishiki, haelewi, na wala hafikirii, yye huamini kile akijuacho tu.
Kuamini kuwa mtaitoa ccm madarakaki ili kuleta mabadiliko, ilihali mkiwatumia makada hao hao wa Ccm, huo ni upumbavu.
Kumpa huyo papa nafasi ya kugombea urais akiwa na wiki 1 ndan ya chama, upumbavu huo.
kumwacha Slaa kisa huyo papa, msaliti, tapeli, mwizi, mzandiki, upumbavu huo.
Najua hoja zangu ztapingwa kwa matusi, kwa 7bu nyie ni mapumbavu.
Hebu sasa tuuone upumbavu wenu hapa kupitia matusi.👍☝👍👍👍👍

Ndugu yangu kuna msemo wa Kiswahili unasema 'Nyani haoni..........!' Lakini tatizo Siyo wewe peke yako, Mkapa, CCM, UKAWA na Watanzania wengi hawana uzalendo, tunashindwa kujua vyama ni vya mpito lakini Tanzania tutakua nayo siku zote. Kama upumbavu ni kutokuona hoja za wengine, afu wewe huzioni za wenzako, huoni kama unajijumuisha! Tuheshimiane na kuheshimu utu maana tusipo fanya hivyo tutakufuru!
 
Ni Hatareeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee, Wazee Hawa Tuwaombe Tu Wapumzike Kimya Kimya, Vinginevyo Watoto Na Wajukuu Zetu

Wakismuliwa Madudu haya Watatafuta Makaburi yao Ili Wamalizie hasira zao Kwa Kutandika Mifupa yao Fimbo.
 
Wapumbavu na malofa tukutane hapa. Tuzungumzie namna ya kujikomboa na kukomboa taifa letu linalodhihaki na tuliowapa dhamana ya kutuongoza.

Tutaweka na picha zikiwaonyesha watoto wa wapumbavu na malofa wakisoma nchi ya mti!

Wakigombania tundu moja la choo mashuleni!

Wakipewa daraja la div 5 katika ufaulu!

Wakisoma kwa taabu sana na mwishowe kukosa ajira!

Tukutane hapa tafadhalini!

Tupia namba yako ya whatsapp niku add kwenye group la wapumbavu na malofa!

Karibuni!
 
Wapumbavu na malofa wanaopata mlo mmoja kwa siku tena kwa magumashi!
 
Safi sana...wacha October wataona upumbavu wetu ulivyo
 
Mkapa mjanja sana kawapoteza maboya kabisa! Hadi kampeni zinaisha watakuwa wanajadili maneno mawili tu yaani Pumbavu na Lofa huku Magufuli akichanja mbuga.
That is too LOW from you..again.
Lazima uwavutie watu wajadili sera zako ili zifahamike na wengi na watu wajue umejipangaje.
Lodilofa amesababisha watu wasijadili sera wala shopping list yake. Hiyo sio positive point unless you encourage watu kumpitisha mtu wasiejua anataka kufanya nini KIPYA na kwa namna gani ambayo wenzake walishindwa.

Shopping list yake ni ileile ya Mkapa na JK, 20 years ago, na anashangaa kwamba hayo hayajafanyika.

Atueleze....Afya vipi?...., dispensary nchi nzima anafikiri ni sawa na peremende?
Tanzania Hospitals.jpg
 
Wapumbavu na malofa walioshindwa kuendelea na masomo yao kwa kukosa ada!
 
Back
Top Bottom