Heshima yenu wanabodi!
Nimesikitishwa sana na kitendo cha Rais wa tatu wa Tanzania Mh.Benjamin Mkapa kuporomosha matusi jukwaani badala ya kujenga hoja!
Mkapa amekuwa mtu wa kupanic sana tangu alipokuwa Rais,aliwatukana waandishi wa habari wa Tanzania hadharani na kuwaita wasiofaa huku akiwakumbatia waandishi wa nje.
Wakati wa kampeni za ubunge jimbo la arumeru mashariki Mkapa pia aliporomosha matusi kwa wapinzani badala ya kujenga hoja matokeo yake Chadema ilishinda asubuhi na yeye kukimbilia uwanja wa ndege na kuondoka mapema sana asubuhi!
Mkapa amerudia kuporomosha matusi jana kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM na kuwaita watu malofa na wapumbavu! Hivi mh.Mkapa pamoja na kukaa ikulu miaka kumi anashindwa kujenga hoja kweli na anaamua kutumia matusi kama sehemu ya kampeni kweli?
Wapinzani fanyeni kampeni ya kistaarabu acheni kujibu matusi ya Mkapa,waelezeni watanzania mtawafanyia nini mkipewa ridhaa,wananchi wanataka maendeleo sio matusi!
Kila la heri UKAWA kila la heri Lowassa na maalimu Seif.